Nchimbi: Mungu nipe moyo wa kusamehe

Nchimbi: Mungu nipe moyo wa kusamehe

Yeye ana uhakika gani kama wale wote waliouawa na jeshi police yeye akiwa waziri wa mambo ya ndani kama wamemsamehe? Shame on U Nchimbi!
 
Laana itamwandama sana,damu za wote waliouawa na polisi kwa baraka zake itakuwa juu ya kichwa chake daima!
 
Bungeni alitamba kwa jeuri mbaya sana, kuwa hakuna tume itaundwa ya bomu mkutano CDM arusha
 
Unafiki mtupu acha kudanganya watu.ulikuwapi siku zote kkutoa kauli hiyo?yamekufika shingoni ndio unanza kuonyesha huruma.namba mungu akulaani kwani mmeua watu wasio na hatia
 
Mungu akupe moyo wa kusamehewa weye mwenyewe kwanza kwani ulio yafanya kwa kipindi ulichoishika wizara hiyo ya ndani, yanazidi umri ulio nao. Kumbe miaka 42 unafanya uovu wa kumzidi babako???
Nakuomba Eee Mungu unayetusikia tukiomba, msamehe kabisa Nchimbi kwani ni njaa tu zilimpelekea kujisahau kuwa aweza siku moja kuachia ngazi kuwapisha wengine.
 
Kila mtanzania awaye yote anajua kilichompata `dk.' emmanuel nchimbi na wenzake watatu (kagasheki,mathayo na nahodha) wote hao wamefurushwa wizarani kwa aibu wakingali wameinamisha vichwa chini!
Ni kutokana na udhaifu wa kiuongozi,lkn kwa nchimbi ni pamoja na machozi ya watanzania waliouliwa ndugu zao kwa amri za nchimbi,hawa ni watz waishio arusha,iringa,morogoro,ruvuma nk. Damu za wahanga zinalia "mh.nchimbi,nchimbiii...,tuokoe,tunauawa bure na watumishi wako" mh.nchimbi kimyaaaa,moyoni anafurahia sera ya "wapigwe tu" ya mkuu pinda. Machozi ya familia ya mwangosi yanaichuruzikia ardhi yakimlilia nchimbi "...tule nini,tuvae nini, tutunzwe na nani..." mhesh.anajirembulia jicho lake kwa raha zake! Sasa nchimbi yaliyomkuta yamemkuta na mengi zaidi yatamkuta kwa sababu ya kushindwa kujua kuwa cheo ni dhamana.
Kabla mate ya wino wa green point pen ya mh.rais hayajakauka,lazima rungu zito livibonde na kuvisambaratisha vyeo vyote vya mwigulu na kumuacha lowa chapa chapa na aibu tele. Historia ni mwalimu.
 
Nchimbi zambi aliyoifanya sasa inamuhukumu,bado mwenzie mwigulu nchemba mauwaji waliyofanya ystaendelea kuwalilia.
 
Tosabiso abangise mopepe santu nalikolo naipele
botema nangae nono ya Yezu mwana nzambe
CHISTMASE mobili mobimba naitese didii
moningate na losambo ya nkolo nzambe nalobi ya
bon a'nnee'. Motema nayaya tete nangai. Izamote
na mwana Nzambe ya 2014

mmmh labda mods wamekuelewa
 
Asante sana, yaani Mungu wa leo ni kijana, anajibu mapema sana, na wanatakiwa kujua mwenye dhamana na roho za wstu ni Mungu pekee na sio Nchimbi, KamuhandaZuberi, Nchimbi au awaye yeyote. Na Mungu atawaumbua wote mchana kweupe
 
Huku kijijini kwetu tumecheza kula na kunywa kwa siku tatu mfululizo bila kupumzika wala kulala Nchimbi anapaswa kufungwa amesababisha wajane,wagane na mayatima kibao na bado tumefunga ili Mungu amuadhibu zaidi ya hapa hafai katesa watafuta haki huyu bwana nadhani atakuwa amepata shock ya mwaka zaidi ya Ezekiel Maige
 
na bado babu seya wanamtesa burkule gerezani itawala sana,mwangosi na kule arusha ndio usiseme kabisa,nilikwisha kusema kila kitu kina mwisho isipokuwa neno la Mungu tuu,lazima wegine wote waonje joto ya jiwe na majibu watapata hapahapa
 
