Ndoa ilivyoteteresha imani yangu (Kisa Cha Kweli)

Ndoa ilivyoteteresha imani yangu (Kisa Cha Kweli)

Abdallahking

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2018
Posts
3,985
Reaction score
10,840
Mkasa : NDOA ILIVYOTETERESHA IMANI YANGU
Mwandishi: IRENE MBOWE (Irene Mbowe Kungwi Lao)
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES





Hiki ni kisa cha ukweli kabisa, anachokielezea Flora, Mwanamke ambaye anakiri Imani yake kutereteka kwa sababu ya Ndoa yake. Alikuwa na alilelewa kwenye familia yenye maadili mema. Na aliogopa dhambi kama ukoma, Na baada ya kumaliza elimu yake , na kufanikiwa kupata kazi, bado alikuwa ni muaminifu kwenye imani yake vibaya mno. Lakini baada tu ya kuolewa mambo yalibadilika. Hembu ongozana na mimi msimuliaji wako Irene Mbowe katika kisa hiki cha ukweli, chenye,, KUFUNDISHA, KUBURUDISHA NA KUADIBISHA.


SEHEMU YA KWANZA: MAISHA NA FAMILIA YA FRORA.
PART 1


Nilizaliwa kwenye familia ya wazazi wasomi, wenye kujua nini maana ya familia, mama yangu na baba yangu siku zote walikuwa wakinuia mamoja, walipenda na kutulea kwa upendo wa hali ya juu.

Tulijikuta sisi watoto tukiwa watoto wenye adabu sana na kusifiwa sana mtaani kwetu, wengi walifikiri baba yetu ni mchungaji lakini ukeli hakuwa mchjungaji ila alikuwa kama mchungaji kutokana na matendo yake na utu wake na namna anavyoishi kwa upendo na mkewe na wanawe.. Hiii ndiyo ilikuwa familia yetu familia ya mzee george maliki.

Tulipenda sana imani yetu, tulipendana sana sisi kwa sisi, na kwa vile tulikuwa tumelelewa kimaadili kila mmoja alipata elimu nzuri sana, mama yetu alikuwa ni nesi na baba yetu alikuwa ni mfanyakazi serikalini, hivyo pesa zao kwa pamoja zilitulea kwa kuhakikisha tunapata huduma na malezi bora, kipindi cha kumaliza mitihani ya kidato cha nne mama yangu na baba yangu waliniambia endapo nitafauli vyema basi wangenizawadia zawadi nono sana, wakati huo kaka yangu na dada zangu walikuwa tayari wako vyuoni, na mimi kama binti wa miwho kwa kudeka sana walifikiri singefanya vizuri.

Lakini nilijitahidi sana kuhakikisha nafauli masomo yangu vyema. Haikuwa hivyo baada ya matokeao, nilifeli na kupata devision 0. Mwaka 1991. Nilijisikia vibaya sana, kwani mama yangu alilia. Baba yangu alinitia moyo sana, vijana wenzangu kanisani walinicheka na kuniambia kwa nini skuwa makini kwenye masomo? Dada zangu hali kazalika walinicheka sana, lakini kaka yangu aliniambia nikisoma tena na kurudia kidato cha nne nitafaulu, na alimshauri baba yangu na mama yangu nirudie mitihan yangu.

Na hivyo sasa nilisubiri mwaka unaokuja ili nirudie mitihani yangu. Kaka yangu aliniambia nikiomba mungu nitafaulu na kikitia nia nitafaulu kikubwa nisome na kuatia nia. Alinitia maoyo sana, na kuanzia hapo nikaona ninaweza. Hivyo nilianza tena kidato cha nne katika shule nyingine. Maombi yangu siku zote yalikuwa mungu ifungue akili yangu nielewe vyema, ahivi ndivyo niliomba kila siku.

Na kweli nilifunguliwa akaiali na kuelewa kwa haraka sana, lakini pia niliomba kukumbushwa nisiwe msahaulifu na nikawpewa kumbu kumbu mzuri sana. Nilifanya maajabu kwenye mtihani wa kufunga shule mitihani ya pre natinaonal mama yangu na baba yangu hawakuamini kuona report yangu, nilipata devision 2. Hesabu ambayo nilikuwa napata f, sasa nilipata c. Ilikuwa ni maajabu kwa familia nzima.

Kaka yangu aliniambia ninaweza kufanya maajabu zaidi kwa kusoma, kutia nia na kuomba mungu akaniusia nisiache kuomba kwani yeye ndiye ambaye imemsaidia sana. Nilirudi shule kama mfalme,, nilifungashiwa kila kitu nilichotaka,, nilipewa kila kitu kizuri na wazazi, babayangu alinifurahia sana, mama pia alikuwaakailia machozi ya furaha sana, nilirudi shsuleni kwa ajili ya mitihani yangu, kipindi hicho nilikkuwa naona wanafunzi wenzangu wakiwa na boyfriiends, niliwashangaa sana.

Wanawezaje kuwa na wachumba ili hali ni wadogo vile, wengi wlinicheka na kuniita mteule ama mlokole ama sister,, jina lililojulikana kulkiko jina langu halisi la flora. Kipindi cha mitihani kilipofika sikuwa nafanya lolote zaidi ya kuomba tu, kwani nilishasoma sana, hivo niliamua kufunga siku 11 kwa ajili ya mitihani yangu niliyokuwa naifanya. Nilishangaa sana, mar ya kwanza niliingia kwenye mtihani wa siasa,, nilishangaa nilivyoweza kuufanya vyema mpaka nikawa ninacheka..

Kisha kwenye mtihani wa biology nao hali kazalika nilishangaa sana na kujiuliza je ni mtihani ama ni mchezo? Mitihani ya mwanzo ilinipa roho ya kutoogopa mitihani ijayo, hivyo nikaendelea akuomba mungu anikumbushe yote niliyosoma na hivi ndivyo kaka yangu alinipa maelezo kwambna nisisome ila niwe namuomba mungu kwani nilishasoma sana kipindi cha nyuma, na hii ilifanya wengi waone kama nimechanganykiwa na kuonekana mpumbavu,, lakini sikujali. Nilimaliza mitihani yangu yote na kurudi nyumbani.

Niliwaeleza wazazi wasijali nitafanya maajabu,, walikwua wakicheka sana, mkesha wa krismas tukiwa tunatoka kanisani, kijana mmoja alinifuata na kuonekana kunihitaji, niliogopa sana nikijua ni dhamabi kubwa na nilikumbuka amitihani yangu na kusema nikifanya hii dhambi nitafeli mitihani yangu, hivyo nilikataa kabisa nilionekana kusichana aliyekomaa lakaini sikutaka kujiingiza kwenye mahusiano ya mapenzi, nilirudi nyumbani nikiwa na hofu ya kutenda dhambi hiyo.

6 (1).jpg
 
SEHEMU YA KWANZA: MAISHA NA FAMILIA YA FRORA.
PART 2


Imani ya kufunga na kuomba iliniingia sana na kuona ni jambo lenye ukweli na mafanikio, hiviyo kila kitu changu nilichotaka nilifunga na kuomba na kilifanikiwa kwa asilsimia zote, na sasa nilianza kuombea matokeo yangu kwa kufunga na kuomba na siku zote niliomba kwa kufunga kwa siku 11 mfululizo nikiwa nafunga tu.

