Sasa Kama una wese Kidebe,hiyo jeuri ya kugeuza ulikotoka utaipata wapi!?? Rubani wa Precision nilimuelewa sana,na alifanya maamuzi yake very professional! RIP Rubani! Wese Kidebe bado ni tatizo kubwa kwa wawekezaji uchwara, wanapenda kucheza na Maisha ya watu!!Huo ndio uamuzi wa busara tunaotumia sisi marubani sio kulazimisha kutua hata kama kuna ugumu kufanya hivyo
MuongoMkuu wewe basi rubani muoga. Mimi ndio zangu hizo hasa naporusha hivi vi cassena single engines. Nimeshawahi kitua kwenye hurricane bahamas.
Pia nimeshawahi kutua kwenye tornado texas. Nimeshawahi kutua kwenye dhoruba ya monsoon. Nimeshawahi kutua kwenye typhoon manilla ufilipino.
Nimeshawahi kutua kwenye tropical cyclone msumbiji tena hizi hizi single engines cassena.
Majaliwa wapo kila mahali..Mungu wa mbinguni atulinde
Na hivi Shujaa Majaliwa Hayupo sijui ingekuwaje!
Nafikiri wavuvi walianza kujongea ziwaniMajaliwa wapo kila mahali..
Mafuta Kidebe ni shida sana!!Kabla ya report nimeshagundua kitu huyu wa precision aliishiwa mafuta aliweka ya kwenda tu kama bodaboda
Hata kwenye viwanja vikubwa duniani kuna kipindi ndege zinashindwa kuruka au kutua kutokana na hali ya hewa kutoruhusu.Msimu wa mvua kipindi hiki ni shida aisee.Ila sio technical issues,ni mambo ya Hali ya hewa.
Huwa yanaisha mkuu.Daaa!!hivi ndege kuishiwa mafuta unadhania ni kitu rahisi kama kwenye bodaboda!!kuna mambo mengine kabla hata ya kuyaandika tumia kwanza halimashauri ya ubongo wako kwanza kufikiria. Inshu ya ndege kuishiwa mafuta ,lazima kuwe na sababu ya kiufundi,iliyopelekea mafuta hayo kutumika tofauti na makadirio,sasa ndege itoke dar,izunguke anga la bukoba mala moja,mafuta yaishe?!!Toka miaka na miaka kwa uwanja wa bukoba ndege kushindwa kutua ni jambo la kawaida sana,Labda kuusaidia uwanja huo kupunguza matatizo hayo ni kuweka taa kwewnye runway,
kwa wanaojua mambo ya ndege (aviation) hakuna jipya hapo kwani ni taratibu za kawaida tu , kwenda uwanja mwingine wa karibu hali ya hewa ikiwa mbaya au kukiwa na kizuizi kingine chochoteNdege ya Air Tanzania imeshindwa kutua Bukoba Airport imerudi Mwanza.
Stay tuned
======
UPDATES
Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) imeshindwa kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba mkoani Kagera kutokana na hali mbaya ya hewa. Badala yake ndege hiyo imelazimika kutua salama katika uwanja wa Mwanza.
Alipoulizwa kwa simu leo Alhamisi Novemba 17 kuhusu tukio hilo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Hamza Johari amethibitisha tukio hilo.
“Ni kweli nimepata taarifa ndege ya Air Tanzania imeshindwa kutua kutokana na hali mbaya ya hewa, kulikuwa na ukungu, mvua, radi na giza uwanja ukawa hauonekani, kwa hiyo rubani akafuta safari na kurudi Mwanza na ametua salama,” amesema.
Awali taarifa iliyotumwa na Mbunge wa Viti Maalum, Neema Lugangira kwenye mitandao ya kijamii ilieleza tukio hilo.
“Still shaken lakini Mungu ni Mwema. Nimepanda ndege asubuhi ya leo kwenda Bukoba. Safari ilikuwa na changamoto, tumefika lakini ndege ikashindwa kutua.
“Nampongeza rubani kwa uamuzi sahihi wa kurudi Mwanza na sasa narudi Dar. Serikali ibebe kwa uzito suala la airport mpya Bukoba,” ameandika.
Hali hiyo imejitokeza zikiwa zimepita siku 11 tangu ndege ya shirika la Precision ilipoanguka katika ziwa Victoria na kusababisha vifo vya watu 19 na wengine 29 wakaokolewa.
Chanzo: Mwananchi
mmmmm!!!hilo ndio nalisikia leo kuwa ndege ina piga alarm ya low fuel,pasipo kuwa na dharura yoyote ile iliyojitokeza ikiwa angani!!!!??labda imezunguka sana kutokana na kushindwa kutua, uwanja iliyokusudia ,kutokana na labda matatizo ya kiufundi au hali ya hewa kuwa sio rafiki.Huwa yanaisha mkuu.
Niliwahi toka Pemba na hizi ndege ndogo nilibahatika kukaa pale mbele na pilot nilikua naona kinachoendelea.
Ndege ilikua inapiga alarm low fuel lakini tuliruka toka pemba mpaka unguja kufika pale unguja hakujaza mafuta akaruka mpaka Dar, jamaa alirisk mno. Ni Mungu tu ndio alitulinda ila yule pilot hakuna makini.
Chato Ipo Jirani Sana Yeye Anakwenda MwanzaKwanini rubani asitue chato mpaka aende mwanza?
Huenda huyu kajifunza kupitia yule alieanguka! Ajali haina kingaYule rubani wa ndege iliyoanguka angefanya kama huyu angeepusha ile ajali, haya matukio ni ya kawaida hasa hali ya hewa inapokuwa hairuhusu kutua uwanja uliokusudiwa.
ccm huwa nibwatu wa hila sana.Kama suala lilikuwa kushusha abiria kwanini asishushe Chato kama sio chuki na ubinafsi wa kutaka uwanja ambao sio kigezo cha kuwezesha kutua kama hali ya hewa hairuhusu huwezi kutua hata kama ni Dar, KIA au Mwanza.
Sasa huyo mbunge alikuwa anaenda kufanya nini Bukoba kama baada ya ndege kuahirisha kutua hapo ikaenda Mwanza kwanini asingeshuka hapo na kwenda kwa meli au basi? Majivuno tupu
Bukoba ni lango la kuzimu kila tukio baya linaasisiwa huko kabla halijasambaa kwenda kwingine
Hata Songwe, fastjet iliwahi kushindwa kutua ikabidi irejee Dar!!Ni kawaida sana hiyo kwenye ndege..kuna siku ndege ya usiku tulikua tumetoka Dar to mwanza na fastjet ile ndege ya mwisho saa nne usiku ilishindwa kutua mwanza airport sababu mvua na hali ya hewa,tukarudi Dar tena.
Baada ya kama 3 hours tukaamsha tena kwenda mwanza..tulifika almost kunakucha . Nilijuta sana kupanda ndege ya mwisho
Hivi Iringa uwanja ni mdogo sana?Hata Songwe, fastjet iliwahi kushindwa kutua ikabidi irejee Dar!!