Nchi 10 kati ya 54 za Afrika na 72.19% ya GDP, bado tuna safari ndefu

Nchi 10 kati ya 54 za Afrika na 72.19% ya GDP, bado tuna safari ndefu

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
7,147
Reaction score
14,699
Tumekuwa tukiaminishwa kuwa uchumi wa nchi za Afrika unaendelea kuwa imara; ukuaji halisi unaongezeka, ikiashiria uwepo wa sera madhubuti za uchumi jumla, maendeleo mazuri katika maboresho ya miundo (hususan katika uboreshaji wa miundombinu), na mifumo ya sera nzuri na madhubuti kiujumla. Inawezekana, lakini kwa hii picha hapa chini, eti hizi nchi 10 ndiyo zina uchumi mkubwa Afrika na zinashikilia asilimia 72.19 ya GDP ya Afrika, basi bado tuna safari ndefu.

GDP (Nominal) of Africa 2019.png
 
Hehehehe!! Kweli ni aibu, hili bara sijui nani kaliroga, maana full umaskini na shithole kote ila wabishi kupita maelezo, unakuta mataifa yenyewe yana raslimali na madini ya kumwaga lakini kitakwimu yanatia huruma.
Rasilimali madini hayaozi
Ni asset ya kesho ni suala la muda tu
 
Na tukisema U.S ana Asilimia Over 80 ya GDP bara lake.Wababe lazima wawepo popote pale wametunishia wadogo misuli.Hata ulaya kuna kina Portugal au Luxembourg ana GDP ya $72 Billions ila kuna kina Germany wana $4 trillions.

Ukitaka uisikitikie Africa ni pale nchi moja ya Ulaya inapolingana uchumi na Africa yote au kuizidi.Au pale United States inapotuzunguka mara kumi!
 
Rasilimali madini hayaozi
Ni asset ya kesho ni suala la muda tu

Ya nini kama mwenyewe unajichokea kwa ukata ilhali yanachumwa na wengine, hivi unajua kadiri mabeberu wanachokonoa sayari za mbali iko siku watagundua madini huko nje mara milioni ya haya ya kwetu na mbinu zitafutwe za kuyashusha bila gharama kubwa, tetesi zipo kwamba yalishaonekana huko sayari za mbali, fahamu haya ya Afrika yanapata thamani kwa sababu ni adimu, lakini mabeberu wakiyapata kwingine kwa wingi yatashuka thamani na Waafrika watabadilisha na kulima mihogo.

Kuna hii sayari ambayo inasemekana imejaa dhahabu kila mahali NASA headed towards giant golden asteroid that could make everyone on Earth a billionaire

Wewe endelea kukaa hapo kijiweni ukijiliwaza kwamba madini hayaozi.
 
Sasa nchi kama DR Congo hata hawapo top 10 na jinsi wanazo madini zote na mashamba yenye rutuba. Pia wana watu wengi (labour force). Wapo zaidi ya watu 80 million. Wakiamua kulima hiyo nchi yao kubwa ambayo ina area sawa na western Europe, wanaweza kulisha Afrika nzima.
 
Hehehehe!! Kweli ni aibu, hili bara sijui nani kaliroga, maana full umaskini na shithole kote ila wabishi kupita maelezo, unakuta mataifa yenyewe yana raslimali na madini ya kumwaga lakini kitakwimu yanatia huruma.

Kama Nigeria hapo, kwa takwimu wapo vizuri ila maisha kwa ground ni hovyo kabisa.
 
Ya nini kama mwenyewe unajichokea kwa ukata ilhali yanachumwa na wengine, hivi unajua kadiri mabeberu wanachokonoa sayari za mbali iko siku watagundua madini huko nje mara milioni ya haya ya kwetu na mbinu zitafutwe za kuyashusha bila gharama kubwa, tetesi zipo kwamba yalishaonekana huko sayari za mbali, fahamu haya ya Afrika yanapata thamani kwa sababu ni adimu, lakini mabeberu wakiyapata kwingine kwa wingi yatashuka thamani na Waafrika watabadilisha na kulima mihogo.

