Hata 40 haijaisha.Wanasiasa wengi wa nchi hii hawana aibu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata 40 haijaisha.Wanasiasa wengi wa nchi hii hawana aibu
Ndo hulka ya chawa ilivyo pindi blanket la zamani likitupwa.We ukuona yule shehe wa bashite haikupita hata wiki akamkana bashite alipochezea spana.Daah Job Ndugai kafunga kazi leo.
Meaning kila jambo alilokua anafanya na Magufuli hakuliafiki??
As a Christian lazima akatubu kanisani, hii ni dhambi ya wazi na itamtafuna.
Ndugai ajiuzulu tu , hii ni zaidi ya aibu.
Sahihi kabisa nadhani rais angewaambia tu wajiuzulu kwa manufaa ya uma, hatuwezi kuwa na kauli za aina hii kila uchwao sijui wanatoa mifano gani kwa vizazi vijavyo,Mama angepanga safu yake mpya na sio hawa jiwe toxin
Kuna mmoja anasema eti walizalisha ajira milioni 12 yaani anadhani bado ni zama za jiwe.Dereva mpya konda wa zamaniSahihi kabisa nadhani rais angewaambia tu wajiuzulu kwa manufaa ya uma, hatuwezi kuwa na kauli za aina hii kila uchwao sijui wanatoa mifano gani kwa vizazi vijavyo,
Ndugai, kigwangala, CAG and the rest is a bad example to the society.
Huyo Ni musibaNdugai tayar ashakua adui wa Veronica France
Ukijumlisha wabunge wote wa chadema tangu iundwe hakuna anaeweza kushauri mambo ya biashara kumzidi mbunge mmoja tu wa CCM mh kimei. Hapo bado sijakutajia wengine kama 100.Wakati ule wabunge wa upinzani wanatoa Maoni kuhusu hili shirika mliwaita mawakala wa mabeberu, sio wazalendo, wanatumika na meneno mengine kibao hadi wengine kupewa adhabu za ovyo ovyo.
Leo mmeingiza nchi hasara mnasema wabunge wachangie kwa uwazi, wabunge wenyewe wako wapi wa kuchangia kwa uwazi.?
Hawa akina Babu Taletale? Waliopelekwa bungeni kama watoto wanapelekwa chekechea..
CCM na Mwendazake mmeifirisi sana nchi hii na bado mnaendelea kuifirisi na kutuona Watanzania kama mazwazwa.
Halafu Spika bila aibu unashauri watu binafsi wanunue mabehewa halafu wawakodishie shirika la Reli si ndio....Yaani unataka uozo uliopo Tanesco uhamie na shirika la Reli sasa sio.?
Watu wamejipanga. Hata ndoto zetu umeme kushuka bei baada ya bwawa la Rufiji kukamilika zitayeyuka. Watajibinafsishia na kutukamua. Tuombe Mungu, yajayo yanatisha.Mheshimiwa spika, kitaalam kupata hasara siyo sababu ya kuacha biashara Bali ni sababu ya kuwa mwangalifu zaidi na kuangalia namna ya kuziba mapengo yaliyosababisha hasara.
Ni kama vile mimba kuharibika siyo sababu ya kuamua kutokuzaa kabisa. Ukikuta mtu mzima anajifanya hazijui changamoto hizi za kibiashara ujue huyo mtu ana lake jambo.
Niseme tu kuwa "we are watching"!!!
Waimba mapambio nao wameanza kumuimbia Kaswida MamaJamani, Sasa jpm anabaki na Nani? Maana mpaka ndugai anamkataa.dunia imejaa wanafiki
Ila Majaliwa kazidi sio kwa kujikunyata kule😁😁Kama kuna watu kila nikiwaangalia katika mikutano ya Rais Samia namuona hana furaha kabisa na anakaa kinyonge sana ni huyu bwana Ndugai. Sijui tatizo ni nini?
Ni ngumu kuifuta rekodi ya Magufulijingalao ,Bia yetu bila kumsahau TataMadiba siwasikii siku hizi wakiimba mapambio kama zama za mwendazake
Marehemu fufuka umuone best yako huku anakukana
Spika wa Bunge Job Ndugai amewaasa wabunge kuchangia kwa uwazi bila kuogopa mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022 na sio kusubiri serikali ifeli kisha walaumu.
Spika amesema kwa mfano Taarifa ya CAG imeonyesha ATCL imepata hasara ya bilioni 60 na kuuliza; je ni sahihi kuendelea kununua ndege nyingine?
Pia ameshauri sekta binafsi kuhusishwa kwenye uwekezaji wa miradi mikubwa kama kununua mabehewa ya treni za kisasa zitakazokuja na sio kila kitu kufanya Serikali huku akisema wabunge nao inabidi washiriki na sio kuwaachia wawekezaji wa kutoka nje pekee japo nayo ni vizuri.
Kuna siku Ndugai atauliza:
Kuna haja ya kuwa na akina Halima Mdee humu bungeni maana sijui wameingiaje?