Nchi 10 kati ya 54 za Afrika na 72.19% ya GDP, bado tuna safari ndefu

Mbona katik upande wa ges tayari mandaliz y awali ikiw ni pamoj n land aquezation zimefanyik kupisha ujenzi wa LNG....pia swala sio kukimbilia tu uonekane umeanza uzalishaj au exploitation n hizo nature resources but how will it benefit your people and country wise ....so kama haupo sure better wait.... mfano kuna uranium kule ruvuma huwezi sema tukurupuk tu...nimesha shudia ukanjanja mwingi sana kwenye madini mfano how in the hell kunya, S.A na india can exied Tz in Tanzanite sells?..
 
Dah! Kwa Afrika nzima naziona nchi 3 tu ndiyo zinajikongoja: Egypt 0.25%, South Africa 0.21% na Nigeria 0.12%. Bado tuna safari ndefu kwelikweli...
Angelis USA [emoji23][emoji23]
 
Land acquisition ipi unayoisema wewe?! Kama ni lililokuwa shamba la Mohammed Enterprises ni tangu awamu iliyopita! Btw, kukimbilia vipi?! Kila mwenye macho na masikio aliona na kusikia jinsi vijana walivyokuwa wanapelekwa nje ya nchi kusoma masuala ya mafuta na gesi!

Aidha tukashuhudia miswada 3 ikipitishwa kwa hati ya dharula kule bungeni, na mmoja wapo unaoihusu matumizi ya mapato ya mafuta na gesi! Tukashuhudia James Mataragio akivutwa kutoka US na kurudi Tanzania ili aisimamie TPDC ambayo kwa mujibu wa Sera ya Mafuta na Gas, TPDC ndie mmiliki wa vitalu!!

Now let's assume hapo kabla "tulikuwa tunakimbilia"! Je, tangu JPM aingie alipeleka muswada upi bungeni utakaohakikisha tunanufaika na gesi yetu unlike ile miswada mitatu ya mwaka 2015?! Au na lenyewe sio la kukimbilia hadi pale tutakapokuwa na uhakika?!

Btw, uhakika wa nini?! Kama sio sera na sheria zinazohakikishia sera na sheria zingine zinasimamiwa, ni kipi kingine tunahitaji ili kuwa tayari?! How many years do we need kuwa na sheria zenye maslahi kwa taifa?! Au tunasubiri hadi taifa litakapokuwa na billions of USD capital zitalazotuwezesha kuchimba sisi wenyewe?!
 
Huwa nasema ifike wakati facts only must talk....siwezi kuwa sifia wezi kama kenya na history inajieleza vizuri kabisa....kenya ipo hapo ilipo sababu ya vitu vikuu viwili
Huko Tanzania ni lini wizi umeisha?! Halafu unadai "Facts Only" wakati huto supporting doc yoyote kuthibitisha kwamba unachoongea ndio fact yenyewe!?

You guys are very funny!!

Look at you... unataka kuleta mambo yako ya TZ vs KE! Kwa jinsi ulivyoisoma hiyo post yangu umeona elements za TZ vs KE?! Kwanini uzungumzie suala la ukoloni EA wakati hoja yangu ime-base Africa?! Au ndo zile ligi zenu za TZ vs KE...

Kama hoja ni ukoloni, kwanini top isiwe Zimbabwe ambayo Mkoloni ametoka juzi kati tu hapa?!

Kama hoja ni ukoloni, Ethiopia iliyo juu yetu iliachiwa viwanda vingapi na wakoloni?!

Kama hoja ni ukoloni, how come uchumi wa Tanganyika post-colonial era ulikuwa ulikuwa almost the same or even higher compared to some of the South East Asian Economies lakini 50+ years baada ya Wakoloni kuwa wameshaondoka the very same country ipo extremely poor kulinganisha ni zile nchi ambazo wakati wa ukoloni walikuwa na nguvu zinazofanana kiuchumi?!

Na kama ungenisoma kwa vituo, ungeona nilipoandika kwamba:-

Modern Economy ndiyo imeiweka Kenya hapo ilipo, na naweza kuthubutu kusema ndio the best economy in South of Sahara if not the whole of Africa!
Mr. Facts Only, wakati hadi kesho unaendelea kuwaota Wakoloni, mie nimeipa gwala KE kutokana na modern economy, na ukisikia modern economy, ndo hii hapa:- Wakati bado mawazo yako yapo kwenye viwanda vya wakoloni, hapo unaambiwa service sector ndiyo largest contributor wa GDP, na hasira zaidi ni pale tunapoona kilimo kinachangia 34.19% wakati Tanzania yenye largest arable land compared to Kenya, huko kilimo kinachangia 23.4%!! Duh!

