Pre GE2025 Ndugai atoa hoja utaratibu kumwona daktari kwa Tsh. 10,000 ufutwe

Pre GE2025 Ndugai atoa hoja utaratibu kumwona daktari kwa Tsh. 10,000 ufutwe

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
SPIKA Mstaafu na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai ameishauri serikali kuangalia upya utaratibu uliopo sasa, katika hospitali nyingi za umma kuwa ni lazima mgonjwa kutoa Sh. 10,000 kwa ajili ya kumuona daktari.

Ndugai, alisema hayo juzi jijini hapa, wakati akichangia hoja kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa (RCC), kilichofanyika jijini Dodoma.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Alisema, hivi sasa upo utaratibu ambao unatumika katika hospitali nyingi za umma, kwa wagonjwa kulazimika kutoa kiasi cha Sh. 10,000 ili wamwone Daktari.

“Hivi huu utaratibu wa lazima mgonjwa atoe Sh. 10,000 kwa ajili ya kumwona daktari, nini mantiki yake yaani kumwona mkuu wa mkoa ni bure kumwona waziri ni bure kwanini kumwona dakatari ni Sh. 10,000,” alihoji Ndugai.

Aidha, alisema kama inawezekana utaratibu huo uangaliwe upya, ili kuona viwango hivyo vinapunguzwa kutoa nafuu kwa wagonjwa ambao wamekuwa na uhitaji wa kuwaona madaktari, kwa ajili ya matibabu mbalimbali.

“Mtu anaumwa lakini hawezi kumuona Daktari hadi awe na Sh.10,000, hebu kama inawezekana basi viwango hivi tuone namna ya kuvipunguza ili tutoe unafuu kwa wananchi wanaohitaji kuwaona madaktari,” alisema.

Kadhalika, alisema hivi sasa katika vituo vingi vya afya vilivyopo kwenye maeneo mbalimbali hususani vijiji ambako watu wengi wanatumia huduma ya kadi za bima ya afya ya jamii CHF, wanakosa huduma kutoka na serikali kutorudisha fedha katika vituo hivyo.

“Hivi sasa katika maeneo mengi ya vijijini kule ambako wanatumia sana kadi hizi za CHF, wanalalamika kukosa huduma kutokana na vituo kukosa fedha ambazo serikali ilipaswa kuzirudisha katika vituo hivyo,” alisema.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Thomas Rutachunzibwa, akitoa ufafanuzi wa hoja zilizotolewa na wajumbe wa kikao hicho, alisema kiasi hicho cha Sh. 10,000 kwa ajili ya kuwaona madaktari kinaenda katika mfuko mkuu wa serikali na siyo mfukoni mwa mtu.

“Fedha hizi zinakwenda kwenye mfuko wa mkuu wa serikali siyo mfukoni mwa daktari, lakini kama ulivyotoa ushauri wako mheshimiwa Ndugai, tutauzingatia kuona namna ya kupitia upya viwango hivi,” alisema Dk. Rutachunzibwa.

Kuhusu fedha zinazopaswa kurudishwa kwenye vituo vya afya kwa ajili ya kuhudumia watumiaji wa kadi za Bima ya Afya ya Jamii (CHF), alisema ipo changamoto kidogo ya kimfumo ambayo inafanyiwa kazi na muda siyo mrefu hali hiyo itakuwa sawa.
Hii ni Afya,Ili nchi isonge mbele lazima iwe na wananchi wake wenye Afya inayotokana na Akili timamu,kumuona Dr ni kuiyumbisha Afya pia, maana kama huna hiyo hela,hutaangaika kumuona Dr.
 
Serikali ndiyo inayochukua hiyo hela wanayoita ya kumuona daktari. Wengi huamini kwamba inaingia mfukoni mwa daktari lakini siyo.

Huyo huyo daktari anayedhaniwa kuchukua hiyo ada (hela ya kumuona daktari) hulazimika kulipia leseni ya udaktari kila mwaka TSH. 100,000/= ambayo nayo huenda serikalini.

Wakati huo huo hiyo leseni daktari hatumii kufanya biashara yoyote bali kutoa huduma (kutibu).
Nikukosoe kidogo mkuu ni laki3!
 
Halaf madaktari wakiona mgonjwa dalili zake haponi au ashakata roho wanakuagiza dawa za bei juuu ili baadae wakaziuze hawa watu hawaogopi kabisa
 
Hahaha! Unalipia leseni serikalini ili uruhusiwe kutibu watu wa serikali

Ndiyo, halafu mwisho ndiyo haya ya kuona kwamba anayechukua hela ya kumuona daktari ni daktari!
 
Halaf madaktari wakiona mgonjwa dalili zake haponi au ashakata roho wanakuagiza dawa za bei juuu ili baadae wakaziuze hawa watu hawaogopi kabisa
Duh, pole sana kama ulikutana na hayo!

Kama kweli wapo walioufanyia hivyo ni vyema ukawaripoti washughulikiwe.

Pia madaktari wameapa kukoa maisha ya mgonjwa kwa hiyo hata kama mgonjwa yupo mahututi hawatakiwi kuacha kumhudumia kwa kufanya kila wawezalo kuokoa maisha yake. Kwa hiyo hakuna daktari atakayemwagizia mgonjwa dawa za bei ghali kisa eti anakaribia kukata roho. Kama utagundua wanakufanyia hivyo basi mwishoni waambie wakurudishie dawa zako kama hazijatumika.
 