Na nilipomaliza maombi baada ya muda matokeo yalitoka, kila ndugu yangu alikuwa na shauku ya matokeo yangu, kla mmoja alitaka kuona matokeo yangu, kaka yangu aliyekuwa karibu na matokeo ndiye ambaye alikuwa ana shauku kubwa mno.

Siku ya jumatano nikiwa natoka kwa fundi kwa ajili ya kuchukua nguo yangu ya sherehe kwa maandalio ya pasaka, nilifika nyumbani na kumkuta baba yangu akinisubiri kwa hamau, alinikumbatia na kuniambia binti maajabu.

Nilimwambia enhe baba niambie, kisha kaka yangu mama yangu na dada yangu mmoja aliyekkuja likizo kwa pamoja walitoka kwa pamoja wakiaimba ule wimbow a “mungu amenihuruumir tendo hili kubwa ssana sikustahilii jambo hili nimelipata bure tu,, sasa na iamba. Nasifu ni huuuruma tu, nasifu ni huruma tu ” nisingeweza kuzuia mahcozi yangu kwani kila mmoja alikuwa analia zaidi sana mamaa, lakaini baba na kaka walikuwa wakicheka, na kisha aliniambia wewe ni binti maajabu, umefaulu sanaa nilianza kupata shauku ya kutazama matokeo yangu,,, na mara niliyaona,, sikuamini nilifurahia sana, nilipata devition one..

Iliyonyooka, nilimsifu sna mungu na kumshukuru kwa upendo wake na huruma zake,, na sasa kujiona msomi kama ndugu zangu na baba yangu na mama yangu. Nilichaguliwa kwenda kwenye shule ya vipaji maalumu, kutokana na kufaulu kwangu. Kaka yangu aliniambia nikiendelea kuogopa dhambi akisisitiza auzinzi aliniambia nitafanya maajabu katika elimu yangu.

Na kujulikana sana, na kweli niliamua kusimamia elimu yangu, na nilimaliza elimu yangu ya kidato cha sita na kuchakugliwa kwenda chuo. Nilikaa miaka yote chuoni kwa heshima ya hali ya juu, na nilimaliza masomo yangu na kuanza kazi kwani niliomba pia nipate kazi nzuri na niipendayo, kama kawaida yangu nilifunga na Kuomba kwa ajili ya kazi na ilikuwa hivyo.
 
SEHEMU YA PILI: UCHUMBA NA NDOA.
PART 1



Nikiwa msichana mrembo sana, mcha mungu na msomi, nilipendwa na wanaume wengi wenye pesa zaoa na elimu zao , lakini niliogopa sana kumtenda mungu dhambi. Na sasa nilisema kijana atakayenifuata nitakubali kuolewa. Naye endapo nitamridhia, na sasa nilianza kuwa na mahusiano an kijana mmoja niliyempenda sana. Nilimuamini, nilimpnenda kwa shati, kila mmoja alimwambia umepata mchumba mwema. Na mrembo na msomi.

Kwa vile wazazi wangu waliishi kwa upendo nilijua hizo ndizo ndoa. Lakini sikuwahi kuwa na marafiki wengi ambao wangrnifanya niogope ndoa. Marafiki zangu wote ni wasichana wataratibu wenye mahusiano ya heshima ma matokeo ni ndoa. Hivyo hili lilinifanya nijue naolewa kwa salama na si kashi kashi.

Elimu ya mchumba wangu ilikuwa juu sana. Na aliniambia atanioa kisha anapaswa kusoma tena miaka 5 kwa ajili ya kukiendeleza kielimu apate mshahara mnono na maisha mazuri. Na akasema anataka kuoa kisha ndo aingie kwenye elimu. Na tulikubaliana hivyo. Haraka sana deusi mpenzi wangu wa moyotulioana naye. Baada ya kuolewa nilipendeza sana. Na kuona haya ndiyo maisha. Raha ya ndoa. Mapenzi moto moto.

Tuna elimu pesa na kila uzuri wa maisha. Na haraka sana nilibahatika kubeba ujauzito. Hapo ndipo niliona ndoa ni paradiso. Nilipendwa sana na deusi. Tuliitwa kumbi kumbi. Na baada ya kujifungua wanangu mapacha alinisaidia kwa hali na mali. Na kuniwekea wasichana wa kazi 2. Ambao ni ndugu zao huko kijijini. Nilipendeza sana na uzuri wamgu kuchanua. Sura yangu iling’aa sana na kuoneka a mrembo wa haja. Deusi alianza kupata wivu jui yangu na kunichunga sana. Na sasa safari ya shule pole pole alianza kuipotezea.

Lakini akiamini nitamuacha. Hivyo hakuliongelea tena. Bado haikunisumbua. Nilikuwa mwema sana kwa mume wangu nilimpenda nilimheshimu na kumhudumia sana. Nilifanya kama mama yangu alivyokuwa akifanya. Niliendelea na maombi yangu kama kawaida. Sikuacha hata kimoja. Kanisani nilipendwa na kuanza kupewa vyeo mbali mbali. Nilikuwa mwenyekiti wa uwt…

Nilikuwa mlezi wa vijana.. Nilikuwa kjongozi wa maombi ya wanawake waombolezaji. Niliheshimika na kuonekana nyota ing’aayo. Wengi mtaani walinipenda sana na kunitaka niwashauri na kuwasaidia kwa mambo mengi. Nilikuwa mwanamke kijana wa nguvu. Nilivalia mavazi ya heshima ya hadhi. Mavitenge ya bei ghali ndiyo nilivalia. Nilikuwa na pesa ya kutosha kununua kila nilichotaka.

Nyumba nzuri gari ya kutembelea ya mume wangu nzuri watoto wazuri na maisha ya kifahari mazuri. Kila rafiki yangu alisema flora na deusi mmebarikiwa. Mume wangu alipendeza sana. Na kunipenda pia. Ndugu zake deusi walisema mke wa deusi anadeka.. Kadekezwa na kunionea wivu.

Lakini sikuwa ninadeka ila nilipendwa tu. Maisha yalisonga sana. Mume wangu hakuwa mlevi kabisa. Na hanywi kileo chochote. Siku moja akanitaka tutoke. Tena sherehe ya kikazi kama boss yeye. Tulienda shereheni na kuanza kula na kunywa. Wanaume wengi walinikodolea macho.