Makubaliano yalikuwa hivi:-

That being said, madai yako kwamba eti walikubaliana KE iwe ndo manufacturing center, na UG & TZ wawe watoa malighafi ni madi yasiyo na maana yoyote!!

Na ingawaje KE ilikuwa na viwanda vingi, si kweli kwamba nchi zingine roles zao ilikuwa ni ku-supply malighafi huku KE akiwa na role ya kuzalisha!

Ukweli ni kwamba, kulikuwa na hadi tax introduction ili kulinda viwanda vichache vya vya UG & TZ! Kikubwa kilichokuwa kimeendelea kuiweka juu ni mentality na sera za kiuchumi... jambo ambalo hata baada ya miaka zaidi ya 50 bado kuna Watanzania mna mawazo yale yale ya ku-justify failure yenu na uwepo wa ukoloni, mara sijui KE walizuia ndege za EAC!!!

Baada ya kuvunjika kwa EAC, Tanzania chini ya Nyerere ilikuwa na ndege takribani 8 lakini zote zilikufa... je, hapo utaisingizia KE tena?!

Viwanda ambavyo Nyerere alivianzishwa vikageuka kuwa ma-godwon! Unataka kusema ni KE ndio walifanya viwanda kuwa ma-godown?!

Vita ya UG na TZ iliathiri sana uchumi wa Tanzania!! Unataka kusema ni KE au Wakoloni ndio walitufanya tukapigane ile vita ambayo kimsingi ilichangiwa sana na Mwalimu kutaka kumrudisha Swahibu wake Obotte madarakani!!!

Acheni kulia lia na kutafuta justification ya failure yetu!!

Hadi kesho Tanzania kuna tatizo la mentality and lack of aggressiveness!

Fanya jaribio dogo tu la kutafuta maneno ya Kiswahili ya matunda na mboga mboga!!! Kama source yako ya kutafuta materials ni online, basi Swahili sources nyingi utakazopata online ni Kenyan Sources!!

Mfano mwingine wa wazi kabisa nimeingia YouTube nika-type "Learn Swahili", na search result ni hii hapa chini:-



Hivi mtu anatakiwa kuwa mzoefu wa KE kujua kwamba madada wenye sura ngumu kama huyo anayetokea juu kabisa ya search result ni Mkenya?!

Na hizo mbili zilizofuata ni from KE!

Na all search results zinapatikana ni hapa: YouTube

Majority ni Kenyan sources!!!

Uliza Freelancers wa Kitanzania wana nafasi ipi over Kenyan Freelancers linapokuja suala la Swahili Translation!! Majority duniani wanadhani Kenya ndo kiliko Kiswahili, na Wakenya wanaitumia kweli kweli hiyo hiyo fursa ukilinganisha na Watanzania!!

Na hapa tukumbushane Swahili Teaching gigs ilivyokuwa imetolewa kule South Africa... yaani hata SA wanaamini ukitaka Kiswahili, nenda Kenya!!!

Sasa ikiwa hata Kiswahili tunashindwa kukitumia na kutufanye tuwe on top of all, ndo itakuja kuwa kwenye hayo mengine?! Au hapo tena unataka kusingizia Wakoloni au EAC?!

And to be honest, hakuna kirusi kikubwa kwa mustakabali wa Tanzania kama watu wa aina yako ambao bado wanaisingizia hostory kama chanzo cha failure yetu!
 
Kusoma unacho andika naona km unaleta porojo hazi justify anything kusu kufaidika kwa shirika la ndege ?
Pili unajifanya unakata kitu ambacho kipo wazi ni kenya aliye kuwa anaplay monopoly all along , Tanzania ivi karibuni tu imeanza kuzalisha upya n kupanua zaid sector ya viwanda ilipotea ...na kipindi kile ilikuwa n kenya mweny viwanda vingi nalo tubishane?
Usicho kijua kipi kuwa kunya ilikuwa ni kama centre of busness...sina haja ya kuleta upinzani wa kenya na Tz ....naongea ukwel uliopo...
Ivi unajua kwenye ile jumuiya ya kwanza moja sababu ya kuvunjika ni kunya kuwa n viti vingi kwenye meza ya kamati ya mamuzi...unaonekana unajua vichache lakina unaleta mihemko yako...
Unajua kuwa kulikuwa n viwanda vyilivyo chini ya umoja EA nani alinufaika navyo zaidi?
 
