Nchi nyingi nilizotembelea mikate ni chakula ila huku kwetu ni kitafunwa

Nchi nyingi nilizotembelea mikate ni chakula ila huku kwetu ni kitafunwa

🤣 🤣 🤣 pole. Now you know.

Jiandae kula mikate asubuhi, mchana na jioni wanabadilisha majina tu; burger, hotdog, pizza, sandwich yote ni mikate tu.
Kabisa burger na hotdog ni mkate ,wanacheza na majina tu
 
Nilishangaa nigeria kuna ugali, tena ugali kwa mlenda, nilijua ni tanzania tu ndio wanakula ugali kumbe hata nchi za afrika magharibi ugali upo. Huenda ugali ukawa ni chakula maarufu duniani.
jioni ya leo sina hamu ya kula ugali au wali, nakula mkate kwa juisi nilale. Nikikosa mkate nakula matunda sahani imejaa inatosha
 
Hata hapa bongo watu wanashindia mkate ila hali ya kiuchumi ikiyumba.
Nimeshuhudia chuo kikuu watu wakishindia mkate
 
Sema Mkuu huku Tz Maisha magumu Sana that way tunaishia kula ugali.
Siyo umasikini hata kidigo! Chakula ni sehemu ya utamaduni. Nilicheka sana nilipokuwa namsikiliza Rais wa Burundi wakati anahojiwa na BBC ni chakula Gani anakipenda alijibu maharage!
Kuna Ndugu yetu alikuwa china kusoma, Kuna wakati tulimtumia unga wa Dona Ili apike ugali maana alikosa hata Raha ya kuishi huko.
 
WATu tushakula ugali na wali kama mboga wewe mkate tu makelelehumu😁
 
Niliwahi fika hospital ya Ikonda iliyopo Makete. Wao wanavipaza sauti kwa maana ya kutolea elimu ya Afya. Kilichoniduwaza ni pale walipokuwa wanashauri suala la lishe na kuhimiza vyakula vifuatavyo ni chakula taka. 1. Mandazi 2.chapati 3. Vitumbua. Na vinginivyo vya ngano vya kukaanga mnavyovijua. Kuanzia pale Huwa nakula kwa nadra sana hivyo vitu
Ni kweli,
 
chakula ni contenti sio Quantity,Kwa wenzetu mkate unaandaliwa kwa kuwekwa mayai,Maziwa kisha wakati wa mlo huambatana na mboga za majani au nyama kisha hushushiwa na matunda Au juice.Huu ni mlo kamili ila Sisi mpaka upate kitu kizitoooo.
 
Kweli kila nchi na tamaduni zake, msosi pia ni sehemu ya tamaduni. Wakati bongo tunajivunia chipsi yai, au supu chapati usichukulie poa, Mrisho Ngasa na Kapombe walishindwa kucheza Ulaya kisa chipsi yai.

Turudi kwenye mada, nikiwa Cape town, nilishuhudia watu wakila soda na mikate kama mlo, Zimbabwe, Zambia, USA wataita hotdog Ila ndio huohuo, Ulaya ukipandisha bei ya mkate utapata shida Sana.

Kwa wakristo sala ya Bwana kuna ile phrase ya our daily bread imekuwa termed kama chakula, hata Yesu Alilisha watu elfu tano samaki na mkate. Mkate ni chakula sio kitafunwa Kwa wenzetu.

Hata huku ni chakula, labda kwenu tu ndo vitafunwa
 
Kweli kila nchi na tamaduni zake, msosi pia ni sehemu ya tamaduni. Wakati bongo tunajivunia chipsi yai, au supu chapati usichukulie poa, Mrisho Ngasa na Kapombe walishindwa kucheza Ulaya kisa chipsi yai.

Turudi kwenye mada, nikiwa Cape town, nilishuhudia watu wakila soda na mikate kama mlo, Zimbabwe, Zambia, USA wataita hotdog Ila ndio huohuo, Ulaya ukipandisha bei ya mkate utapata shida Sana.

Kwa wakristo sala ya Bwana kuna ile phrase ya our daily bread imekuwa termed kama chakula, hata Yesu Alilisha watu elfu tano samaki na mkate. Mkate ni chakula sio kitafunwa Kwa wenzetu.
Wanaokula mikate ndio wenye akili kuliko wanaokula ugali
 
Siyo umasikini hata kidigo! Chakula ni sehemu ya utamaduni. Nilicheka sana nilipokuwa namsikiliza Rais wa Burundi wakati anahojiwa na BBC ni chakula Gani anakipenda alijibu maharage!
Kuna Ndugu yetu alikuwa china kusoma, Kuna wakati tulimtumia unga wa Dona Ili apike ugali maana alikosa hata Raha ya kuishi huko.
Niliiona hii nilicheka kinoma nikaimagine yaani daa eti yaani kwenye mlo usipoweka maharage haelewi isee inawezekana mwamba akija kwenu halafu anuse harufu ya ndondo na hamjampa anaondoka anasikitika daa wameamua kuninyima maharage powa tu!
 
Unalosema ni kweli kabisa na ninashangaa inakuaje hapa bongo kunakuwa na tatizo la nguvu za kiume wakati tuna vyakula vyenye nguvu na virutubisho.

Sasa mfano SA nilifika nikakuta machakula hayaeleweki nikajiuliza hawa wanaishije. Nadhani kibongo bongo tuna tatizo la kukinai ngono lakini kwa nguvu siamini hata kidogo kwamba kwa kula chipsi yai ndio kufanye mtu asiwe na nguvu za kiume wakati zipo nchi hawajui wali na wakipika wali wao utakimbia.
Tatizo la nguvu za kiume halipo ila wafanyabiashara wa mitishamba walitengeneza liwe tatizo ili wapige hela kwa kulitangaza sana.

Vilevile kama umenotice kitu currently kuna wahuni wana advocate" Mental Health" kwa kufanya ionekane kuwa ni tatizo kubwa linalohitaji intervention wakati hata halipo watu wanatafuta namna ya kupiga hela za watu.

Rejea namna mafuta ya wanyama yalivyopigwa vita na watengenezaji wa mafuta ya mimea enzi hizo utabaini trend ilivyo.

Usicheze na wajasiriamali.
 
Back
Top Bottom