SIKU chache baada ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi kuvuliwa wadhifa wake kwa tuhuma za kushindwa kusimamia wizara yake, kiongozi huyo ametaka apewe moyo wa upendo na kusamehe. Nchimbi ambaye ni mbunge wa Songea Mjini kwa tiketi ya CCM, alisema hayo juzi kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook, wakati akisherehekea kutimiza miaka 42 ya kuzaliwa.
“Kama Mwenyezi Mungu angeniuliza ni kitu gani anipatie kwa muda huu, ningemuomba anipatie moyo wa upendo na kusamehe,” aliandika.
Mawaziri wengine waliovuliwa nyadhifa zao pamoja na Nchimbi, ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mathayo David Mathayo na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha.
“Sasa nina miaka 42, namshukuru Mungu kwa kunibariki na kunisaidia kwa kipindi cha mwaka mzima, nawashukuru wazazi wangu, kaka, dada na marafiki zangu, pia ninawashukuru waajiri wangu watu wa Jimbo la Songea na Watanzania wote.
“Ninaukubali upendo wenu na kuniunga mkono…Kama Mungu ataniuliza leo kitu gani anipatie jibu langu litakuwa rahisi, nitamwambia Mungu wangu naomba moyo wa upendo kwa kila mmoja, moyo wa kumsamehe kila mmoja pasipo kujali nini nitarudishiwa, anipe moyo wa kuwatumikia watu kwa saa 24 kwa siku,” alisema Dk. Nchimbi.
Dk. Nchimbi na wenzake wanne walienguliwa madarakani baada ya Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wao mara baada ya kupewa taarifa za wabunge kuwashinikiza mawaziri hao wajiuzulu kwa sababu ya yaliyojitokeza katika Operesheni Tokomeza Ujangili.
Kuondolewa kwa mawaziri hao kulitokana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli, kuwasilisha taarifa ya kamati yake iliyobainisha unyama mkubwa waliotendewa wananchi katika operesheni hiyo.
Operesheni hiyo ilikuwa ikizihusisha wizara za mawaziri hao waliong’olewa ambapo inadaiwa watendaji waliokuwa wakiiendesha waliua watu, kujeruhi na kuharibu mali mbalimbali ikiwemo mifugo.
Matukio mengine yaliyobainika kwenye operesheni hiyo ni wanawake kubakwa na wengine wakilazimishwa kufanya mapenzi na mama, wakwe au watoto wao.

Source : Tanzania Daima – Nchimbi: Mungu nipe moyo wa kusamehe

My Take
Bado nafikiria ni kwanini Nchimbi anaomba apewea Moyo wa Kusamehe , tena kwenye siku yake ya kuzaliwa, ina Maana amekosewa sana huyu Bwana !!!!



Kama Nchimbi anaomba moyo wa upendo na kusamehe yafaa angetafakari ya fuatayo:
1.Angefanya nini kama yule mwanamke aliye uawa kama angekuwa ni dada yake au mama yake?
2.Angefanya nini kama wale watoto waliokuwa wakimtegemea mama yao sasa wamebaki wapweke ndiyo angekuwa ni yeye?
3.Angefanya nini kama yule mama aliyeingizwa chupa ya soda ukeni na njia ya haja kubwa kama ange kuwa ni mama yake,shangazi yake au dada yake?
4.Angefanyaje kama yule mheshimiwa aliyeambiwa afanye mapenzi na mti kama angekuwa ni baba yake au kaka yake?
5.Angefanyaje kama wale wanawake waliobakwa kwa zamu kama wangelikuwa ni shangazi zake au mama zake?
Kwa maoni yangu:
Baada ya kupata taarifa zile kama waziri alitakiwa kuwaomba radhi watanzania kupitia vyombo vya habari kutokana na vitendo hivyo vya kinyama vilivyotokea katika wizara iliyochini yake ili watanzania ndiyo waone kama wanaweza kumsamehe au laa kuliko kujiona kama yeye ndiyo kaonewa.
 
Kama Nchimbi anaomba moyo wa upendo na kusamehe yafaa angetafakari ya fuatayo:
1.Angefanya nini kama yule mwanamke aliye uawa kama angekuwa ni dada yake au mama yake?
2.Angefanya nini kama wale watoto waliokuwa wakimtegemea mama yao sasa wamebaki wapweke ndiyo angekuwa ni yeye?
3.Angefanya nini kama yule mama aliyeingizwa chupa ya soda ukeni na njia ya haja kubwa kama ange kuwa ni mama yake,shangazi yake au dada yake?
4.Angefanyaje kama yule mheshimiwa aliyeambiwa afanye mapenzi na mti kama angekuwa ni baba yake au kaka yake?
5.Angefanyaje kama wale wanawake waliobakwa kwa zamu kama wangelikuwa ni shangazi zake au mama zake?
Kwa maoni yangu:
Baada ya kupata taarifa zile kama waziri alitakiwa kuwaomba radhi watanzania kupitia vyombo vya habari kutokana na vitendo hivyo vya kinyama vilivyotokea katika wizara iliyochini yake ili watanzania ndiyo waone kama wanaweza kumsamehe au laa kuliko kujiona kama yeye ndiyo kaonewa.[/FONT][/SIZE][/I]

Nchimbi ni mtu hatari sana tena katili muuaji mtesaji hastahili kusamehewa mpaka pale atakapotubu mbele ya kanisa.
 
Vipi Mwigulu hajawandaa vijana wa kuandamana na kuchoma bendera na kumtusi kqatibu wa maccm kwa kuliondoa jembe la Songea?
Mbona kuna double standard jamani? Kigoma kwa Zito sawa na Songea pia.
 
Hadithi ya fundi cherahani kunyang'anywa SINDANO tu na mwenye cherahani!......basi hawezi shona tena?
 
Back
Top Bottom