Nchi za Afrika za Francophonie na Common wealth zinalipa Trillion 3000 kila mwaka kwa Ufaransa na Uingereza kama fidia ya faida za ukoloni

Nchi za Afrika za Francophonie na Common wealth zinalipa Trillion 3000 kila mwaka kwa Ufaransa na Uingereza kama fidia ya faida za ukoloni

Kwa sasa naandika kwa kifupi sana, ila nitaleta andika kamili kesho au baadae.

Nitaanza na Francophone Africa. mnafahamu kwamba Ufaransa iliwasainisha makoloni yake yote mkataba unaoitwa ‘Agreement for the continuation of colonialism’ kabla hajawapa ‘uhuru feki’?

Msingi wa mkataba huu ni kwamba Ufaransa anadai alipwe kwanza fidia ya maendeleo yote ya kiutawala na miundo mbinu ambayo aliwekeza kwenye nchi hizo ili aweze kuondoka.

Kuna nchi mbili ziligoma kusaini , kilichowakuta kiliwaogopesha makoloni mengime yote na wakasaini. Wale waliogoma, Ufaransa aliondoka , lakini alichukua kila kilicho chake ambacho kinahamishika, vile ambavyo havihamishiki walivichoma moto vyote, waling’oa reli, walichoma moto majengo yote ya kiutawala, walichoma moto maghala yote ya chakula, walitia sumu visima vyote, waliharibu kila kitu! Ndio wakaondoka, kuona dhahama hiyo, wote waliobaki walisaini.

Kupitia mkataba huo wa siri wa kinyonyaji, nchi za Francophone Africa wanalipa Dollar Billioni 500 kila mwaka kwa Ufaransa, na sharti kuu ni iwe siri , wananchi wasiambiwe.

Marais wengi wapya wa nchi hizo kila walipoingia madarakani walikutana na mkataba huu, na hawakuamini walichokiona, na wakagoma kulipa, kila aliyegoma aliuwawa au kupinduliwa. Angalia histora ya Marais wa nchi hizo, utashangaa, wengi sana wameuwawa na kupinduliwa.

Burkinafaso mfano, walishamuuwaga Thomas Sankara, hata huyu Rais wao wa sasa, huu mkataba ulimuumiza sana roho, na akawafukuza wafaransa na kusema wazi kabisa , haogopi kufa, na hata majaribio ya mapinduzi wameshamfanyia majaribio zaidi ya 10, na bado wanaendelea kumuwinda. Ameina bora akatafuta alliance na Urusi, na wameingia military pact ya kumlinda kwa malipo kidogo. Inshort huyu Dogo kawaambia Ufaransa lije jua ije mvua, halipi hiyo pesa!! Na kawatimua nchini kwake!

Huo mkataba nitauleta na nitauchimbua msharti yake yalivyo makali, inaumiza sana. Dollar billion 500 kila mwaka wale mbwa wanavuna, inauma sana!

Safi sana inapendeza
 
Hivi ni utani ama kweli. Mbona naona ni kama jambo lisilowezekana. Sasa huko kwenye umoja wa Africa viongozi Huwa wanakutana kujadili nini kama unyonyaji ni mkubwa hivyo
Sio utani, nenda pale ubalozi wa Ufaransa, waambie unahitaji kuelimishwa kuhusu utendaji kazi wa CFA. 85% ya reserve unatakiwa upeleke Ufaransa, na yeye atazitumia atakavyo.., na wewe ukizihitaji inabidi ukakope kwa mkopo wenye riba ya kibiashara, na hutakiwa kukopa zaidi ya 20% ya pesa zako kwa mwaka. Ukigoma kupeleka yanakukuta ya Thomas Sankara au Laurent Bagbo. Ona dogo rais Burkinafso anavyowindwa kuuwawa na kupindukiwa, hadi kakimbilia kwa Putin kuomba ulinzi.., maana anagoma kupeleka pesa..

Hatabsisi wa Commonwealth, tunaminywa vilivyo kupitia mikopo hewa ya lazima toka IMF na WB, mama kafikisha deni Trilioni 100 toka Trillion 50. Kipi kimefanya hizo pesa?
 
Kwahiyo hujaona mfano mwingine? Kuwa na adabu jukwaani.
Adabu is overrated and relative.

Naweza kukuambia kuwa wewe kuweka habari nzito kama hii bila hata link ya reference nako ni kukosa adabu kwa wasomaji wa JF.
 
Adabu is overrated and relative.

Naweza kukuambia kuwa wewe kuweka habari nzito kama hii bila hata link ya reference nako ni kukosa adabu kwa wasomaji wa JF.
Link mbona hata wewe umeweka, inatosha.
 
Link mbona hata wewe umeweka, inatosha.
Sasa ukiweka habari nzito kama hii ambayo inasomeka kama conspiracy theory, weka na link.

Source ni muhimu.

Uoneshe kwamba hii habari ina source si kitu ulichotunga mwenyewe au kusikia kijiweni tu.
 
Sasa ukiweka habari nzito kama hii ambayo inasomeka kama conspiracy theory, weka na link.

Source ni muhimu.

Uoneshe kwamba hii habari ina source si kitu ulichotunga mwenyewe au kusikia kijiweni tu.
Link uliyoweka wewe imetosheleza
 
Link uliyoweka wewe imetosheleza
Nimeweka links mbili moja ya kuelezea point yako na nyingine ya kuweka muktadha zaidi kwamba Ufaransa ya Charles de Gaulle na ya leo ni tofauti na suala hili lina historia ndefu na ambayo haijanyooka kama unavyotaka kusema wewe, kwamba Waafrika wanaolaumu Ufaransa mpaka leo wanakwepa wajibu wao wa kujiongoza wenyewe.

