Ndani ya siku 100 za Uongozi wake, Rais Samia amefanya mambo makubwa

Ndani ya siku 100 za Uongozi wake, Rais Samia amefanya mambo makubwa

Gesi badala ya kuelekezwa Kwa wananchi Kwa bei nafuu ikauzwa nchi jirani tunayoshindana nayo kiuchumi.

Mikopo Kwa miradi isiyokuwa na ulazima wa kukopa.

Bajeti inayolenga kuongeza uvunjaji wa Sheria Kwa boda boda na ongezeko la watumiaji wa vinywaji vikali.
Hatushindani na nchi yoyote kiuchumi, Sisi tunapambana kukuza uchumi kwa faida yetu.

Unataka tusiuze gesi tuuze nini, ubuyu?
Au kwa kuwa Kenya ni waafrika wenzetu kwa hiyo tusiwauzie gesi, ila ungesikia tunaiuza ulaya ungeona poa tu.

Kama tunashindana na wakenya kiuchumi, basi tusiwauzie Kenya Chakula ili afya zao zidhoofike tuwashinde kiuchumi au vipi?
 
Hatushindani na nchi yoyote kiuchumi, Sisi tunapambana kukuza uchumi kwa faida yetu.

Unataka tusiuze gesi tuuze nini, ubuyu?
Au kwa kuwa Kenya ni waafrika wenzetu kwa hiyo tusiwauzie gesi, ila ungesikia tunaiuza ulaya ungeona poa tu.

Kama tunashindana na wakenya kiuchumi, basi tusiwauzie Kenya Chakula ili afya zao zidhoofike tuwashinde kiuchumi au vipi?
Una umri gani kamanda??
 
Mi namshukuru sana kuwadhibiti viongozi wa kujimwambafai maana walijiona miungu,, kuwa wana amri yoyote juu ya utu wa mtu.

Hili ni kubwa sana kwangu.

Asante mama. Mungu ambariki rais SSH
 
Ongezeko kubwa la kodi wakati huo huo mishahara haijaongezwa kwa miaka sita sasa.
Gesi badala ya kuelekezwa Kwa wananchi Kwa bei nafuu ikauzwa nchi jirani tunayoshindana nayo kiuchumi.

Mikopo Kwa miradi isiyokuwa na ulazima wa kukopa.

Bajeti inayolenga kuongeza uvunjaji wa Sheria Kwa boda boda na ongezeko la watumiaji wa vinywaji vikali.
 
Mama anapiga kazi nzuri
Lakini udini kwa mbali naona ni mdini. Jingine, she is so obsessed with gender balance. Anadhani bado ni mwanaharakati wa enzi ziilee akiwa kwenye ma NGO ili apate wafadhili ilibidi ujitoe fahamu kuitetea gender equality. Kosa la tatu uzanzibari vs ubara yuko oversensitive kuitetea kwao zenj. Akirekebisha hayo matatu akajiona kwanza yeye ni Mtanzania mengine ndipo yanafuata hakika atakuwa rais bora wa awamu zote tangu tupate uhuru. She is very balanced to be honest.
 
Lakini udini kwa mbali naona ni mdini. Jingine, she is so obsessed with gender balance. Anadhani bado ni mwanaharakati wa enzi ziilee akiwa kwenye ma NGO ili apate wafadhili ilibidi ujitoe fahamu kuitetea gender equality. Kosa la tatu uzanzibari vs ubara yuko oversensitive kuitetea kwao zenj. Akirekebisha hayo matatu akajiona kwanza yeye ni Mtanzania mengine ndipo yanafuata hakika atakuwa rais bora wa awamu zote tangu tupate uhuru. She is very balanced to be honest.
Mkuu ulitaka avue hijabu na asiteue muislamu hata mmoja ili uthibishe kuwa siyo mdini?

Mimi naona teuzi zake hazina viashiria vya udini labda kama tunakubaliana kuwa ili rais muislamu asiwe mdini basi ateue waislamu kidogo sana kadri iwezekanvyo.