Narudia... ACHA POROJO!!

Na kwa mara nyingine nasisitiza hili taifa lipo hapa kwa ajili ya watu aina yako ambao hadi karne ya 21 bado wanalia lia kuhusu athari za wakoloni!!

And I repeat, KE kuwa na viwanda vingi hakukufanya Tanzania isiwe na viwanda!! Na ni kutokana na ukweli huo ndio maana hata Mwalimu alijenga viwanda vingi tu hata kabla jumuiya haijavunjika!!

An objective question lingekuwa ni kwanini basi viwanda hivyo vya Mwalimu havikuleta productivity iliyotarajiwa ingawaje jibu linafahamika!!!

Ni aibu miaka 59 baada ya uhuru, na miaka almost 40 tangu kuvunjika kwa EAC ya mwanzo halafu bado unadai eti KE ipo hapo kwa ajili ya Mkoloni alimwachia viwanda, na eti kwa sababu alichukua ndege za EAC!

Tanzania ina ardhi ya kutosha kuliko KE! Tanzania tuna raslimali nyingi kuliko KE! Tuna ukanda mrefu wa bahari kuliko KE! Tuna maziwa na mito mingi kuliko KE! Tuna mbuga nyingi za wanyama kuliko KE!

Almost kila kitu tunacho kwa wingi kuliko KE halafu bado leo hii unazungumzia KE ipo hapo kwa ajili ya viwanda vya wakoloni wakati raslimali tulizonazo zinaweza kufanya makubwa kuliko yaliyofanywa na hivyo viwanda vya kikoloni!!

Nimekuuliza kama KE ipo hapo kwa ajili ya viwanda vya mkoloni, Ethiopia liyokuwa juu yetu ipo hapo kutokana na viwanda vilivyoachwa na nani?! JIBU HILO SWALI!!

Pili, nimekuuliza viwanda ambavyo vilijengwa na Nyerere vipo wapi?! Unataka kusema vilikosa effeciency kwa sababu ya viwanda vya mkoloni Mwingereza alivyoacha Kenya? AGAIN, JIBU HILO SWALI!!

Kila anayetaka kutumia ubongo wake sawa sawa anafahamu uchumi wa Tanzania mosi, ulivurugwa na ujamaa ingawaje tulianza vizuri, na pili, ulivurugwa baada ya nchi kuingia vitani Uganda!

Hapo tena nimekuuliza; ni KE au wakoloni ndo walitufanya kuingia vitani Uganda?! Hapa pia, badala ya kuendelea kujiliza liza na historia, JIBU HILO SWALI!

Tanzania tulikuwa na viwanda kibao vya nguo... unataka kusema hivi vilikufa kwa sababu ya KE kuwa na viwanda vya kikoloni?!

Vile viwanda ambavyo vilikuwa Morogoro na Mwanza unataka kusema vilikufa kwa ajili ya viwanda vya wakoloni vilivyoachwa KE?

Pale Arusha kulikuwa na General Tyre East Africa! Unataka kusema kile kiwanda kilikufa kwa ajili ya viwanda vya vikoloni vilivyokuwa vimeachwa KE?

Pale Kurasini kulikuwa na kiwanda cha kusindika samaki... unataka kusema kilikufa kwa ajili ya viwanda vya kikoloni vilivyoachwa KE?! Au unataka kusema kilikufa kwa sababu KE alikuwa anahodhi manufacturing?!

National Milling iliuawa na viwanda vya KE?! RTCs ambazo zilienea kote Tanzania ziliuawa na viwanda vya KE?!

NImekupa mfano unaoweza kueleweka hata na mtoto wa darasa la pili kwamba, ingawaje Tanzania ndo watumiaji wakubwa wa Kiswahili, lakini KE ndo wana-take advantage zaidi ya Kiswahili kuliko Watanzania, to the point majority of Swahili sources online ni za Wakenya!!

Je, hilo nalo ni kwa sababu ya Wakoloni kuwekeza KE?!

Kisha unadai:
Tanzania ivi karibuni tu imeanza kuzalisha upya n kupanua zaid sector ya viwanda ilipotea ...na kipindi kile ilikuwa n kenya mweny viwanda vingi nalo tubishane?
Hivi unajua unachoongea wewe?! Unaweza kutaja orodha ya viwanda ambavyo vilijengwa miaka ya 70 wewe?! How come tuanze kupanua sekta ya viwanda hivi sasa wakati tulikuwa na viwanda vya kumwaga miaka ya 70?! Viko wapi hivyo viwanda?

