Nchi moja serikali mbili: Unafahamu kuwa bado China ipo kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe?

Nchi moja serikali mbili: Unafahamu kuwa bado China ipo kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe?

Mto Songwe

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2023
Posts
6,683
Reaction score
14,060
Chukua hii kwa ufupi:

Nchi ya China inayopatikana mashariki ya mbali ya bara la Asia.

Hii ni nchi moja yenye serikali mbili zilizo katika mgogoro wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo havijatamatika toka 1949 mpaka sasa.

Katika nchi ya China kuna serikali mbili zinazo ng'ang'ania mamlaka ya kutawala China moja au yote.

Serikali hizi ni Jamhuri ya China inayopatikana katika visiwa vya Taiwan na serikali ya Jamhuri ya watu wa China inayopatikana bara.

Asili ya vita hivi vya wenyewe kwa wenyewe ni mapinduzi ya wakomunisti wa China ambao kwa sasa wanaunda serikali ya Jamhuri ya watu wa China kuingia vitani na serikali ya Jamhuri ya China ilivyokuwa inatawala sehemu kubwa ya China kwa wakati huo chini ya chama cha Kuomintang.

Vita vyao vilipiganwa kwa muda mrefu mpaka pale wakomunisti walipotwaa maeneo ya China bara na kusimika Jamhuri ya watu wa China na serikali Jamhuri ya China kukimbilia kisiwani jambo lililowapa ugumu wakomunisti kwa wakati huo kuweza kabisa kuishinda Jamhuri ya China na kuiangusha moja kwa moja.

Mara kwa mara wakomunisti wamekuwa wakijipanga kuiangusha kabisa Jamhuri ya China nayo Jamhuri ya China kwa mara kadhaa imejaribu kutaka kutwaa tena madaraka ya China yote.

Kifupi mpaka sasa China ipo vitani wao kwa wao muda wowote wakishindwa kufikiana tamati kwa njia ya amani basi mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yataibuka tena China kati ya Jamhuri ya China na Jamhuri ya watu wa China( wakomunisti).
 
Hao vibaka waliokimbilia kwenye kisiwa cha Taiwan watadhibitiwa muda sio mrefu!

Hao ni vibaka wanaoshirikiana na NATO ili waweze kuivunjavunja China yote vipandevipande. Bahati mbaya hawana uwezo huo na hawatokaa wawe nao. Sanasana wataisababishia NATO matatizo yasiyoweza kurekebishika.
 
Hao vibaka waliokimbilia kwenye kisiwa cha Taiwan watadhibitiwa muda sio mrefu!
Hao ni vibaka wanaoshirikiana na NATO ili waweze kuivunjavunja China yote vipandevipande...bahati mbaya hawana uwezo huo na hawatokaa wawe nao. Sanasana wataisababishia NATO matatizo yasiyoweza kurekebishika
You know what serikali zote hizi mbili madai yao yanafanana kuhusu kuitawala China yote.

Kila serikali inajiona ina haki hiyo
 
Hao vibaka waliokimbilia kwenye kisiwa cha Taiwan watadhibitiwa muda sio mrefu!

Hao ni vibaka wanaoshirikiana na NATO ili waweze kuivunjavunja China yote vipandevipande. Bahati mbaya hawana uwezo huo na hawatokaa wawe nao. Sanasana wataisababishia NATO matatizo yasiyoweza kurekebishika.
Apo unaongea n msuli wako ukiwa madrasa kisiju
 
Madrasa na mambo ya China na Taiwan wapi na wapi?? Madrasa zimekukosea nini? Au ndo mafundisho unayopata kwenye kanisa lako la mabati chini ya mchungaji wako wa kinyaks
Madrasaa c ndiko mnakofundishwa kuchukia ubeberu. Ni mwiko kwa mkristo halisi kujua juu ya dini zingine za ajabu ajabu
 
Hiyo sio sababu! Taiwan ni kama shahawa mbele ya daktari mbobevu mbele ya China bara. Tena Taiwan ni sehemu ya jamhuri ya watu wa China
Yaaasss visiwa vya Taiwan ni sehemu ya China ambayo Jamhuri ya China ndipo yalipo makao makuu yake kwa sasa na serikali ya Jamhuri ya China ndio inaamini Taiwan na maeneo yote ya China ina haki nayo ila sio Jamhuri ya watu wa China.

Na Jamhuri ya watu wa China nayo inaamini yenyewe ina haki pekee kuhusu maeneo yote ya China pamoja na Taiwan ndani yake palipo makao makuu ya Jamhuri ya China na inaamini Jamhuri ya China haina haki hiyo kuhusu China.
 
Madrasaa c ndiko mnakofundishwa kuchukia ubeberu. Ni mwiko kwa mkristo halisi kujua juu ya dini zingine za ajabu ajabu
Sasa hata kama hivyo ndivyo,, je kwenye huu uzi kuna sehemu yoyote inahusisha masuala ya madrasa Zaidi ya China na Taiwan? Kwa kuingiza habari hizo za madrasa hapa hujioni wewe ndie mwenye chuki kwa hizo unazoziita imani nyingine
 
China aliigwaya na ataendelea kuigwaya US!
Nafikiri unaizungumzia Jamhuri ya watu wa China ?

Sio kweli kuwa Jamhuri ya watu wa China inaihofia U.S maana kwa sasa U.S sio tishio kijeshi kwa Jamhuri ya watu wa China kama ilivyokuwa miaka ya 50 ninaweza sema Jamhuri ya watu wa China inajaribu kusogeza mbele muda ili kuona maafikiano ya amani baina yake Jamhuri ya watu wa China na Jamhuri ya China kama yatafikiwa.

Maafikiano ya amani yasipo fikiwa kuna asilimia kubwa kuzuka vita baina ya hizi serikali mbili katika muendelezo wa kugombania utawala wa China
 
Back
Top Bottom