Hoja za udini hazina mashiko
 
laana ya mashee wa uamsho iliyosajiliwa rasmi haitomwacha mtu ,hata mtu afanye wema kiasi gani ,ikiwa una dhamana ya kuwafuatilia na kujua hatima yao basi nawe unawajibika katika laana tatizo Mwenyezi mungu hana halaka tu hili ndilo tatizo kubwa sana kwetu sisi kuona hivyo ila ana mipango yake na haingiliwi katika maamuzi.
Mashehe wa Uamsho chini ya Sheikh Farid ni hatari kama Osama.

Siku watakayoachiwa tu tutaanza kusikia, Kanisa limelipuliwa, padri kauliwa au kituo cha Polisi kimevamiwa.

Watanzania tuwe wakweli, matukio ya 2014 Mbagala, Bukoba na Zanzibar yalitia doa amani ya nchi yetu. Tanzania iko salama kwa mashehe kuwa rumande. Potelea pote.

Kuna kitu Serikali inakijua sisi hatukijui, tisijelaumu wakileta madhara
 
NDANI YA SIKU 100, RAIS SAMIA AMEFANYA MAMBO MAKUBWA

Wanaandika Ndugu Twahir Abasi Kiobya na Denis Shanyangi

Kama kuna jambo lolote linalonipa amani na Faraja kwenye nafsi yangu katika siku 100 zilizopita, basi ni kuona kuwa tuna rais wa aina ya Mama Samia Suluhu Hassan.

1. Ndani ya siku 100 tu za utawala wake, Keshaondoa zimwi la 6% retention fee kwenye mikopo ya elimu ya juu, Hii retention fee ilikuwa ni pasua kichwa sijawahi kuona, mtu ulikywa unalipa lakini deni haliishi, na kinshahara chako kinakwanguliwa tu month after mobth

2.Wale standard 7 waliotimuliwa na Magufuli kipindi cha Uhakiki mama kasema walipwe stahiki zao, Hii ni faraja kubwa kwa ndugu zetu wa darasa la Saba ambao walivuja jasho kwa haki kabisa kwa ajili ya Taifa hili.

3. Serikali ya mama iko serious kwenye kupandisha madaraja ya watumishi wa serikali yaliyosimama kwa miaka 5 ya Magufuli.

4. Samia anarudisha uhuru wa habari kwa mfano online TVs sasa zimefunguliwa

5. Wafanyakazi wa serikali wamepunguziwa PAYE hadi 8%

7. Ameshatoa bilion 172 kwa ajili ya kuboresha barabara za vijijini angalau barabara hizo ziweze kupitika. Ifahamike kuna watu wanashindwa kuwahisha wajawazito hospitali kujifungua kwa sababu ya barabara mbovu, Hatua hii ya mama itasaidia sana.

8. Serikali yake imeweka utaratibu wa watoto wanaopata ujauzito waendelee na masomo, hili ni jambo zuri katika vita dhidi ya umasikini, ujinga na maradhi. Maana huwezi kumsaidia mtoto kwa kumfukuza shule maana ukifanya hivyo unamtia yeye na mwanae umasikini wa kutisha, na litakuja kuwa ni mzigo kwa Taifa mbeleni

9. Mama karudisha common sense kwenye suala la Korona, sasa hivi hatusemi tena "Changamoto ya kupumua", bali tunasema Korona—Huwezi kupambana na ugonjwa usiotaka kuuita hata jina lake ukaushinda, lakini sasa hivi tunapambana nao kitaalamu na siyo kienyeji

10. Rais Samia karudisha nidhamu ya wateule, wasijimwambafy na kuzichukulia poa mamlaka, Sasa hivi yule kijana jeuri ananyea ndoo

11. Rais Samia kakataa kupora pesa za watu ili eti kuongeza makusanyo, yeye anataka kodi za haki

12. Rais Samia keshafungulia account za watu zilizofungwa kimagumashi

13. Rais Samia anataka mabenki yatoe interests rate ndogo, anataka 10% ili wananchi waweze kuafford kukopa na kuendesha biashara zao, Riba ya mabenki enzi za nyuma ilikuwa pasua kichwa, ilikuwa inaenda hadi 25%

14. Rais Samia kaamua mradi wa Gesi Lindi uendelee, faida za mradi huu ni kubwa, tutapata gesi kwa ajili ya viwanda vyetu, tutauza nje, na tutazalisha umeme mwingi zaidi.