According to African Business Magazine, Top 5 Banks in East Africa are Kenyan Commercial Bank, Barclays Bank (KE), Equity Bank (KE), Standard Chartered Bank (KE) na Cooperative Bank (KE)!

Sasa ulitarajia Standard Bank (TZ) na Barclays Bank (TZ) ziwepo kwenye hiyo orodha wakati tuliamua uchumi wetu kuuweka chini ya dola, na matokeo yake benki kama Standard Chartered Bank na Barclays zikataifishwa na kuundwa NBC ambayo na yenyewe tulishindwa kuiendesha!!??

And to be honest, hili jukwaa huwa nalikwepa sana kwa sababu najua nikikutana na watu aina yako, halafu mtu akaamua kueleza uhalisia, itakuwa tunajivua nguo wenyewe!!

But what else should I expect kutoka kwa mtu ambae, generally speaking, 90% ya post zake ni Ligi ya KE vs TZ?! Mbaya zaidi, hata kujenga hoja za kubadilisha nyekundu kuwa damu ya mzee, uwezo huo hauna!!!

Hoja zako zisizo na kichwa wala miguu zitasababisha nifanye kile kile ambacho huwa najizuia kukifanya kwenye hili jukwaa manake mtu ukielezea uhalisia inakuwa tunajivua nguo wenyewe!!!
 
Wew unaongea mada mbili tofaut au ndio mihemko .....mada yangu siyo kwanin Tz iko nyuma ya kenya au kwanini ethiopia iko mbele ya Tz.....mada ni kivipi kenya imefika hapo ilipo....acha porojo....wala sina haja y kukulazmisha ...kila mtu na content n welewa wake....upite kimyakimya sikunyinge ujifunze kuto badili mada...
 
Nikukot inisaidie nini ....nyie ndio wale wanao amini kuandik sn ndio kuelewek.....cha zaid umeishi kubadili topic[emoji23]...pita kimyaaa
 
Nikukot inisaidie nini ....nyie ndio wale wanao amini kuandik sn ndio kuelewek.....cha zaid umeishi kubadili topic[emoji23]...pita kimyaaa
Look at you!! "Nikukot unisaidie nini" halafu bado una-quote!!! Jibu ulichoulizwa, kama huna jibu, stfu!
 
Upuuzi mtupu!! Nani kaongea mada tofauti kama sio wewe mwenyewe?! Mada yangu iliangazia uchumi wa Africa, with example to KE relative to top African economies!!

Badala yake, ukaja na hoja ambazo bila shaka ndizo zimekufanya ujiunge JF... Kenya vs TZ! Mara oh, Kenya wezi; mara East African Community! Mara Wakoloni!!!
 
Ungekuwa unatak kujibiw ungejib ww cyo kubadilisha topic.....cna haj y kujib mtu wa miemko...
Una matatizo si kidogo!! Yaani hujijui kabisa kwamba ndie umebadili topic!! Unadai nimebadili topic baada ya kukuonesha ni namna gani hoja yako isivyo na mantiki yoyote!!!
 
Wanaposema madini hayaozi wanamaanisha yataendelea kuhitajika miaka elfu na elfu, kwa namna moja ama nyingine. Umetumia mfano wa Nitrogen kutengeneza natural gas, huku ukisahau kuwa bado unahitaji "natural occuring N2" kama malighafi.

Hata tekinolojia ya kutengenza lightweight composite materials za ndege bado inahitaji madini ya asili ili kutengeneza mchanganyiko unaotakiwa.

Africa ina Gdp ya $2.4 trillion. Sawia na uchumi wa UK au France.
Hiyo ni definition tuu waliyoiweka wazungu to keep the narrative. Si kweli kuwa UK ni Tajiri kuliko Afrika, hata kwa kiasi cha samaki tuu walio Afrika, wanathamani zaidi ya hiyo $2.4T.
 
Wanaposema madini hayaozi wanamaanisha yataendelea kuhitajika miaka elfu na elfu, kwa namna moja ama nyingine. Umetumia mfano wa Nitrogen kutengeneza natural gas, huku ukisahau kuwa bado unahitaji "natural occuring N2" kama malighafi.
Wanaposema "madini hayaozi" hawana maana nyingine zaidi ya "No Hurry in Africa"!!

Na katika dunia ambayo tech inakua kila siku wala usijidanganye kwamba eti yataendelea kuhitajika miaka maelfu kwa maelfu! Of course, yanaweza kuendelea kuhitajika lakini wakati huo thamani yake imeshuka!!