Kuna hii sayari ambayo inasemekana imejaa dhahabu kila mahali NASA headed towards giant golden asteroid that could make everyone on Earth a billionaire

Wewe endelea kukaa hapo kijiweni ukijiliwaza kwamba madini hayaozi.
Asteroid Belt very rich in rare metals huko ndio the next frontier kwa Nchi zilozo na akili timamu.

Africa hatuna astrophysicists, elimu Ni ovyo, ufisadi na uzembe Kama kawaida alafu tufikiri kuwa madini yetu yatatusaidia wakati Nchi za Ulaya tayari wamo njiani kufika sayari za Mars na Mwezi wa Jupiter Europa?
 
Asteroid Belt very rich in rare metals huko ndio the next frontier kwa Nchi zilozo na akili timamu. Africa hatuna astrophysicists, elimu Ni ovyo, ufisadi na uzembe Kama kawaida alafu tufikiri kuwa madini yetu yatatusaidia wakati Nchi za Ulaya tayari wamo njiani kufika sayari za Mars na Mwezi wa Jupiter Europa?
Dah! Kila nikifikiria haya mambo nahisi kama volcano inataka kulipuka kichwani kwangu.

Sijui tumekosea wapi!
 
Dah! Kila nikifikiria haya mambo nahisi kama volcano inataka kulipuka kichwani kwangu.

Sijui tumekosea wapi!

Waafrika tutafune vitabu tuache ukajanja mwingi, tuwekeze kwenye elimu na kuhamasisha matumizi ya ubongo, wasomi na wataalam wengi Afrika hawasomi wala kutafiti, wengi wnawaza mkwanja au kupata fursa ya kwenda ughaibuni.

Hamna kitu huniuma unakuta unaandaa bonge la ripoti kisha unapokeza rasimu na kuomba mkutane baada ya wiki muijadili, siku ikifika hakuna aliyesoma hata ukurasa mmoja, wazembe wa kusoma. Maujanja yote haya ya mabeberu yapo kwenye vitabu, wala usihangaike au kuumiza akili, kula "mbuku" tu.
 
Na tukisema U.S ana Asilimia Over 80 ya GDP bara lake.Wababe lazima wawepo popote pale wametunishia wadogo misuli.Hata ulaya kuna kina Portugal au Luxembourg ana GDP ya $72 Billions ila kuna kina Germany wana $4 trillions.

Ukitaka uisikitikie Africa ni pale nchi moja ya Ulaya inapolingana uchumi na Africa yote au kuizidi.Au pale United States inapotuzunguka mara kumi!
South korea peke yake tu ina $1tril.

hiyo ni sawa na mchi zote za africa combined.
 
Kama Nigeria hapo, kwa takwimu wapo vizuri ila maisha kwa ground ni hovyo kabisa.
Ukiangalia sana sana nchi waliojizalia wengi kama panya i.e Nigeria, Tanzania na Ethiopia, wananchi wao wanateseka sana ila Ethiopia sijaona ikiwa na madini ya maana kama Nigeria na Tanzania ambao wananchi wake wanaishi kama mandondocha.
 
ukiangalia sana sana nchi waliojizalia wengi kama panya i.e Nigeria, Tanzania na Ethiopia, wananchi wao wanateseka sana ila Ethiopia sijaona ikiwa na madini ya maana kama Nigeria na Tanzania ambao wananchi wake wanaishi kama mandondocha.