15. Kesi za Kubambikiza rais Samia kazifuta, watu 172 waliobambikiziwa kesi na TAKUKURU rais Samia keshazifuta, Huu ni utu na ubinadamu ulioje!

16. Mama kafuta adhabu ya kulipa 10% kwa wale wanaochelewa kuanza kulipa mkopo wao bodi ya mkopo

17. Mama Samia keshashusha bei za bando ambazo utawala uliopita uliacha umepandisha na kupelekea kuleta taharuki kubwa nchini, Imagine eti ulikuwa ukiweka sh 2000 hupati GB hata moja, lakini sasa hivi angalau kwa sh 2000 unapata GB 1 na kuendelea

18. Rais Samia keshafanikisha uuzwaji wa mahindi yetu Kenya Wakulima sasa hivi mioyo yao kwatu, imetukia tuli

19. Rais Samia keshafanikisha utiwaji saini dili la kuiuzia Kenya gesi, hili ni dili safi safi sana, tuna gesi nyingi tu, tukitumia wenyewe na ziada tukiuza na kupata mpunga mrefu itasaidia kwenye uchumi wetu

20. Rais Samia ameendeleza miradi ya kimkakati ya mtangulizi wake, amepeleka hela kwenye miradi yote ya maana ya mtangulizi wake

21. Ndani ya siku zake 100, Rais Samia ameshatangaza ajira zaidi ya 9000 za walimu na wahudumu wa Afya na vijana wetu maelfu kwa maelfu wameomba. Hili ni jambo zuri sana, na huu ni mwanzo tu Mama anaendelea kumwaga ajira kwa vijana wetu.

22. Ndani ya siku 100, Rais Samia kapunguza faini za pikipiki kutoka 30000 hadi 10000, hii habari njema ilioje kwa wenzetu wa bodaboda!

23. Ndani ya Siku 100 za uongozi wake, Rais Samia kapunguza gharama za kuunganisha umeme mijini kutoka shilingi 300000 hadi shilingi 27000, hili ni jambo zuri sana, wananchi wanapunguziwa mzigo wa maisha.

24. Ndani ya siku 100, Mheshimiwa rais Samia, amerejesha imani ya Wawekezaji, Dangote anasema Tanzania chini ya Rais Samia ni mahali pazuri pa kuwekeza, Manji amerudi maana yake confidence ya Wawekezaji na wenye mitaji imeanza kurudi, hii itasaidia wawekezaji kutengeneza ajira zaidi na kulipa kodi serikalini

Kwa hiyo by all Standards, Rais Samia ameupiga mwingi sana ndani ya siku zake hizi 100 za utawala wake.

Na namtabiria makubwa kwa sababu ana Hekima, Utu, Subira, Yuko open minded, Ni mchapakazi sana, ana exposure, ana uzoefu mkubwa.

We are Lucky kuwa mama is our president
Naunga mkono hoja. Kwa kweli Rais SSH anaupiga mwingi kama Ngolo Kante wa Chelsea. Anakaba, anatoa assist halafu ana speed ya hatari.

Naamini hata Katiba bora ya wananchi atatuachia. Mungu enedelea kumbariki Rais wetu SSH azidi kuiweka nchi inapotakiwa
 
NDANI YA SIKU 100, RAIS SAMIA AMEFANYA MAMBO MAKUBWA

Wanaandika Ndugu Twahir Abasi Kiobya na Denis Shanyangi

Kama kuna jambo lolote linalonipa amani na Faraja kwenye nafsi yangu katika siku 100 zilizopita, basi ni kuona kuwa tuna rais wa aina ya Mama Samia Suluhu Hassan.

1. Ndani ya siku 100 tu za utawala wake, Keshaondoa zimwi la 6% retention fee kwenye mikopo ya elimu ya juu, Hii retention fee ilikuwa ni pasua kichwa sijawahi kuona, mtu ulikywa unalipa lakini deni haliishi, na kinshahara chako kinakwanguliwa tu month after mobth

2.Wale standard 7 waliotimuliwa na Magufuli kipindi cha Uhakiki mama kasema walipwe stahiki zao, Hii ni faraja kubwa kwa ndugu zetu wa darasa la Saba ambao walivuja jasho kwa haki kabisa kwa ajili ya Taifa hili.