Nilianza kuogopa mume wangu angeona. Kisha alimiambia flora kumywa wine kidogo… Mh… Nilishangaaa nikakataa. Yeye akanywa glass mbili kisha tatu kisha nne. Na kuamza kulewa. Na sasa hali ya ulevi ikawa inamshawishi anipe na mimi. Nilikataa kata kata. Akiwa kasimama huku anaongea kilevi na maneno ya kejeli aliniwasha kibao kimoja shavuni cha nguvu mpaka nikaona cheche…
 
SEHEMU YA PILI: UCHUMBA NA NDOA.
PART 2


Nilimtazama na kushangaaa… Kisha akarudia kingine na ndipo nikaamini si yeye bali kuna shetani ndani yake. Nililia ma kuanza kuondoka huku marafili wakinisihi nibaki. Naarafiki ma wake zao nao ni walevi. Niliamua kuondoka kuepusha shari. Nilifika home na luanza kulia lwa uchungu wa hali ya juu nisijue nifanyeje. Uso ulibakiza alama za vidole. Nilioga niliomba mungu na kulala. Saa saba usiku kwa mara ya kwanza nilishtuka na kujikuta niko mwenyewe. Kisha honi ya gari iliita. Nilienda kufungua mlango na kumpokea nikiwa na hasira ya hali ya juu.

Na alipoingiza gari aliniburuza ndani kwa kipondo cha hali ya juu na kuniambia nilikuwa najionyesha kwa wanaume ili wanitongoze. Majaribu kwa flora yanaanza: Nilipigwa kama nyanya. Nilishangaa sana. Sikulala chumbani bali jikoni kwa kujibanza banza ili watoto wasinione. Asbh nilijitazama kwenye kiyoo na kujishangaa nilivyokuwa nimeumia. Aliamka asbh na kujiandaa akaondoka na kuniambia haishi na malaya.

Niliumia sana. Niliomba ruhusa kazini na kwenda kwa mama yangu kumuelezea kisa kizima. Mama alinishangaa na majeraha. Baba aliumia sana na kusema nisiondoke ila atamuita na kumkanya alichofanya ni hatari. Na baadae baba alinituma kwa wadhamini ili nikae huko mume aje. Jioni mume alipigiwa simu na wadhamini na hakuonyesha kujali. Baadae sana alikuja na kusema alilewa nimsamehe.

Kirahisi tu hivyo. Nilishangaa. Nilirudi nyumbani kwa makubaliano akinipiga tena basi. Kwa vile nilikuwa na hasira ilikuwa ngumu kumchekea. Alimiambia anatola akacheke na wengine. Na kweli aliondoka. Alirudi saa sita usiku akiwa kalewa. Nilianza kuogopa kupigwa na hivyo niligungua mlango na kunyamaza kimya kuepusha kupigwa. Aliingia ndani na kusema hataki maswali. Sikumjibu nilinyamaza.

Asubuhi kama kawaida aliondoka zake bila salamu wala kutaka kujua lolote. Ilikuwa ni siku ya maombi. Nilienda kanisani kuongoza kipindi. Nilikuwa na mzigo mzito moyoni . Sikuona upako wala njia kufunguka. Kipindi hakikuwa kizuri kama siku zote. Na hivyo sasa ilibidi niwe wazi kwa wenzangu. Niliwaelezea kila kitu. Na waliniambia tuombe. Tuliomba ila bado sikuweza kububujika. Nilikuwa na hasira sana. Na chuki moyoni. Wenzangu walinihurumia na kuniambia hilo ni jaribu kwa kazi njema niifanyayo. Na hivyo lazima nilishinde.

Sikuwa nawaelewa. Umsamehe akupigaye how?mume mlevi how?roho iliingia chuki mbaya. Nilirudi nyumbani na kumkuta mume amekaa sebuleni. Ilikuwa ni saa kumi na mbili jioni. Alianza kuniambia nimetoka wapi. Nilimjibu kanisani…. Kisha akarudia kwa kejeli kanisaniiii..

Na kunifyonza. Nilichukia sana na kupitiliza jikoni. Alinifuata huko huko na kunipiga sawa sawa. Niliumia sana. Nililia sana. Nilikumbuka nilivyojiyltunza usichana wangu na kumtukuza mungu iweje aniache?nililia. Hakujali. Alioga na kuondoka na kuniacha. Tena safari hii kwa kuchukua kibegi kidogo na kuondoka. Niliumia sana. Nililia sana. Haraka nilimueleza mama kila kitu.

Mama aliniambia tukutane mahali tuzungumze tena kanisani kwani hakutaka mume ajue tunazungumza. Usiku kucha nililala peke yangu. Mawazo. Nilikesha kwa kuwaza. Nilimchukia deusi vibaya mno. Haswaaa. Sikumpenda kabisa. Asbh nilielekea kanisani tulikutana na mama. Nililia mno.

Nilimuelezea mama kila kitu. Ndani kanisani wenyewe. Mama aliniambia mwanangu wewe umekuwa muaminifu sana. Shetani anakuonea wivu. Anataka kukuvuruga. Na kaona hapa nfipo pa kukuvuruga. Msamehe mumeo na muombee. Akaniambia mwanangu usiposamehe unazaa chuki na kisasi. Kisasi ni kibaya sana hakitendi haki ya mungu. Hivyo samehe kwa faida yako kwanza.

Kisha faida ya wanao alafu mumeo. Sikuwa namuelewa mama. Niliona anaongea pumba. Aliniambia mwanangu samehe. Nilikataa kata kata. Alijaribu kunisihi sana lakini sikumuelewa kabisa. Nililia mno. Aliniombea sana. Kisha akaniangalia na kuniambia flora umekomaa. Wewe ni mwanangu. Ni mke na rafiki yangu.

Je unaweza kutofikiria ubaya nikupe kisa changu? Nilimtazama kisha nikamuona akidondosha machozi.. Nilipata hofu na kutamani kumsikiliza mama. Nilitaka kujua ataniambia nini juu ya kisa chake.Je alipigwa na baba? Kama ndio aliwezaje kusamehe? Je, alifanyajwe na baba ili hali walipendana hivyo?nilimtazama mama ambaye bado alikuwa akilia sana na kudondosha machozi mengi na kujifuta na khanga yake makamasi. Kisha nikamwambia mama ndio nataka kukusikiliza. Niambie. Moyo wangu ulianza kuingia baridi na chuki ya jambo nisilolijua.
 
SEHEMU YA TATU: MAISHA YA MAMA YAKE FLORA.
PART 1


TULIKUWA TUMEKAA TU KANISANI MIMI NA MAMA YANGU. TULIONGEA KWA SAUTI YA CHINI SANA . KANISA LILIKUWA NA MWANGWI. KILA MAMA ALIPOPENGA MAKAMASI SAUTI ILISIKIKA SANA. KISHA AKANIGEUKIA NA KUNIAMBIA…”Flora ndoa ni kitu kingine na kumtumikia Mungu ni kitu kingine.

Ndoa yako unaipenda sana. Ila kumtumikia Mungu ni jambo jengine kabisa. Mimi nilitumika sana kanisani nilipokuwa msichana. Miaka hiyo wazazi hawakujua thamani ya elimu. Nilikaa kanisani kwa uaminifu sana. Kazi yangu kanisani ilikuwa ni kufanya usafi na kufuma vitambaa vya Madhabahu ya Bwana.