Kama Ndugai (mtu ambae amewahi kuwa Naibu Spika Kwa miaka 5, na Spika kwa miaka 5. Lakini pia ni mbunge wa muda mrefu).
Hajui hiyo pesa inayoitwa ya kumuona daktari huwa inakwenda wapi?
Na kazi yake ni nini?

Basi itoshe kusema tuna very long long safari.
 
Halaf madaktari wakiona mgonjwa dalili zake haponi au ashakata roho wanakuagiza dawa za bei juuu ili baadae wakaziuze hawa watu hawaogopi kabisa
Ungetumia neno baadhi, msg yako ingeleta uhalisia.
 
SPIKA Mstaafu na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai ameishauri serikali kuangalia upya utaratibu uliopo sasa, katika hospitali nyingi za umma kuwa ni lazima mgonjwa kutoa Sh. 10,000 kwa ajili ya kumuona daktari.

Ndugai, alisema hayo juzi jijini hapa, wakati akichangia hoja kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa (RCC), kilichofanyika jijini Dodoma.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Alisema, hivi sasa upo utaratibu ambao unatumika katika hospitali nyingi za umma, kwa wagonjwa kulazimika kutoa kiasi cha Sh. 10,000 ili wamwone Daktari.

“Hivi huu utaratibu wa lazima mgonjwa atoe Sh. 10,000 kwa ajili ya kumwona daktari, nini mantiki yake yaani kumwona mkuu wa mkoa ni bure kumwona waziri ni bure kwanini kumwona dakatari ni Sh. 10,000,” alihoji Ndugai.

Aidha, alisema kama inawezekana utaratibu huo uangaliwe upya, ili kuona viwango hivyo vinapunguzwa kutoa nafuu kwa wagonjwa ambao wamekuwa na uhitaji wa kuwaona madaktari, kwa ajili ya matibabu mbalimbali.

“Mtu anaumwa lakini hawezi kumuona Daktari hadi awe na Sh.10,000, hebu kama inawezekana basi viwango hivi tuone namna ya kuvipunguza ili tutoe unafuu kwa wananchi wanaohitaji kuwaona madaktari,” alisema.

Kadhalika, alisema hivi sasa katika vituo vingi vya afya vilivyopo kwenye maeneo mbalimbali hususani vijiji ambako watu wengi wanatumia huduma ya kadi za bima ya afya ya jamii CHF, wanakosa huduma kutoka na serikali kutorudisha fedha katika vituo hivyo.

“Hivi sasa katika maeneo mengi ya vijijini kule ambako wanatumia sana kadi hizi za CHF, wanalalamika kukosa huduma kutokana na vituo kukosa fedha ambazo serikali ilipaswa kuzirudisha katika vituo hivyo,” alisema.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Thomas Rutachunzibwa, akitoa ufafanuzi wa hoja zilizotolewa na wajumbe wa kikao hicho, alisema kiasi hicho cha Sh. 10,000 kwa ajili ya kuwaona madaktari kinaenda katika mfuko mkuu wa serikali na siyo mfukoni mwa mtu.

“Fedha hizi zinakwenda kwenye mfuko wa mkuu wa serikali siyo mfukoni mwa daktari, lakini kama ulivyotoa ushauri wako mheshimiwa Ndugai, tutauzingatia kuona namna ya kupitia upya viwango hivi,” alisema Dk. Rutachunzibwa.

Kuhusu fedha zinazopaswa kurudishwa kwenye vituo vya afya kwa ajili ya kuhudumia watumiaji wa kadi za Bima ya Afya ya Jamii (CHF), alisema ipo changamoto kidogo ya kimfumo ambayo inafanyiwa kazi na muda siyo mrefu hali hiyo itakuwa sawa.
Serikali itoe maelezo ya kueleweka hizi fedha ni za nini? Ushauri wa daktari ni muhimu sana na unapaswa kutolewa bure. Kitendo cha kutoza kumwuona daktari kunasababisha watu kununua dawa bila utaratibu na kuwasababishia madhara wagonjwa!
 
Duh, pole sana kama ulikutana na hayo!

Kama kweli wapo walioufanyia hivyo ni vyema ukawaripoti washughulikiwe.

Pia madaktari wameapa kukoa maisha ya mgonjwa kwa hiyo hata kama mgonjwa yupo mahututi hawatakiwi kuacha kumhudumia kwa kufanya kila wawezalo kuokoa maisha yake. Kwa hiyo hakuna daktari atakayemwagizia mgonjwa dawa za bei ghali kisa eti anakaribia kukata roho. Kama utagundua wanakufanyia hivyo basi mwishoni waambie wakurudishie dawa zako kama hazijatumika.
Mdogo wangu alikuwa ICU ashafariki siku tatu alikuwa kwenye coma tunaagizwa dawa za bei kweli ngoja nikae kimya
 
Mdogo wangu alikuwa ICU ashafariki siku tatu alikuwa kwenye coma tunaagizwa dawa za bei kweli ngoja nikae kimya

Pole sana!

Naamini nia yao haikuwa mbaya bali ni katika juhudi tu za kumuokoa.
 
Iwe 1,000/=


Cc: Mahondaw
Mkuu nafikiri hata ikiwa hiyo 1,000 bado watu watalalamika tu.

Hata hivyo hiyo hela ya kumuona daktari ni sehemu ya wananchi kuchangia uendeshaji wa huduma za afya.

Labda lile suala la bima kwa wote likikamilika.
 
Back
Top Bottom