3. Serikali ya mama iko serious kwenye kupandisha madaraja ya watumishi wa serikali yaliyosimama kwa miaka 5 ya Magufuli.

4. Samia anarudisha uhuru wa habari kwa mfano online TVs sasa zimefunguliwa

5. Wafanyakazi wa serikali wamepunguziwa PAYE hadi 8%

7. Ameshatoa bilion 172 kwa ajili ya kuboresha barabara za vijijini angalau barabara hizo ziweze kupitika. Ifahamike kuna watu wanashindwa kuwahisha wajawazito hospitali kujifungua kwa sababu ya barabara mbovu, Hatua hii ya mama itasaidia sana.

8. Serikali yake imeweka utaratibu wa watoto wanaopata ujauzito waendelee na masomo, hili ni jambo zuri katika vita dhidi ya umasikini, ujinga na maradhi. Maana huwezi kumsaidia mtoto kwa kumfukuza shule maana ukifanya hivyo unamtia yeye na mwanae umasikini wa kutisha, na litakuja kuwa ni mzigo kwa Taifa mbeleni

9. Mama karudisha common sense kwenye suala la Korona, sasa hivi hatusemi tena "Changamoto ya kupumua", bali tunasema Korona—Huwezi kupambana na ugonjwa usiotaka kuuita hata jina lake ukaushinda, lakini sasa hivi tunapambana nao kitaalamu na siyo kienyeji

10. Rais Samia karudisha nidhamu ya wateule, wasijimwambafy na kuzichukulia poa mamlaka, Sasa hivi yule kijana jeuri ananyea ndoo

11. Rais Samia kakataa kupora pesa za watu ili eti kuongeza makusanyo, yeye anataka kodi za haki

12. Rais Samia keshafungulia account za watu zilizofungwa kimagumashi

13. Rais Samia anataka mabenki yatoe interests rate ndogo, anataka 10% ili wananchi waweze kuafford kukopa na kuendesha biashara zao, Riba ya mabenki enzi za nyuma ilikuwa pasua kichwa, ilikuwa inaenda hadi 25%

14. Rais Samia kaamua mradi wa Gesi Lindi uendelee, faida za mradi huu ni kubwa, tutapata gesi kwa ajili ya viwanda vyetu, tutauza nje, na tutazalisha umeme mwingi zaidi.

15. Kesi za Kubambikiza rais Samia kazifuta, watu 172 waliobambikiziwa kesi na TAKUKURU rais Samia keshazifuta, Huu ni utu na ubinadamu ulioje!

16. Mama kafuta adhabu ya kulipa 10% kwa wale wanaochelewa kuanza kulipa mkopo wao bodi ya mkopo

17. Mama Samia keshashusha bei za bando ambazo utawala uliopita uliacha umepandisha na kupelekea kuleta taharuki kubwa nchini, Imagine eti ulikuwa ukiweka sh 2000 hupati GB hata moja, lakini sasa hivi angalau kwa sh 2000 unapata GB 1 na kuendelea

18. Rais Samia keshafanikisha uuzwaji wa mahindi yetu Kenya Wakulima sasa hivi mioyo yao kwatu, imetukia tuli

19. Rais Samia keshafanikisha utiwaji saini dili la kuiuzia Kenya gesi, hili ni dili safi safi sana, tuna gesi nyingi tu, tukitumia wenyewe na ziada tukiuza na kupata mpunga mrefu itasaidia kwenye uchumi wetu

20. Rais Samia ameendeleza miradi ya kimkakati ya mtangulizi wake, amepeleka hela kwenye miradi yote ya maana ya mtangulizi wake

21. Ndani ya siku zake 100, Rais Samia ameshatangaza ajira zaidi ya 9000 za walimu na wahudumu wa Afya na vijana wetu maelfu kwa maelfu wameomba. Hili ni jambo zuri sana, na huu ni mwanzo tu Mama anaendelea kumwaga ajira kwa vijana wetu.

22. Ndani ya siku 100, Rais Samia kapunguza faini za pikipiki kutoka 30000 hadi 10000, hii habari njema ilioje kwa wenzetu wa bodaboda!