Niliimba kwaya pia. Sauti yangu nzuri sana kwa kwaya. Nakumbuka miaka hiyo hakukuwa na vyombo vya muziki kama sasa hivi. Tulitumia ngoma kinanda na makopo ya mawe. Lakini niliiomba vyema sana na kubariki wengi sana. Na kama unakumbuka wimbo unaoimbwa sasa hivi kanisani na kwaya kuu ni mimi niliutunga. Ule usemao… Mama alianza kuuumbia nao ulisema hivi…

Verse 1:
Umeanza safari ya mbinguni usigeuke nyuma… ukiwa nayo nia njema mbinguni utafikaaaa

Solo:
Mbinguni hakitaingiaaa.
Mbinguni eeeeee
Wote: kinyonge wala kidhaifuuuu katika mbimbu ya Utukufu watakuwepo waluotakaswa..

Solo:Mbinguniiiiiiiiiii
Wote:Mbinguni…..

Verse2
Mke wa lutu aliiianza safari kwenda Soari
Lakini aligeuka nyuma akawa jiwe la chumvi..

Chorus…..

NILIKUMBUKA WIMBO HUU NA SAUTI YAKE NZURI. MAMA HAKUWAHI KUNIAMBIA ALIWAHI KUWA MTUMISHI KANISANI WALA MUIMBA KWAYA. NILISHANGAA ALIWEZAJE KUTUNGA WIMBO MZURI NAMNA ILE. SAUTI YAKE NZURI NA YENYE MVUTO WA HALI YA JUU. NILIVUTIWA SANA. KISHA MAMA AKAENDELEA.

Mama aliendelea kuniambia. Niliimba sana mwanangu. Nilifanya kazi nzuri kanisani. Walikuja wamisionari na kunipeleka shule ya unesi. Nilisoma vyema na wakanipeleka nje ya nchi kwa masomo na kupata degree huko. Kisha nikaolewa na baba yenu. Sikuwahi kuacha kazi ya kuhudumia kanisa kila nilipopata nafasi mara baada ya kazi yangu.

Mungu alinibariki sana. Baba yenu alianza vituko baada ya kupandishwa cheo kazini. Na baada ya muda alifukuzwa kazi. Nilimlilia Mungu na akanisaidia sana na kunipandisha cheo kazini nikawa mkubwa wa manesi. Na mkunga mkuu niliyejulikana sana. Lakini ni kwa sababu nilimuamini Mungu na shetani alinimatisha tamaaa. Kanisa lilifungua hospital na nilienda kusoma tena kwa ajili ya kusimamia hospital hiyo.

Nilifanya vyema. Nilikaa ulaya miaka 2. Kisha nilituma nauli baba yako na ndugu zako wakaja tukakaa kwa miaka mingine 2. Na kisha tukarudi na baba kunishukuru sana na kuanza kutafuta kazi kwani kule alisoma kozi mbali mbali na kuwa msomi mzuri sana. Sikubesabu ubaya wake ila nilisema nafanya huruma kwani Mungu alinihurumia mimi kuwa nesi niwaangalie ninyi…
 
SEHEMU YA TATU: MAISHA YA MAMA YAKE FLORA.
PART 2



Mama aliendelea kuongea huku akibubujikwa na machozi…. nilimsikiliza lakini bado sikuona unyama wa baba. Na sasa nilitaka kusikia unyama gani baba alimfanyia mama… bado niliona baba hana tatizo kama deusi. Mama alisita kidogo kuendelea kuzungumza kisha akalia sana kwa sauti ya juu. Na baada ya hapo mama alinitizama na kuniambia Flora narudia tena je una nguvu za kutoweka kisasi?

Nilimtazama mama na kumwambia ndio. Mama Aliniangalia kisha akaniambia nimfunue mguu wake. Nilimfunua mguu wake mpaka kwenye paja lake.. nilishtuka kuona nilichoona… sikuamini…. nilimtazama tena mama kwa makini sana na kumuuliza mama ni nini hiki?aliniambia umeona nini?nilimwambia mama nimeona kama sijaona….

Niliona kitu cha ajabu sana. Mama alikuwa na mguu wa bandia.. nilisimama kwa mshangao… kwa miaka yangu 26 sikuwahi kulijua jambo hili. Tuliamini mama yetu alizaliwa akichechemea kumbe hakuwa na mguu.. nilishtuka… nilimuuliza mama ni nini hiki? Mama alifuta machozi na kuniambia je unajua jina baba yako analoniita?nilimwambia ndio najua. Akaniuliza ananiita nani?nilimwambia anakuita NYOTA…ndio mwanangu.

Mimi ni nyota. Nang”aaa duniani na Mbinguni. Baba yenu nilipomuita ulaya alikuja na kisha aliendeleza ubabe wake. Na siku moja akiwa kalewa alinipiga na nilidondoka kwenye ngazi na mguu kuvunjika. Na kwa kuogopa atafungwa kutokana na sheria za kule baada ya kuniomba msamaha sana nilificha kosa na mguu ukaoza. Na hivyo ulikatwa. Lakini nilimsamehe.

Tulirudi Tanzania hakuna aliyejua. Hata mchungaji wala wazazi wala watoto. Nilitoa msamaha wa moyoni. Na leo hii nimekuambia ukweli ili ukusaidie. Nataka uwe nyota kwa Mumeo. Na ninakusihi toa siri zote ila hii kamwe usimwambie mtu tafadhali mwanangu. NILILIA SANA KWA MAELEZO YAKE. KISHA MAMA AKANIKUMBATIA NA KUNIAMBIA NIAHIDI HUTASEMA. nilimtazama nikilia sana na nikamwambia Sitasema.

Baba yenu aliporudi Tanzania alipata mafanikio makubwa sana. Alikuwa boss mkubwa sana serikalini. Alipata pesa nyingi sana. Lakini hakuwahi kuwa mlevi wala mzinzi. Wengi walimuita luther.. alionekana mtanashati sana. Na mwanaume mzuri sana. Lakini alinipenda vibaya mno.

Alikuwa muaminifu vibaya mno. Niliishi kama Nyota. Kwa furaha na amani. Alinisaidia kila kazi ngumu. Na hakuna aliyewahi kujua sina mguu. Wote niliwaficha. Ilikuwa ni rahisi sana. Nilisema nina ugonjwa wa visigino hivyo muda wote nilivaa soks na raba nzuri sana. Na ninyi hamkuwahi kulijua hilo.

Nilipotaka kupumzika tulifunga chumba na kuvua mguu na nilikaa kwa muda ndani na baba tukizungumza na hamkuruhusiwa kuingia. Na hata mlipoingia mlinikuta kitandani nimejifunika na hamkujua lolote. Hivi ndivyo niliishi. Na ilawa siri kubwa sana. Wengi wanajua nina matatizo ya kisigino kama ulivyojua na wewe na wenzako.

Je unaweza kumsamehe mumeo kwa kosa la kukupiga na kulewa? Nilimtizama mama nikamwambia naumia kwa nini anipige naumia. Mama alisisitiza nimsamehe na nisisimulie tena mtu matatizo ya mume wangu. TULIMALIZA KUONGEA. MAMA AKANIAGA. NJIA NZIMA NILILIA. NILISHANGAA JINSI AMBAVYO MAMA AMEWEZA KUFICHA SIRI HII. KWELI ALIMSAMEHE BABA. KWELI ALIMSAMEHE. NILIFIKA NYUMBANI NIKIWA HOI NIMECHOKA KWA MAWAZO AKILINI.
 
