Nchi ambayo Wafanyabishara wanaweza kugharamia safari za Rais za Kitaifa na Kimataifa haiwezi kujali maslahi ya wananchi wa kawaida

Nchi ambayo Wafanyabishara wanaweza kugharamia safari za Rais za Kitaifa na Kimataifa haiwezi kujali maslahi ya wananchi wa kawaida

The Assassin

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2018
Posts
4,942
Reaction score
20,077
Juzi tuliambiwa gharama za safari za rais za kitaifa na kimataifa zinagharamiwa na wafanyabishara ambao hawatajwi majina.

Katika akili ya kawaida, kama wafanyabishara wanagharamia safari za mkuu wa nchi nje ya nchi na ndani ya nchi maana yake tayari rais ameshakuwa compromised na wafanyabishara. Hivyo wafanyabishara wanafanya vile wanavyotaka.

Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya mkuu wa nchi kuwekwa mfukoni na watu kadhaa ama kikundi flani cha watu ambao wanaweza kumpa maelezo na kumtuma cha kufanya.

Hali hii imejitokeza mbele ya macho yetu. Rais wetu anafadhiliwa na kikundi flani cha watu ambao wanamuelekeza cha kufanya kwani tayari kikundi hicho kinafadhili shughuli za rais na shughuli za serikali.

Kwa msingi huo, ndio maana unaona wafanyabishara wanajiamulia kupandisha bei ya mafuta ambayo yalinunuliwa kwa bei ya chini na hakuna kitu Serikali itawafanya.

Msukuma ameshangaa mafuta yaliyonunuliwa mwezi Februari kupanda bei ghafla sawa na mafuta yanayouzwa leo kwenye soko la Dunia.

Tukubaliane kwamba kaama nchi tumepigwa na kitu kizito kichwani. Mkuu wetu wa nchi yuko mifukoni kwa watu.
 
Ninasikia siyo kugharamia safari tu; wanamsaidia kisiasa pia.

Kuna chama fulani kilikuwa kinadai Katiba Mpya, kiongozi wao amepenyezewa bahasha ya khaki mchezo ukaisha.

Wazalendo nchi hii walikuwa Nyerere na Magufuli tu!
 
Juzi tuliambiwa gharama za safari za rais za kitaifa na kimataifa zinagharamiwa na wafanyabishara ambao hawatajwi majina...
Sasa wewe ndugu hata ukiwambiwa hao waliogharamia utawafanya nini? Mambo menginr muyaache kama yalivyo.

Matajiri ndio Moyo wa taifa
 
Ninasikia siyo kugharamia safari tu; wanamsaidia kisiasa pia.

Kuna chama fulani kilikuwa kinadai Katiba Mpya, kiongozi wao amepenyezewa bahasha ya khaki mchezo ukaisha.

Wazalendo nchi hii walikuwa Nyerere na Magufuli tu!
Na wewe tu basi wengine woote hamna kitu🤣🤣
 
Hatari yake ndio kama hii, wanashindwa kusimamia maslahi ya nchi.

Mtu anakulipa unapata wapi nguvu za kumkaripia.
 
Hatari yake ndio kama hii, wanashindwa kusimamia maslahi ya nchi.

Mtu anakulipa unapata wapi nguvu za kumkaripia.
Basi badala na wewe kulalamika jiunge kwenye kundi linalomfadhili Rais na wewe unufaike.
 
Back
Top Bottom