23. Ndani ya Siku 100 za uongozi wake, Rais Samia kapunguza gharama za kuunganisha umeme mijini kutoka shilingi 300000 hadi shilingi 27000, hili ni jambo zuri sana, wananchi wanapunguziwa mzigo wa maisha.

24. Ndani ya siku 100, Mheshimiwa rais Samia, amerejesha imani ya Wawekezaji, Dangote anasema Tanzania chini ya Rais Samia ni mahali pazuri pa kuwekeza, Manji amerudi maana yake confidence ya Wawekezaji na wenye mitaji imeanza kurudi, hii itasaidia wawekezaji kutengeneza ajira zaidi na kulipa kodi serikalini

Kwa hiyo by all Standards, Rais Samia ameupiga mwingi sana ndani ya siku zake hizi 100 za utawala wake.

Na namtabiria makubwa kwa sababu ana Hekima, Utu, Subira, Yuko open minded, Ni mchapakazi sana, ana exposure, ana uzoefu mkubwa.

We are Lucky kuwa mama is our president

Tutumie common sense bhas wakat mwingine, hayo mambo makubwa unayoyasemwa kuna watu nyuma yake walianzisha, acheni sifa za kipumbavu
 
Mi namshukuru sana kuwadhibiti viongozi wa kujimwambafai maana walijiona miungu,, kuwa wana amri yoyote juu ya utu wa mtu.

Hili ni kubwa sana kwangu.

Asante mama. Mungu ambariki rais SSH
Hili ni jambo. muhimu sana ili wateule wakumbuke kuwa cheo ni dhamana!
 
Kwa hiyo by all Standards, Rais Samia ameupiga mwingi sana ndani ya siku zake hizi 100 za utawala wake.

Na namtabiria makubwa kwa sababu ana Hekima, Utu, Subira, Yuko open minded, Ni mchapakazi sana, ana exposure, ana uzoefu mkubwa.

We are Lucky kuwa mama is our president
Huhitaji orodha ndefu kiasi hicho kupigia debe.

Mstari mmoja tu wa anapoharibu unatosha kabisa kufuta hizo rasharasha unazoweka hapa.

Ni kama sifa alizopewa mtangulizi wake katika mambo kadhaa aliyoyafanya yakionekana kuwa mzazuri kwa taifa; lakini jambo moja au mawili mazito zaidi zaidi yamevuruga kila kitu alichokisimamia Mwendazake.

Vuta subira, utapewa huo mstari mmoja au miwili itakayokuonyesha kwamba mama anaiuza Tanzania kwa walanguzi na wachuuzi kwa bei cheee! Hapo ndipo utakapogundua kwamba hajafanya lolote la maana katika hizo siku 100.
 
Huhitaji orodha ndefu kiasi hicho kupigia debe.

Mstari mmoja tu wa anapoharibu unatosha kabisa kufuta hizo rasharasha unazoweka hapa.

Ni kama sifa alizopewa mtangulizi wake katika mambo kadhaa aliyoyafanya yakionekana kuwa mzazuri kwa taifa; lakini jambo moja au mawili mazito zaidi zaidi yamevuruga kila kitu alichokisimamia Mwendazake.

Vuta subira, utapewa huo mstari mmoja au miwili itakayokuonyesha kwamba mama anaiuza Tanzania kwa walanguzi na wachuuzi kwa bei cheee! Hapo ndipo utakapogundua kwamba hajafanya lolote la maana katika hizo siku 100.

Ni Mpaka hilo unalolisema litokee kwanza, hatuwezi kupiga ramli kwa sasa kuwa lazima itakuwa hivyo unavyofikir

Lakini so far so good Mama anakwenda vizuri
 
Ni Mpaka hilo unalolisema litokee kwanza, hatuwezi kupiga ramli kwa sasa kuwa lazima itakuwa hivyo unavyofikir

Lakini so far so good Mama anakwenda vizuri
Hizi si ni siku 100?
Hayo mazito huwezi kuyaona katika siku 100, ila misingi yake na dalili zake (mwelekeo) ndio unaoonekana.

Hayo ya rasharasha ni utamu wa peremende tu.
 
Back
Top Bottom