SEHEMU YA NNE: NYUMBANI
PART 1

NILIFIKA NYUMBANI AKILI IKIWA IMENIVURUGIKA. NILIMTAZAMA MAMA YANGU NA KUKUMBUKA SIKU MOJA ALIANGUKA AKIWA ANATOKA KAZINI. NILIMUONA ILA ALINITUMA KUITA JIRANI. NA SIJUI ALIJIBURUZAJE NA NILIMKUTA CHUMBANI NA ALISEMA BABA AKAITWE HARAKA SANA. ALIJIFUNGIA CHUMBANI NA JIRANI ALIVYOKUJA ALISEMA ANAOGA YUKO OKAY. KISHA BABA ALIITWA NA WALIKAA CHYMBANI KAMA KAWAIDA YAO. SASA NILIANZA KUPATA PICHA ALIKUWA MBOVU WA MGUUU NA HAKUTAKA NIONE. NILIKUMBUKA PIA NAMNA ANAVYOPENDA KUDANCE NA MOTION YAKE ILIVYO.. NILIANZA KUPATA PICHA ALIVYPKUWA AKIDANCE TENA NA BABA AKIMSHILA NA WAKICHEZA KWA FURAHA. NILIPATA PICHA SIKU YA MAHARI YANGU ALIVYOKUWA AKICHEZA KWA FURAHA SANA. NILIENDELEA LUSHANGAA. NILIKUMBUKA KITU KIMOJA… MAMA ALIMSAIDIA SANA MKE WA KAKA YANGU KWA UZAZI NA MKE WA KAKA YANGU ALIWAHI KUKAA CHUMBANI NA MAMA WAKIZUNGUMZA KWA MAMBO YAO YA KUSULUHISHA UGOMVI… JE WIFI YANGU ANAJUA?JE DADA YANGU ANAJUA?DE DADA YANGU ANAJUA?JE KAKA YANGU ANAJUA?NILIWAZA MENGI. NILITAMANI KUONGEA NAO MMOJA MMOJA. NA NILITAMANI PIA KUMWAMBIA BABA KWAMBA NIMEJUA UPENDO WAKE NI WA KINAFIKI NI KWA VILE ALIMUUMIZA MAMA NA SI UPENDO WA DHATI…. NILIPATA HASIRA GHAFLA NA KUPANGA SAFARI YA KUMUONA BABA.
 
SEHEMU YA NNE: NYUMBANI
PART 2



Nilikumbuka sauti ya Baba ikiita Nyotaaaaa.. na mama aliitika kwa furaha sana na kuachia tabasamu lake na kufanya mwanya wake uonekane. Kisha baba alimsogelea na kumbusu mama yangu katika paji la uso… picha hii ilinijia na kuona busu lile ni la usaliti. Kama la Yida Eskariote aliyemsaliti Yesu kwa Busu. Nilimchukia Baba kuanzia hapo. Niliumia sana. Nilijuta nimejua ya nini. Nikiwa yumbani mume wangu alikuja na hakunisemesha lolote. Na mimi kwa kiburi sikumsemesha lolote. Nilinyamaza. Tulanuniana. Asbh nilienda kazini. Sikuwa na furaha. Mume aliondoka na yeye. Kila mtu kwa namna yake. Mchana nikiwa kazini baba yangu alikuja lumiyembelea. Alitaka kujua naendeleaje. Moyo ulinipasuka kumuona… kisha aliingia ofcn kwangu akiwa na tabasamu. Baba alinipenda sana. Alishangaa sijamchangamkia nilikuwa namuona kama sijui nini. Nilitamani kumtemea mate.Baba alinisogelea na kuniambia mwanangu samehe. Msamehe mumeo. Mungu atakusamehe na kikujalieni mafanikio mengi. Kuna baraka za mafanikio tele kwenu msamehe mumeo. Kidogo simanzi ikaniingia. Nikaanza kupata huruma. Nikamkumbatia baba. Nikamuona alivyo na upendo kwa kuweza kuacha uzinzi na ulevi kwa ajili ya mama. Niliona sasa sura mpya. Alijinyima starehe na anasa kwa ajili ya mke wake. Nilimuona hodari sana . Kwanza nilihisi mama alipokosea ilikuwa ni lazima amsamehe ili asikumbuke mguu. Sasa nilitaka kujua baba naye aliwahu kumsamehe mama?nilimuuliza baba je umewahi kuuziwa na mama ukamsamehe?baba alinitizama na kuniambia mwanangu hakuna mwanadamu asiyekosea ila kusamehe ni lazima. Nilimuuliza ni nini ambacho mama alikukosea na ukamsamehe ili niweze kupata nguvu ya kusamehe.Baba alinitizama. Kisha akaniambia mwanangu nakupenda na nitakueleza. Ila iwe siri yako tu. Usimwambie yeyote yule. Nilimwambia sawa baba. Baba aliniambia kwamba mama alikuwa mvivu sana. Hakuweza kufanya kaxi za mikono. Na alikuwa akigombana na wasichana kila siku. Na alifukuza wasichana wote. Na hivyo kwa uvivu wake niliweza kumvumilia kumpenda na nilifanya kazi zote. Niliitwa mume bwege lakini nilimsamehe mke wangu na sikujali. Miaka yetu mwanamke hakuwa na sauti. Lakini mama yenu alikuwa na sauti . Ila kwa upendo nilimvumilia sana. NILIMTAZAMA BABA YANGU. NIKAKUMBUKA ALIVYOKUWA AKIMFULIA MAMA YANGU NGUO ZAKE NA SARE ZA KAZINI. NILIJUA KWELI NDOA NI SAFARI NDEFU NA KILA MMOJA ANA VHA KUELEZA NA KIKASISIMUA. NANI ANGEJUA HAYA YOTE KWA NDOA ILE ILIYOKUWA IKISIFIKA VILE?Nilimwambia baba nitamsamehe mume wangu. Nitamsamehe. Baba aliniambia sio utamsamehe msamehe sasa hivi ndo utoke nje. Nilicheka kisha nikamwambia baba nitamsamehe.
 