Nimekupa mfano wa Blue Point na Space X! Usidhani wale jamaa wanataka kwenda kutalii sayari za mbali bali wameshanusa potential iliyopo kule!! Sasa wakati unaamini madini yataendelea kuhitajika miaka maelefu kwa maelfu, si ajabu wakati huo watu watakuwa wanashusha madini kutoka Sayari ya Mars!!!

Enzi zetu wakati tupo Primary School, tulikuwa tunaambiwa miongoni mwa mabara yote, kuna Bara la Antarctica ambalo haliishi watu!! Leo hii tunapoongea, routes za kwenda Antarctica zimeongezeka baada ya kugundulika mali asili za kumwaga huko!

Hata ule mkataba uliosaini mwaka 1991 ukitaka kuto-exploit natural resources in Antarctica , leo hii watu wanapambana uwe nullified ili watu waka-exploit resources!!

Routes sawa na hizo zimeongezeka Baltic Sea, and it's a matter of time kabla hawajaanza kutoana macho!!

Yote hiyo ni kuonesha dunia hamsubiri anayesema eti "madini hayaozi"!! People always stay awake kutafuta alternatives, na hadi wengine tutakapokuja kusema "it's time", trust me... it's too late!!!

Mifano ipo... hivi unadhani hivi sasa Middle East wanaringa na mafuta yao kama ilivyokuwa miongo iliyopita wakati shehen za mafuta na gesi hazijangulika sehemu nyingine?! Who imagined kwamba Kusini mwa Tanzania peke yake kungekuwa na over 50 trillion cubic feet of gas reserve?!!

Kama Tanzania tunayo reserve kama hiyo, na Msumbiji imeshathibitika kuwepo kwa uwingi vile vile... bila kusahau Somalia!! Nini kitafanya reserve kama hiyo au zaidi ya hiyo kutokuwepo kwenye nchi zingine zile zilizo ukanda wa Red Sea, Atlantic and the rest of Indian Ocean?!

Waarabu walitoboa kwa sababu mafuta ilionekana na bidhaa adimu ambayo yalipatikana kila mahali!!!

Usishangae miaka 50 ijayo dunia ikawa na mabwawa ya mafuta huku watu wakiendelea kutafuta alternative energy source!!
 
Hiyo ni definition tuu waliyoiweka wazungu to keep the narrative. Si kweli kuwa UK ni Tajiri kuliko Afrika, hata kwa kiasi cha samaki tuu walio Afrika, wanathamani zaidi ya hiyo $2.4T.
Utajiri wako ni ule unaoweza kuboresha maisha yako, na sio huu utajiri tunaoimba kila siku kwamba Afrika tajiri huku watu wake wakiendelea kufa kwa maradhi yanayotibuka!!!

Siwezi kuonea fahari PhD ya baba ambae ni kichaa, na badala yake bora nionee fahari diploma ya baba wa kambo inayoweza angalau kuleta ugali kwa mchicha mezani!!!
 
Umeongea fact brooo....watu akili bado ni narrow sanaaaa....wamebaki na blabla...nyingi
 
Thamani itashukaje wakati madini yatazidi kuwa haba?

Bado huko kwengine yawezekana kukawa na madini tofauti na ya kwetu kutokana na utofauti wa fizikia ya huko (temp, radiation, gravity etc). Hivyo bado madini ya duniani yakawa na thamani kubwa, vile vile itachukua miaka mingi kupungua gharama za kuyaleta madini hayo duniani na kuweza kufanya biashara.


Hiyo yote ni kutokana na uhaba, kama mtu anaweza kuokota embe dodo chini hana haja ya kupanda mti.
Tatizo siyo kuchimba bali kuwa tayari ili nchi ifaidike. kumbuka tulivyoliwa kwenye madini kwa miaka 20, kwa kuwa hatukuwa tayari kuyachimba, tuliharakisha tuu.

kama nchi haiko tayari (kisheria, kimiundombinu, kitaalamu) watakao faidika wengine na sisi kuendelea kuwa masikini. Hii ndiyo sababu ya kusema, "hayaozi", ikimaanisha tusikurupuke sasa, kwa kuwa yatakuwepo hata kesho.

Mahitaji ya maliasili yatazidi kuongezeka, kwakuwa watu wanazidi kuongezeka duniani, hivyo kama bado hatuwezi kunufaika ni heri tusubiri ili wanetu watakapo kuwa na akili wanufaike.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…