Hypersonic WMD
JF-Expert Member
- Apr 11, 2024
- 1,337
- 1,876
Kampuni ya Airplanes Africa Limited (AAL) yenye makao yake Morogoro, imetangaza kuanza safari za ndege tatu za kwanza zilizotengenezwa Tanzania, aina ya Skyleader 600. Mkurugenzi wa AAL, Bw. David Grolig, alisema ndege moja imetua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kama sehemu ya uzinduzi.
Pia, soma: Ndege ya Kwanza kutengenezwa Tanzania yazinduliwa
Grolig alithibitisha kuwa kampuni yao imepata kibali cha mamlaka husika baada ya kuthibitisha ubora wa ndege hizo, ambazo ni za kisasa na zina viwango vya kimataifa. Ndege hizi, zikiwa na uwezo wa kubeba abiria wawili pamoja na rubani, ni suluhisho bora la usafiri kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla.
AAL, kampuni ya kwanza Tanzania kutengeneza ndege za aina hii, imetengeneza ndege hizi kutokana na mazingira mazuri ya uwekezaji nchini. Gharama za kununua ndege hizo ni nafuu kama kumiliki gari. Ndege hizo pia zilioneshwa katika Maonyesho ya Watengenezaji wa Bidhaa ya Tanzania (TIMEXPO 2024) yanayoendelea katika Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Pia, soma: Ndege ya Kwanza kutengenezwa Tanzania yazinduliwa
Grolig alithibitisha kuwa kampuni yao imepata kibali cha mamlaka husika baada ya kuthibitisha ubora wa ndege hizo, ambazo ni za kisasa na zina viwango vya kimataifa. Ndege hizi, zikiwa na uwezo wa kubeba abiria wawili pamoja na rubani, ni suluhisho bora la usafiri kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla.
AAL, kampuni ya kwanza Tanzania kutengeneza ndege za aina hii, imetengeneza ndege hizi kutokana na mazingira mazuri ya uwekezaji nchini. Gharama za kununua ndege hizo ni nafuu kama kumiliki gari. Ndege hizo pia zilioneshwa katika Maonyesho ya Watengenezaji wa Bidhaa ya Tanzania (TIMEXPO 2024) yanayoendelea katika Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