SEHEMU YA TANO: FLORA ANAANGUKA DHAMBINI
PART 1



Baba aliondoka na kuniacha. Nilimaliza kazi zangu na kuanza kufunga ofisi. Nilipomaliza kufunga ofisi nilitoka nje ili kuelekea kituoni kuwahi staff bus ambalo hucbukua kwanza watu wa ofisi fulani headnoffice na kutufuata sisi wa branch office. Nilipotoka nje ilikuwa ni ajabu. Kumbe nilichelewa sana. Na sikuwahi basi. Nikiwa naangalia ustarabu mwingine mwanaume mmoja mweusi mrefu alinisalimia.Hujambo Flora?niligeuka kumtazama. Ni mwanaume nisiyemfahamu. Ila nilishangaa amenitambuaje?alisema tena wewe si mrs Deusi?niliitika ndio. Akaniambia pole umechelewa bus. Nilishukuru. Kisha aliniaga na kuniachia business card yake. Aliondoka na kwenda kupakia gari la kifahari sana. Gari jeusi. Na alipooanza kuondoka alinipungia mkono. Na aliondoka. Na mimi nilipunga pia. Nilifika ngumbani na wazo la kumsamehe mume. Alipofika mume nilikuta mtoto mgonjwa. Nilimuangalia mtoto na kumuandaa. Kisha nikamueleza mr kumpeleka mtoto hospital. Mr kama hakuona umuhimu. Aliniambia anapitia mahali hivyo dereva taxi anakuja kunipeleka. Nilimwambia Deusi ni wewe ama umelogwa?huoni mtoto mgonjwa wewebjamani?pepo gani hilo linakusumbua lakini wewe mwanaume? Hasira sijui ziliyoka wapi. Taxii aliyoita ilikuja na sikuipakia. Kisha nikaitisha taxii yangu na kuondoka. Tulipata matibabu na kurudi nyumbani. Kuwa na mawazo mengi kuninifanya nikasahau jambo muhimu sana kanisani. Nilisahau kikao cha mkutano mkuu wa uwt. Hivyo nilifuatwa asbh saa nne nikiwa nimekaa na mtoto na kuambiwa mwenyekiti unasubiriwa kikao kianze. Nilishtuka. Na kusahau kama kuna mkutano. Niliwaomba waahirishe mkutano ninauguliwa. Na hivyo tufanye kipindi kijacho. Ilikuwa ni mkutano wa wenyekiti wote wa uwt wa kanda. Na walikuwa wanatafuta mwenyekiti ama raisi wa uwt taifa. Na jina langu lilipendekezwa. Nilisahau jambo hilo. Hivyo mkutano huo mkubwa na wa heshima kwa kazi ya Mungu nikaupuuza kwa ajili ya UJINGA.

Aliyetumwa aliondoka. Na nilijiona niko sahihi. Baada ya lisaa limoja nilipigiwa simu na kuelezwa ofcn kuna mgeni. Anaomba kuzungumza na mimi. Niliuliza ni nani?secretary alisema hamjui. Kisha niliongea naye kwa simu ya mezani ya nyumbani. Alisema anaitwa Fransis . Mh.. sikuwa namfahamu. Alijitambulisha sana. Na mwisho akasema ngoja nikurahisishie. Mimi ni likuona jana. Nimepita kukusalimia tu. Sasa nilimkumbuka. Ni mwanaume niliyemuona jana. Aliniambia nilikuona kama huna furaha nikasema nikuache ila leo nimekuja kukujulia hali. Nilimueleza ninauguliwa ma mtoto hivyo sitakuwa kazini mpaka jumatatu. Alinipa pole sana na kuniambia angependa kujua mtoto anaendeleaje na kama sitajali naweza kumpigia kwa namba zake alizonipatia kwa simu. Mh… nilishangaa kwa upendo wake. Alikata simu na niliendelea na shughuli zangu. Jioni Mume alikuja kama kawaida kinuno kiliendelea kushika hatamu. Mwanaume gani asiyejali afya ya mtoto. Nilimchukia. Na kama kawaida aliondoka na kwenda tena bar. Kiliniuma sana. Nilijilaza kitandani na mwanangu. Nikiwa naugulia kupuuzwa. Na mara msichana aliniita na kuniambia kuna simu. Niliuliza kutoka wapi akasema mjomba kapiga. Niliamka na kufuata simu.

Nilifuata simu ambayo dada aliiweka pembeni na kuja kuniita. Nilifika na kuinua simu. Akili iliniambia ni kaka yangu kwani ndiye huwa tunamuita mjomba. Haloo?upande wa pili ukiita na sasa niliweza kujua ni sauti ambayo naweza kuikumbuka..
Haloo. Nani mwenzangu? Niliuliza japo sauti niliihisi.
Flora mtoto anaendeleaje? Alilitaja jina langu kwa ustadi wa hali ya juu. Nilimueleza mtoto hajambo anaendelwea vizuri.
Aliniambia nimepewa dawa gani ?
Nilishangaa anawezaje kujali hivyo. Milimueleza dawa nilizopewa na akaniambia ni vyema nikae na mtoto karibu na kumpatia maji mengi na matumda fresh especial machungwa.
Kipindi hicho kulikuwa na uhaba wa machungwa.
Nilimueleza machungwa upatikanaji wake ni mgumu sana. Kisha akaniambia…
Please flora.. be serious. Hata kama hayapatikani tutayatafuta. Mtoto ni bora sana. Tafadhali kesho nijulishe naweA kukupataje nikupatie machungwa. Tutayapata tu hakuna tatizo.
Nilimshukuru sana .
Asante Flora kuzumgymza na mimi nawatakia usiku mwema wewe na wanao. Mwambie anko i love her.
Kisha alikata simu.
Kwa dakika kadhaa niliendelea kuishikilia simu ile. Nilimtafakari sana na kumuona ni mwanaume wa ajabu. Mwenyevupendo na kujali sana. Alizumgumza kwa upole wa hali ya juu. Kwa huruma sana. Muda huo ilikuwa jioni sana. Nilifurahia na kujikuta napata faraja ya hali ya juu.

Tulikula na wanangu. Kisha tukaelekea kulala. Baada ya muda nilisikia mlio wa gari nankisha likazima. Sikulisikia tena. Niliamka na kuchungulia. Alikuwa ni mume wangu. Nilimtazama akiwa analumbana na mwanamke. Kisha nilizima taa za nje na kuziwasha tena. Bado waliendelea kulumbana. Nilisikiliza sana mazungumzo yao na ilikuwa ni kulumbana kwamba kwa nini ametoka kimapenzi na rafiki yake. Nilishangaa sana. Mume wangu anapiganiwa na wanawake? Kiliniuma. Nilitoka nje ili kuona kama naota ama ni ukweli . Nilikutana na mwanamke ninayemjua kwa Jina la mwenge. Mwanamke huyu ni moja ya wanawake makubuhu mtaani. Alikuwa akimshutumu Deusi kutoka na rafiki yake ili hali ni mpenzi wake. Kiliniuma sana. Nilipotoka mwanamke huyo aliondoka na mimi nikafungua gati mr aingie. Aliingia na nilifumga geti. Sikumsemesha maana ni mwepesi wa kupiga. Nilinyamaza na nikasema nitaongea naye asbh. Tulilala kwa kiburi. Nikiwa na hasira na akiwa kalewa. Niliumia sana. Mume hajali mimi wala mtoto mgonjwa. Kiliniuma sana. Nililala kwa hasira na kuota mambo mengi. Kisha nilishtuka saa nane na sikulala tena mpaka saa kumi na mbili asbh. Niliamka na kukaaa sebuleni. Ilikuwa ni majira ya saa tati asbh. Deusi aliniambia anaenda buchani anataka kupikiwa mtori. Nilimpuuza. Kisha akaondoka. Baada ya dakima kadhaa simu iliita na niliifuata. Alikuwa ni rafiki yangu amabye alionyesha kunijali. Aliniambia kwambaachungwa anayo. Nitayapataje?nilimwambia naweza kuyafuata aseme alipo. Aliniambia alipo na haraka nilivalia track suite yangu na kufunga khanga na kuondoka. Nilifika alipo. Niliona gari yake. Kwa woga niliangalia kushoto na kuliakisha nilamsogelea na kumsalimia. Asante sana. Nilimshukuru.
Hapana u deserve better service.. ur such a beautfull woman.. nashangaa Deusi anavyokutreet. Hajui thamani yako flora. Nilishtuka na kumuuliza unamfahamu?alisema ndio. Ninamfahamu. Naona siku hizi amakuwa kijana wa ajabu sana. Anatoka na kila mwanamke. Atakuua mamiii… take care of ur self….
Mh… nilipata hasira na uchungu. Kisha machozi yakanitoka.
Do not cry baby…. usilie Flora. Usilie. Nilizidi kulia na kuo a dunia inanicheka.
Kwa upendo aliniambia hembu ingia garini. Niliingia na aliondoa gari mahali pale kisha akawasha kiyoyozi na kunipatia maji akaniambia kunywa tuliza hasira. Aliendesha gari lake mpaka mahali kwenye ngumba kunwa sana ya kifahari. Na kumuamuru mlinzi afumgue gate. Kisha tukaingia humo. Aliniambia samahani kukuleta huku. Nilihisi pale sio mahali salama. Ila sikutaka pia uende nyumbani ukilia. So please dry ur tears then get fit and i will give you a ride. Alikuwa akizunguka zunguka kwenye mjengo huo. Nilikuwa nashangaa sana mjengo huo mzuri wenye unadhifu.

