Ndoa za kikristo hazifati maandiko ya kwenye biblia, zinafata sheria za viongozi wa makanisa

Actually Hakuna andiko ndani ya Biblia linalokataza kuoa mke zaidi ya mmoja badala utakuna na Hili andiko

“Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia.”
— Kutoka 21:10 (Biblia Takatifu)



Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 

Mwili mmoja lakini sio akili moja wala roho moja!

Hata hivyo mambo ya ndoa yanaenda kufutika siku za usoni.

Si vijana wa kiume au wakike wataokubali kufungiwa kwenye mahusiano ya kudumu yasiyo na lazima wala tija.
 
Ndoa, kama ilivyo dini ni utamaduni ambao hautaweza kusimama dhidi ya pingamizi za nyakati.
 
Kwani walioa Wanawake zaidi ya mmoja hawana michepuko?
Ishu ni kwamba anaongeza mke kitakatifu ama mchepuko kihuni, mwengine ni lazima aongeze mchepuko hawezi kuongeza mke
 
Ndoa zipo za aina 2 km sijakosea

Km itakua nmekosea pahala naomba kusahihishwa kwa lugha rafiki sio lugha chafu

Ni km hivi kuna ndoa za namna hii

  • Ndoa za kidini aidha kikristu au kiislam
  • Ndoa za kimila au mitala

Sasa hapo ndoa za kidini

Tutaanza kwa wakristu au wakristo, unaruhusiwa kuoa mke mmoja tu na ni marufuku kuachana nae hadi unatenganishwa nae na kifo ingawa wapo watu wanajiondoa kwenye hii ndoa kilazima baada ya kushindwana kabisa

Tukija kwa waislam unaruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja yaan kuanzia mmoja hadi wanne ndio kikomo na pia unaruhusiwa kuacha na kuoa mwingine muda wowote unaotaka wewe, ni kuandika taraka na kuacha kesho unaenda kuchagua mwingine unamtafuna ukimchoka unamuacha

Mfano mzuri nna ndugu yangu, yeye ni muislamu ameshaoa na kuacha mara 15 mpaka sasa ana watoto 10 na kila mtoto ana mama yake

Ushaelewa?

Pia kuna ndoa za kimila, hizi ndoa hufungwa kwenye maboma au zinatambulika km Ndoa za bomani, sasa ndoa hizi za kimila ndio kufuru maana hakuna limit ya wake unaostahiri kuoa yaan wewe tu na ukwasi wako na kiborodinda chako km unaweza kuhudumia wanawake 10 chukua 10 waoe wazalishe wahudumie

Ushaelewa?

Kwa hio nahitimisha kwa kusema kwamba, mtoa mada ulitakiwa uhame aidha uhamie uislam au uhamie kwenye mitala yaan ndoa za kimila ili ukaishi unavyotaka wewe maana unaonekana wewe ni mzee tombatomba alimaarufu km kitombi unataka udunge dunge kila papuchi na hata ukipewa 10 kwa mkupuo hazitakutosha, uliza wanaofunga Ndoa za kimila yaan wamejitahidi sana wake watatu yaan hapo amejitahidi na huku sheria za kimila zinasema au zinamruhusu hakuna limit ya wake wa kuoa oa idadi yoyote unayoiweza wewe

Ushaelewa au nianze upya?
 
Kwanza maandiko mengi yanakandamiza wanawake. Halafu mjue Biblia kuna vitabu vingi tu havijaandikwa kwenye Biblia.
Km vitabu gan? Emu vitaje

Mimi najua wakatoriki wanatumia vitabu 73 ila waprotestant, wasabato, na wengineo wanatumia vitabu 66 tu sababu vitabu 7 wamevikataa hawavitumii
 
Nimekuuliza swali huko nyuma kuhusu kauli yako kwamba mwanaume kuoa wake wengi ni umalaya,

Nakuuliza upya tena, Kina Musa walikuwa malaya ??
Mkuu,hapa utashambuliwa sana,imani ya mtu katika dini fulani inaathiri sehemu ile ya ubongo inayoathiriwa na uraibu wa madawa ya kulevya..so una mlima wa kupanda ili watu wakuelewe.
Mimi nilishangaa sana kuja kusikia kwamba Italy ni nchi ya tatu kwa low rates za ufungaji ndoa.Waliotuletea haya mautaratibu,wao wenyewe yamewashinda huko!!
 
Uzi wako nimeupenda na nasema uko sahihi. Watu wakibisha wabishe tu maana ni haki yao. Maandiko yanasema siku za mwisho watu watawalazimisha wenzao wasioe!!
 
Unaonekana mgumu sana kuelewa, point ya mleta mada ni kwamba Suala la mke mmoja ni suala la kanisa wala si Mungu aliyetoa maagizo mwanaume kuoa mke mmoja, mleta mada akatoa mfano wa mtume Mussa alikuwa na mahusiano ya karibu na mungu lakini bado alikuwa na wake wengi.
 
Hata ibrahim alikuwa na wake wengi, hata Solomon aliyebarikiwa hekima alikuwa na wake wengi.

Viazi watakuja kusema "oooh hizo habari za agano la kale, tupo agano jipya sasa"

So Km agano la kale halina maana, habari zake ziondolewe kwenye mafundisho ya kanisa now.
 
Baada ya kuandika "maoni yako binafsi" hebu sasa jenga hoja zako kwa kunukuu maandiko kifungu kwa kifungu. Mwanamume mwenye mtazamo wa aina hii hatoshi kuwa mume wa ndoa. Acha kufuata mkumbo huku huelewi ni nini unachokitaka. Watu wenye mitazamo ya hovyo namna hii ndio mnaizika taasisi ya ndoa na kufanya ionekane ni ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia.

Nasikitika kukuarifu kwamba hujajua kweli bado, jibidiishe katika kumtafuta Mungu kwa kusoma neno lake nawe utaishi.

Amina
 
Mwanangu umeongea point, hamna agano jipya bila agano la kale
 
Tutajie wake wa Abrahamu sie viazi.
 
Changamoto yako ya ndoa haiwezi kubadilisha maandiko ya biblia wewe pambana na hali yako!
So kweli kuwa ndoa za Kikristo hazifuati maandiko ila tunapokutana na Changamoto kwenye ndoa huwa tunatafuta maandiko ili tujifariji tunapoyakosa ni lazima tulalamike kama mtoa madam anavyofanya.
 
Mkuu, uhusiano wako na Mungu ni personal i.e hauhitaji mtu mwingine akupe approval.

Wewe kama umesoma biblia na ukaona hakuna sehemu inakataza ndoa za wake wengi, fanya uoe.

Hata kwenye Uislamu kuna baadhi ya madhehebu yanatakaza ndoa za wake wengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…