Ujasusi wa kiuchumi hauhusiani na 10% wanayopewa viongozi wa CCM kutoa bure rasilimali zetu.Mataifa ya nje khasa mataifa makubwa wana uwezo mkubwa wa kuingilia mataifa madogo kwa njia mbalimbali.
Njia mojawapo ni ya ujasusi.
Mwaka 2016, niliongelea hili suala la ujasusi wa kiuchumi na kiteknolojia kupitia hapa: Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari
Kwa andiko kama hili lililowekwa hapa, sidhani kuwa hata huyo aliyeliandika ataweza kusoma mkataba wowote na kuuelewa.Hata hiyo mikataba tukipewa tuisome yachosha hivyohivyo na ndo twaishia kusaini bila kusoma hadi mwisho na kuelewa.
Mbona umenielewa!Wala hueleweki, mwanzako para 2 zingetosha na wewe mstari mmoja tu ungetosha.
Wakoloni wanarudi kwasababu huu ndo wakti muafaka.Ni wapi kwenye post yangu nimemtaja JPM, au unajishuku? Hivi Richard umetuchukulia sisi humu jukwaani ni kama hao wa kwenye vijiwe vya alkasusu? Ramani ya dunia hii ni kitu adimu, mpaka useme kuna mtu anayo as if ni kitu adimu sana? Mimi hapa nina ramani ya dunia nzima, na rasilimali, viwanda, majengo mbalimbali ndani vya dunia hii. Je hiyo ni ishara kuwa nataka kwenda kuchukua utajiri wa maeneo hayo? Nimekuuliza wakoloni wameondoka hapa nchini miaka 60 iliyopita, ni lini wamewahi kurudi kuchukua madini yetu kijasusi bila kuingia mikataba na viongozi wetu? Richard achana na hizi hekaya kama za mtu aliyechanganyikiwa.
Tatizo ni lilelile umaskini na kupenda 10%
Wakoloni wanarudi kwasababu huu ndo wakti muafaka.
Hata mwenzetu Barafu aliongelea hili kuhusu mgodi wa Almasi wa Williamson.
Hili la wao kurudi nimelizungumzia kwenye mada.
Pia nikamtaja huyo mwandishi Kaplan ambae kitabu chake kinazungumzia mabeberu watatu watakaokuwa wakipigana vikumbo ndani ya bahari ya Hindi.
Nchi hizo za kibeberu ni China, Marekani na India.
Nimeeelezea uzuri tu.
Mkuu 'eliakeem', kwa kusoma tu kichwa cha habari ya andiko hilo, tayari nimekwishatambua ni habari ya aina ambazo kikawaida huwa sizipi uzito sana.Embu jaribu kusoma hii, pole pole utapata maana.
Tanzania's Late President Magufuli: "Science Denier" or Threat to Empire?
While his COVID-19 policies have dominated media coverage regarding his disappearance and suspicious death, Tanzania’s John Magufuli was hated by the Western elites for much more than his rebuke of lockdowns and mask mandates.unlimitedhangout.com
Nadhani naposema ramani hujaelewa.Ukisema mambo ya 10% utaeleweka. Sio mambo ya kusema sijui kuna mtu ana ramani, au atachukua raslimali kijasusi. Namna pekee raslimali zetu zinaweza kutoka bila sisi wananchi kufaidika, ni tamaa za hawa viongozi wetu majizi ya kura, na sio kijasusi kama ulivyotaka kupotosha hapo mwanzo.
Tanzania kwa sasa ni ya pili Afrika kwa kuzalisha dhahabu pekee baada ya Afrika Kusini.Hao mabeberu sijui wawekezaji wapo tu miaka yote, na hawatumii nguvu bali ushawishi na 10%. Ukiona wanatumia nguvu, basi ujue nchi husika ina matatizo mengine hasa ya kiutawala. Na isitoshe nchi yetu haina madini ya hivyo, kiasi kwamba hao wakoloni wachanganyikiwe.
Uhusiano upo kinachotakiwa ni vitu viwilli vyaitwa kwa kiingereza lobbying and grooming.Ujasusi wa kiuchumi hauhusiani na 10% wanayopewa viongozi wa CCM kutoa bure rasilimali zetu.
mara mikataba kama hiyo inakipengele cha NDA (non-disclosure agreement )Huvyo huwezi kukiuka hicho kipengele kirahisiHapa najiuliza kwa nini mwendazake akuuweka wazi mkataba wa bandari ya bagamoyo ili nasi tuuone ulivyo wa ovyo?
Sent using Jamii Forums mobile app
Tanzania kwa sasa ni ya pili Afrika kwa kuzalisha dhahabu pekee baada ya Afrika Kusini.
Wafahamu hilo?
Sasa icho kipengele kingefanya kazi Kama shughuli ujenzi ingekubaliwa, lakini saizi mkataba haufanyi kazi Yani waste au kwa ajili ya kujifunzia tu kwa trainee na wanafunzi.mara mikataba kama hiyo inakipengele cha NDA (non-disclosure agreement )Huvyo huwezi kukiuka hicho kipengele kirahisi
Jamani hakuna tena mabeberu dunia.huyu jamaa kafilisika kimawazo.CAG kakague Wizara ya Madini na Nishati utujuze.Hupati dhahabu mpaka huyo au hao mnaowaita mabeberu waje wawekeze mamilioni ya dola.Sio madini tu sekta zote zinataka wawekezaji wenye mitaji.Tuliwakimbiza wakati wa awamu ya 5 matokeo yake CAG kayatoa.Jamani amkeni hii ni awamu ya 6LOOoo, unachosha sana na mizunguko isiyokuwa na maana aiseee!
Para mbili tatu zingetosha kabisa kueleza kitu.
Haya, 'source' yako ya haya mambo ni ipi?
Haya mambo ya kukazania 'Mabeberu,.... mabeberu' kila wakati na kusahau kuwasilisha habari muhimu ya taarifa inazingua sana.
Sasa sijui hapa kijadiliwe kipi, mabeberu, au njia tunazoweza kuzifanya tunufaike na hizi mali zetu?
Utanisamehe kama nitakukwaza kwa haya niliyoandika, lakini ukweli nimekwazwa na njia yako ya uwasilishaji wa habari yenyewe, ambayo nadhani ni habari muhimu.
Andiko la Hovyo kabisa nililopata kusoma!