Zilipita dakika kadhaa kisha akaniambia naweza kukupeleka sasa. Niliogopa sana. Hofu ilinijia. Wazo la lwamba ananitaka kimapenzi nilikuwa nalo kutokana na muonekano wake. Alihisi naogopa.
Flora usiwe na wasi wasi. Unahitaji kuoendwa. Kubembelezwa na kujaliwa. Wewe ni mwanamke mrembo sana. Usiyestahili mateso. Nilikupenda sana siku ya kwanza nilipokuona. Moyo wangu ulilipuka mamii. Isipokuwa sikulazimishi. Na sihitaji jibu la mdomoni mwako. lets our heart talk. Unaweza kukataa ila moyo ukakubali. Unaweza kukubali ila moyo ukakataa. Mapenzi ni miyoyo na nafsi mamii. Usijilazimishe. Just relax baby…
Fransis aliongea kwa style ambayo tangu nizaliwe sijawahi kusikia maneno hayo na namna yanavyotamkwa. Moyo ulidunda mbio na sura kunibadika. Nilishindwa kuongea na kuanza kutetemeka na maneno kunitoka kwa kugugumia kama mwenye kugugumizi.
Fransis alinitazama tena kisha akasema… Flora ur the best woman ever…. a woman of my dream…
Kisha akanipakiza garini na kuondoka.
Nilihofu naweza kukutana na mr. Alinihakikishia usalama wangu. Aliniambia i will never do a mistake. Namjua Deus ni jeuri. Usijali. Nitakulinda. Nilifika nyumbani na mawazo tele. Upendo wa Fransis ulikuwa wa hali ya juu. Nilimhudumia mtoto na kisha nikajibwaga kitandani kusubiri mume arejee. Mume hakurejea. Japo aliondoka na pensi na tishirt kama mwanaume ajaye nyumba i mapema. Tulimsubiri sana bila mafanikio. Jioni iliingia. Kisha nikasema sitakuwa na fadhila kama sitamshukuru Fransis kwa upendo wake kunipatia machungwa.
Niliiendea simu na kumpigia.Ilikuwa simu ya nyumbani kwake. Hakupokea. Iliita sana. Kisha nikajisikia vibaya. Baadae kidogo nilipiga tena. Alipokea. Na aliposikia ni sauti yangu alionyesha mufurahia sana

Ooo… is that you inocent woman?
Yes.. nilijibu.
Kisha nilimwambia asante sana kwa machungwa. Nashukuru mno. Yamemfaa mtoto.
Fransis alisema do not mention… its a minor thing mamaa. U deserve the best.
Aligugumia kidogo kisha akaniambia mamii nikuache upumzike. Lala salama. Kesho nitakuwa ofisini kwa shughuli zangu nyeti nitakucheki endapo utakuwa free. Ama ukipata nafasi nipigie saa nane mchana. Bye . Aliniaga na nikaenda kukaa kwenye kochi nikimuwaza Fransis.
 
SEHEMU YA TANO: FLORA ANAANGUKA DHAMBINI
PART 2



Siku iliyofuata ilikuwa ni jumapili. Nilijiandaa kwenda kanisani. Nilikuwa mzito sana. Na mwenye hasira nyingi sana. Tuliongozana na mr. Njiani tulilumbana vibaya mno. Na kugombana haswa. Niliona ubaya wake haswaa kwa ukubwa mnoooo. Tuligombana na akasema haendi kanisani tayari ni nuksi. Na mimi nilimwambia hivyo hivyo. Kisha nikashuka garini na kurudi nyumbani. Aliondoka na hakutaka hata kukaa hata myumbani. Nilifika nyumbani na kujilaza kitandani nikilia sana. Sikutoka kabisa chumbani hadi niliposikia hodi saa tisa mchana. Walikuwa ni wanawake wa kanisani. Walikuja kunisalimia. Niliwakaribisha na tulaanza kuzungumza. Walinitia moyo na kuniambia yatapita ni mapito tu. Ma wakaniambia shauku yao ilivyo kuu na wanavyoniombea nipate mafasi ya uwenyekiti taifa. Mimi nilijaribu kuwaeleza ugumu wake na jinsi nilivyobanwa. Waliniambia kwamba nikishughulika ma mambo ya Mungu na Mungu atashughulika na mambo yangu.
Sikuwa tena habari ya maombi. Na wala sikuwa naona umuhumu tena wa kanisa. Makwazo ya deusi ndiyo yalitawala akili yangu kisha Fransis aliiyeka akili yangu haswaaaa.

Wakati tukiwa tunaendelea kuzungumza simu iliita. Alikuwa ni Fransis kwa uhakika. Nilipokea simu.
Haloo Flora..
Haloo Fransis habari?
Nzuri sana mamii. Nimesubiri sana simu yako nini mbaya?
Hapana nimepata ugeni tafadhali tuzungumze badae.
Please please Florah usiache kunipigia please. Sawa mamii..
Ndio nitafanya hivyo.
Okay mamii. Unanivutia sana na moyo wangu unateseka sasa. One thing…. please let our heart talk..
Bye mamii.
Alikata simu na niliduwaa kwa dakika moja. Kisha nikarudi kuzungumza na wanawake wale.