Kwamba hiyo hofu ya kupinduliwa wakijiondoa iko overblown.

Umesoma hiyolink ya pili kupata muktadha mkubwa zaidi kuliko hiyo simple story unayotoa?
 
Nimeweka links mbili moja ya kuelezea point yako na nyingine ya kuweka muktadha zaidi kwamba Ufaransa ya Charles de Gaulle na ya leo ni tofauti na suala hili lina historia ndefu na ambayo haijanyooka kama unavyotaka kusema wewe, kwamba Waafrika wanaolaumu Ufaransa mpaka leo wanakwepa wajibu wao wa kujiongoza wenyewe.

Kwamba hiyo hofu ya kupinduliwa wakijiondoa iko overblown.

Umesoma hiyolink ya pili kupata muktadha mkubwa zaidi kuliko hiyo simple story unayotoa?
kwamba nchi za CFA hawalazimiki kupeleka 85% ya reserve zao benki kuu ya Ufaransa kila mwaka? Kwamba wakizihitaji hizo pesa hawalaazimiki kukopa kwa riba?
 
kwamba nchi za CFA hawalazimiki kupeleka 85% ya reserve zao benki kuu ya Ufaransa kila mwaka? Kwamba wakizihitaji hizo pesa hawalaazimiki kukopa kwa riba?
No, hawalazimiki kuendelea na mfumo huo, wao ni nchi huru.

Nyerere anajulikana dunia nzima kwa "The Nyerere Doctrine of State Succession".

Hao viongozi wa Africa hawajasoma hiyo?

West Africa wanajeshi kila baada ya miaka kadhaa wanapindua nchi kwa kusema hawataki unyonyaji wa Wafaransa, mbona hatuoni wakijjondoa kwenye mfumo huu?

Utawalaumu vipi Wafaransa zaidi ya Waafrika miaka yote hii baada ya Waafrika kuanza kujitawala?
 
Mwanzo niliona Kama unatania lakini baada ya kuisoma Link moja hapo juu nimejikuta nacheka tuu

Inaweze kanaje mtu aliye kutawala ndiye akufundushie jeshi lako?

Ina wezekanaje ukawa huru na ukapangiwa Cha kufanya na aliye kuwa amekutawala? Kwamba Kama unatatizo niite Mimi nikusaidie sio mwingine?

Inaweze kanaje mtu aliye kuwa amekutawala Ana kiambia upo huru na anakulazimisha uzungumze lugha take Kama lugha ya taifa?

Inaweze kanaje mtu aliye kuwa amekutawala anakuambia kwamba Mali yoyote utakayo igundua niambie Mimi Kwanza nikii kataa ndipo umpe mwingine?

Kuna mengi ya kipuuzi yanasikitisha Sana Africans leaders nivilaza mpakaka kufa
 
Hivi ni utani ama kweli. Mbona naona ni kama jambo lisilowezekana. Sasa huko kwenye umoja wa Africa viongozi Huwa wanakutana kujadili nini kama unyonyaji ni mkubwa hivyo
Ufaransa ni mnyonyaji kweli kweli, hadi kuna viongozi wenzake huko bara ulaya wanamkandia sana, hasa hasa yule mama wa italia, Giorgia Meloni.
 
No, hawalazimiki kuendelea na mfumo huo, wao ni nchi huru.

Nyerere anajulikana dunia nzima kwa "The Nyerere Doctrine of State Succession".

Hao viongozi wa Africa hawajasoma hiyo?

West Africa wanajeshi kila baada ya miaka kadhaa wanapindua nchi kwa kusema hawataki unyonyaji wa Wafaransa, mbona hatuoni wakijjondoa kwenye mfumo huu?

Utawalaumu vipi Wafaransa zaidi ya Waafrika miaka yote hii baada ya Waafrika kuanza kujitawala?
Wanaojaribu kupinga mfumo huu wapo, wengi wamuwawa na wakawekwa vibaraka wanaondeleza mfumo, wanaopinga wachache kama Rais wa Burkinafaso wanaonjeshwa joto ya jiwe.., huko ndio kulazimishwa.., na ilianza kwa Sekou Toure wa Guinea 1958
 
Wanaojaribu kupinga mfumo huu wapo, wengi wamuwawa na wakawekwa vibaraka wanaondeleza mfumo, wanaopinga wachache kama Rais wa Burkinafaso wanaonjeshwa joto ya jiwe.., huko ndio kulazimishwa.., na ilianza kwa Sekou Toure wa Guinea 1958
Sasa hapo shida Waafrika wamekosa organization. Huwezi kupinga structural power imbalance ya dunia kwa kutegemea watu.

Unapinga kwa kutengeneza strong institutions.

Mfaransa lazima atetee interests za Ufaransa kuinyonya Africa, that is to be expected.

Waafrika wanafanya nini kujikwamua?
 
Sasa hapo shida Waafrika wamekosa organization. Huwezi kupinga structural power imbalance ya dunia kwa kutegemea watu.

Unapinga kwa kutengeneza strong institutions.

Mfaransa lazima atetee interests za Ufaransa kuinyonya Africa, that is to be expected.

Waafrika wanafanya nini kujikwamua?
Sasa kumbe tunabishana nini? , maana unachosema ndicho ninachosema.., kwamba Africa inanyonywa..
 
Back
Top Bottom