Kwa Afrika ni kawaida tu, maana kwa Tanzania watu ni wengi ila eneo la nchi ni kubwa sana na sehemu nyingine hapajaguswa kabisa. Shida ya hizi takwimu unakuta kuna nchi nyingine zinafanya sensa feki na kuficha idadi ya watu ili zionekane vizuri kwenye makaratasi ila kiuhalisia wanazaana kuliko hata panya. Hii lockdown ime onesha jinsi nchi zinavyozaliana hovyo hovyo hapa Afrika.
 
ukiangalia sana sana nchi waliojizalia wengi kama panya i.e Nigeria, Tanzania na Ethiopia, wananchi wao wanateseka sana ila Ethiopia sijaona ikiwa na madini ya maana kama Nigeria na Tanzania ambao wananchi wake wanaishi kama mandondocha.
Tanzania ina ukubwa wa eneo la kilometa za mraba 947,303 na populations ya 59,734,218

Kenya ina ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 580,367 na populations ya 47,564,296 (sensa 2019)

Hadi hapo tunaona ni nani anazaliana sana na ukumbuke Tz ni kubwa karibu mara mbili ya Ke.

Next time acha kuandika ujinga.
 
Ya nini kama mwenyewe unajichokea kwa ukata ilhali yanachumwa na wengine, hivi unajua kadiri mabeberu wanachokonoa sayari za mbali iko siku watagundua madini huko nje mara milioni ya haya ya kwetu na mbinu zitafutwe za kuyashusha bila gharama kubwa, tetesi zipo kwamba yalishaonekana huko sayari za mbali, fahamu haya ya Afrika yanapata thamani kwa sababu ni adimu, lakini mabeberu wakiyapata kwingine kwa wingi yatashuka thamani na Waafrika watabadilisha na kulima mihogo.
Kuna hii sayari ambayo inasemekana imejaa dhahabu kila mahali NASA headed towards giant golden asteroid that could make everyone on Earth a billionaire

Wewe endelea kukaa hapo kijiweni ukijiliwaza kwamba madini hayaozi.
Kimondo watakimaliza lakini sisi tutakuwa na reserve kwa vizazi vyetu "thats how resource sharing operates" ni ujinga kumaliza kila kitu kwa hofu ya ugunduzi mwingine outerspace.

Na huwezi jua, huenda ikawa ni gold variety isiyofikia thamani ya hii ya Africa.
 
ukiangalia sana sana nchi waliojizalia wengi kama panya i.e Nigeria, Tanzania na Ethiopia, wananchi wao wanateseka sana ila Ethiopia sijaona ikiwa na madini ya maana kama Nigeria na Tanzania ambao wananchi wake wanaishi kama mandondocha.
Nadhani unaongozwa na mihemuko na ushabiki wa Tz vs Ke, huu ni ushabiki mbaya sana maana unakufanya usione mbali na akili yako inakuwa dormant. Unaposema "nchi waliojizalia kama panya" halafu ukazitaja Tanzania na Ethiopia ni kukosa hoja na ni ushabiki uliopitiliza. Kwa Nigeria naweza kukubaliana na wewe kwa kuwa ina ukubwa wa 923,768 km² (ndogo kuliko Tanzania) lakini ina idadi ya watu tariban milioni 200.

Lakini Tanzania ina ukubwa wa 945,087 km² na idadi ya watu (wanaokadiriwa) milioni 58, hii ni nchi kubwa kuliko nchi zingine nne (ukizichanganya pamoja) za Afrika Mashariki: Kenya (580,367 km²) yenye watu milioni 47.56; Uganda (241,037 km²) yenye watu milioni 42.72; Rwanda (26,338 km²) yenye watu milioni 12.3 na Burundi (27,834 km²) yenye idadi ya watu milioni 11.18. Zote kwa pamoja zina idadi ya watu milioni 113.76.

Tukija kwenye population density utagundua kuwa Tanzania ina 62 people per square kilometer; Kenya ina 80 people per square kilometer; Uganda (229 per square kilometer); Rwanda (525 per square kilometer) na Burundi (463 per square kilometer). Sijui hapa wanaojizalia kama panya ni kina nani?

Pia nchi ya Ethiopia ina ukubwa wa 1.104 million km² na ina idadi ya watu milioni 109.2, na ina population density ya 83 people per square kilometer, bado huwezi kusema eti wanazaliana kama panya, labda kama umekosa hoja ya msingi.
 
Back
Top Bottom