Waliendelea kunisihi nikubali kugombea. Ila nilikataa kata kata. Walishangaa jinsi nimebadilika. Tuliomba pamoja na waliondoka.
Ni kama nilikuwa natamani waondoke nizungumze na Fransis. Roho ya kuchukia kazi ya Mungu iliniingia kwa kasi ya ajabu.
Wakati nikiwa najiandaa kuongea na simu rafiki yangu aliingia kunisalimia. Ni mfanyakazi mwenzangu tuliyependana na kusaidiana sana. Alijua habari zangu. Alinihurumia sana. Na aliniambia flora wewe ni mrembo sioni kwa nini uumizwe. Aliniambia kwamba amekuwa kwenye shida ya ndoa ila kilichsaidia ni kupuuza matatizo na kusonga mbele. Alikuwa akiniamini kwa maombi sana. Na alikuwa akiniogopa. Hivyo hakuwa akinieleza upuizi wowote. Baada ya muda niliamua kumpigia simu fransis kwani niliona Beti haondoki.
Fransis aliniambia anasafiri nje ya nchi ndani ya simu tatu kufuata mzigo wake. Hivyo angetamani kuon5gea na mimi nfipo asafiri. Aliniambia angetamani kusafiri akiwa na jambo jipya maishani mwake. Nilisisimkwa mwili kwa namna alivyokuwa akiongea. Niliohopa sana kwa hofu. Kisha nilimueleza kwamba nitamjibu kesho nikifika ofcn. Tulikubaliana na kuagana. Beti alihisi jambo. Ila anijuavyo alisita kuniuliza na aliogopa kuhisi ndivyo sivyo. Tuliagana na Beti na nilienda kulala. Nilianza kusikia hali ya tofauti kidogo. Hasira zilipungua. Uchungu nao ulianza kuisha. Nilihitaji faraja. Na niliiona kwa Fransis.

nilifarijika sana kwa kuona kwamba kuna mtu ambaye anaweza kunisikiliza na kunihurumia, nilihesabu ni heshima sana, na kuanza kuwaza endapo sitatatufa muda wa kuonana naye basi nitakuwa sina shukrani, nilimfikiri sana fransis na kuanza kuwaza ni mwanaume wa wapi mbona sijawahi kumuona siku za nyuma ni nani huyu? ni msomi , ni mtanashati, ni mwanaume ambaye anaonekana anajua upendo na upole, je ana familia? niliwaza sana na kuanza kumuona mke wake ni mwanamke ambaye ana bahati sana . nilikumbuka aliniambia utanifahamu tu flora utanifahamuu… niliyakumbuka maneno yake haya na sasa shauku ya kmfahamu zaidi niliihitaji, niliamini yeye ananifahamu sana, sikutaka kuajua kanifahamuje lakini niliamini annifhamau kwani kwa namna ambavyo alikuwa akimuelezea deusi niliona ni mwanaume anayenifahamu fika. nilihama kwa fransis na kuhamia kwa deusi,, nilikumbuka alivhyokuwa akizozana na mwenge,, mwanamke ambaye hana thamani na aliyeishusha thamani yangu kwa mume wangu vilivyo, nilijiuliza kwa nini mume angu awe na mahusiano na mwanamke yule wa ajabu kiasi kile? niliona mume kanizalilisha vya kutosha, na kuniona sifai. mume alirejea na hakukuwa na maelewano mazuri kabisa, niliumia kumuona na alivyonizalilisha, nilimtazama aliavyovalia alivyochoka asivyojipenda,, nilimuhurumia kwa siku chache tu lakini alibadilika kabisa,, kisha nikamwambia siku hizi hata huendi salon? alinitazama na kuniambia ndio siendi nenda wewe kwani si una kichwa chako.. nilicheka kwa kejeli na hapo alirusha mkono wake kutaka kupiga na niliukwepa. aliendela kunisuka suka lakini nilimkwepa kisha akanifukuza ndani na kuniambia toka nje mshenzi wewe,, niikaa nje ya geti nikitafakari, niliumia sana,ilikuwa ni majira ya saa sita usiku,, nilikumbuka kitu..

akili yangu moja kwa moja iliniambia muda huo huo niende kwa rafiki yake ambaye ni majiran zetu, niligonga na kuwaeleza ugomvi wote, mume na mke wa hapo nilpofikia walinihurumia sana na kwanza waliniambia nipumzike kisha wakamfuata, wote walimfuata na kwenda kwa pamoja. waligonga mlango na kumsihi afungue,, kwa aibu alifungua na walimuelez kwamba niko kwao kwa vile amenifukuza, muda huo huo mke wa rafiki alikuja kunichukua na kurudi nyumbani,, sasa walitaka kutusuluhisha na kutuuliza kulikoni,, hapo ilikuwa ni muda mzuri wa kuzngumza,, mume alielezwa asema nini tatizo,, hakuna na chakusema zaidi ya kusema huyu mwanamke anajiskia sana na kujiona mzuri , ni hivyo tu alisema, na aliouliza je hakuheshimu? alisema heshima ni ya kinafiki anajifanyamama wa kanisani lakini ni mnafiki,, aliulizwa je anakunafikia wapi hakusema lolote,, majirani walimsihi aache tabia hiyo kwani anaweza kusabbisha ndoa kutetereka na kuvunjika, alisema hana pa kwenda atakaa hapa hapa nani amtake,,, nilipoulizwa nini tatizo nilieleza kwamba amekuwa mlevei na hakuwa anaakunywa hapo awali,, pia amekuwa na mahusiano ya mapenzi na mwenge,, niliposema mwenge kila mmoja alihamaki na mumejirani alimtazama deusi na kumwambia sasa unavuka mipaka kwa nini umekuwa mzembe hivyo mpaka unamzalilisha mkeo aliongea sana kumuonya na mume alisema amekbali kuonyeska na hatarudia tena na mambo yaishe, tulishikishwa mikono nikiamini walau sasa mambo yatakuwa mazuri kidogo .baada ya majiani hakuongea lolote, kwa muda wa siku hizo chache sikuweza kumuandalia chochote kwa ujeuri wake na kunifanya niwe na mawazo na hasira, niligundua hana viatu visafi, hana nguo nzuri za kazini, ilikuwa ni majira ya saa nane na robo usiku,,, nilijahidi kuamka mapame kumuandaaa. na haraka sana saa kumi na moja na nusu nilishaamka na nakumuandalia yeye kisha nikajiandaa mimi. nilimsalimia na kumueleza akaoge,,lakini hakunijibu badala yake aliniambia usifikiri nitakupeleka kazini na gari,, utaende na dala dala.. nilishangaa na nikaona anafikiri huduma yangu inahitaji malipo,, kumbe nilikuwa nafanya kama wajibu wangu.. niliondoka na yeye aliamka na kuondoka, alinipita nimesimama kituo cha dala dala nasuiri usafiri,, machozi ya uchungu yalindondoka,, kwani mbele kidogo alipakiza watu kuwapatia lift, nilijiuliza hao watu wananielewaje na walinipita kunisalimia,, nikiwa naendelea kulia yule mwanamke aliyenishauri jana yake akiwa na mumewe alipita na garni na kuniona na kusimamisha garni kisha kunipatia lift,, nilikuwa nalia sana na kwenye gari nilimsimulia kisa kizima,, alinihurumia na kuniambia acha kujitesa mama,, raha jipe mwenyewe unalia nini sasa? leo ndo umejua anatoka na mwenge? mbona ndio story mtaani unalia nini? wewe si unaomba omba mungu kisha akacheka na kuniambia atanitafuta tuongee zaidi kwani tulikuwa tumeshafika , nilishuka na aliondoka. na kukubaliana jioni tukutane tena ajekunifuata.
 
Back
Top Bottom