Nchi za kijamaa (communist) na siasa za vyama vingi huwa haviivi

Nchi za kijamaa (communist) na siasa za vyama vingi huwa haviivi

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Duniani leo nchi za kijamaa (communism) zimebaki chache sana. Imebaki China, Vietnam, Cuba, Tanzania na zingine mbili tatu. Mtu anayesema Tanzania siyo nchi ya kijamaa anakuwa anakosea sana. CCM chama kinachoongoza nchi yetu ni chama cha kijamaa. Katiba yetu inasema hivyo, na hata sheria na taratibu za kuendesha nchi zimetungwa kwa mtazamo huo wa kijamaa.

Ukiangalia nchi hizi nne, ni Tanzania pekee ambayo ni nchi ya kijamaa lakini inafuata mfumo wa vyama vingi. China, Vietnam, na Cuba hakuna habari za vyama vingi. Sababu ni kuwa ujamaa na vyama vingi hauendani kabisa. Ujamaa ni mfumo fulani wa kidikteta, hauwezi kuendana na siasa za vyama vingi.

Matatizo ya kisiasa tuliyonayo leo yanatokana na kuchanganya ujamaa na mambo ya vyama vingi. Ingekuwa vizuri tuchague moja.
 
Uko sahihi kabisa, ila hapa kwetu kwa sasa tumebaki na ujamaa uchwara. Wako wanufaika wa keki ya taifa kwa halali na haramu, wanajua fika ccm ikitoka madarakani mirija yao ya muda mrefu itakatika.

Hivyo wako radhi wapore uchaguzi ili waendelee na mlo. Namna pekee ya kuwatoa madarakani hawa wajamaa uchwara, ni kuleta machafuko tu.
 
Hapana. Nchi za kijamaa ni nyingi. Na hizo ulizotaja sio za kijamaa. China, Vietnam, Cuba,tz,ni inchi za kikomunist. Nchi za kijamaa ni USA
 
Lakini ukiangalia Practically, hakuna nchi duniani ambayo imeshawahi kuwa Communist (kwa kurejea sifa za Ukomunist). China tunaweza iita Socialist sababu, socialist in its wider sense, inaruhusu mifumo fulani ya kibepari kuexist kwenye jamii, ndio maana Unaweza ona watu kama kina Jack Ma wapo. Vinginevyo katika Ukomunist kitu kama Alibaba kisngeweza kuwepo (katika namna ilivyo leo).

By the way, i don't see a problem ya kuwa na chama kimoja ikiwa wananchi wanajamii wenyewe wako Ok na mfumo huo.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Kwani hizo nchi mnazoziita za kipebari hazina ujamaa? Nenda Ulaya magharibi kote uchumi wao unaitwa wa kibepari kwa maana tu ya kwamba serikali zao hazijihusishi kwenye uendeshaji na uzalishaji lakini linapokuja kwenye masuala ya huduma za kijamii (elimu, afya, na vitu kama hivyo) ni ujamaa mtupu.
 
Kwani hizo nchi mnazoziita za kipebari hazina ujamaa? Nenda Ulaya magharibi kote uchumi wao unaitwa wa kibepari kwa maana tu ya kwamba serikali zao hazijihusishi kwenye uendeshaji na uzalishaji lakini linapokuja kwenye masuala ya huduma za kijamii (elimu, afya, na vitu kama hivyo) ni ujamaa mtupu.
Umechanganya.
Uchumi wao ni wa kibepari ujamaa umebakia kwenye mgawanyo wa raslimali.
Hii ndio mfumo sahihi yaani uchumi ushikwe na sekta binafsi kodi imilikiwe na serikali kisha igawe sawa kwa wote
 
Umechanganya.
Uchumi wao ni wa kibepari ujamaa umebakia kwenye mgawanyo wa raslimali.
Hii ndio mfumo sahihi yaani uchumi ushikwe na sekta binafsi kodi imilikiwe na serikali kisha igawe sawa kwa wote
Ndicho nilichomaanisha. Mbona kama tupo sawa?

Shida yangu ni hawa ndugu zangu waliomezeshwa kuwa ujamaa ni mbaya, wanaomeza kila kitu bila kutathmini na kuchanganya za kwao.
 
Ndicho nilichomaanisha. Mbona kama tupo sawa?

Shida yangu ni hawa ndugu zangu waliomezeshwa kuwa ujamaa ni mbaya, wanaomeza kila kitu bila kutathmini na kuchanganya za kwao.
Ujamaa sio mbaya ubakie kwenye mambo ya kijamii na sio kwenye uzalishaji
 
Duniani leo nchi za kijamaa(communism) zimebaki chache sana. Imebaki China, Vietnam, Cuba, Tanzania na zingine mbili tatu. Mtu anayesema Tanzania siyo nchi ya kijamaa anakuwa anakosea sana. CCM chama kinachoongoza nchi yetu ni chama cha kijamaa. Katiba yetu inasema hivyo, na hata sheria na taratibu za kuendesha nchi zimetungwa kwa mtazamo huo wa kijamaa...
Huu ndiyo ukweli unaoisumbua Tanzania. Na nijuavyo hakuna mahali popote duniani U communist umewahi kufaulu. Hata sisi tutacheza makidamakida mwisho wa siku majirani zetu ' kina Rwanda na Kenya wakiendelea kutuacha mbali . U communist ni u dictator kwa kifupi .
 
Kati ya idea mbovu kabisa kuwahi kutokea dunian mojawapo ni ujamaa huu
Ni mfumo fulan hiv wa kidictator tu wakuua watu na kuwafanya watu waishi kimaskini sanaaaaaa refer Tz ya nyerere , North Korea , Cuba
Shida ya huu mfumo wananchi ndo ulazimishwa kuishi kijamaa huku watawala wakiishi kibepari.Nyerere alikuwa akitumia colgate,sabuni,wananchi chumvi na majivu kupigia mswaki, Nyerere hakuwahi kupanga foleni kugombea bidhaa.Check Magari na ndege za kifahari ya Kipanki Korea kaskazini.
Ktk watu kondoo dunia na wanatakiwa kukombolewa kifikra ni watu wa North Korea aisee hawa watu wanaishi dark age.
 
Well said Angalia hata Urusi pamoja na akili zao lakini ujamaa umesababaisha iwe nchi ya hovyo.
 
Lakini ukiangalia Practically, hakuna nchi duniani ambayo imeshawahi kuwa Communist (kwa kurejea sifa za Ukomunist). China tunaweza iita Socialist sababu, socialist in its wider sense, inaruhusu mifumo fulani ya kibepari kuexist kwenye jamii, ndio maana Unaweza ona watu kama kina Jack Ma wapo. Vinginevyo katika Ukomunist kitu kama Alibaba kisngeweza kuwepo (katika namna ilivyo leo).

By the way, i don't see a problem ya kuwa na chama kimoja ikiwa wananchi wanajamii wenyewe wako Ok na mfumo huo.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Your right. CCM wangekuwa na dhamira ya kweli na hili taifa wangetutosha kabisa. Just, imagine 60 years bado tunajengewa vyoo na Marekani. Huu sio umaskini wa raslimali ni umaskini wa kimfumo(Institutional poverty).
 
Back
Top Bottom