Ndugu Gwajima, hii barabara isipotengezwa kiwango cha lami, kura katafute Mbweni!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,207
Reaction score
13,839
Hii barabara ina walalahoi wengi,
Hii baabara inaenda baraza la mitihani
Hii barabara inaweza kuunganisha Mbezi Ndumbwi na barabara ya Goba
Hii barabara ina hudumia shule kubwa ya St Mary's
Hii barabara tayari ilishajengwa madaraja mawili kuunganisha vitongoji vya kwa Maranda na dispensary ya Ndumbwi.
Hata barabara za Mbezi NSSF na zingine ni hadithi tu!

Lakini tunaona kasi ya barabara za lami Mbweni kwa wazito.

Gwajima, tukupe tahadhari tu, kule Mbweni waliko wazito hawafiki hata 15,000.
Sisi huku tuko nafikiri 150,000(Mbezi Beach, Mbezi Juu, Goba).
Na hili la wakazi tumeanza kulifanya kazi, 2025 siyo mbali.
 
Mbona umemkosea adabu? Huyo ni Askofu, mheshimiwa pia ni mNEC wa CCM. Tafadhali edit umpe heshima yake
Kuingia siasa alikosea njia, sasa wananchi tunataka kile alichoahidi.
Akishindwa tunampiga chini.
Hatutaki bla bla, tunataka hii barabara kiwango cha lami, nothing less!
 
Gwajima ajipange tena upya mwaka 2025 hata ndani ya wajumbe wa CCM yenyewe, kwa kuwa 2020 kura zake hazikutosha isipokuwa akabebwa na JPM. Achilia mbali upinzani atakaoupata kutoka CDM.
 

Kwani yuko hapo kwa ajili ya kura alizopata? Mtishie kwa jingine ila sio hilo la kura. Siku hizi mshindi anapangwa na uongozi wa CCM, kisha tume ya uchaguzi inapangiwa idadi ya kura za kumtangaza.
 
Huyu jamaa kwa maneno tu 😂🤣 2025 usishangae amepita kwa kishindo
 
Mbona umemkosea adabu? Huyo ni Askofu, mheshimiwa pia ni mNEC wa CCM. Tafadhali edit umpe heshima yake
Hamna askofu hapo, huyo ni tapeli kwenye koti la dini. Kwani ukiwa mNec wa ccm ndio nini? Ccm yenyewe kama chama ni genge la wahuni tu, sasa mnec ndio nini? Au kwakuwa mnategemea mbeleko ya vyombo vya dola mnaona ccm ni bonge la chama?
 
Hamna askofu hapo, huyo ni tapeli kwenye koti la dini. Kwani ukiwa mNec wa ccm ndio nini? Ccm yenyewe kama chama ni genge la wahuni tu, sasa mnec ndio nini? Au kwakuwa mnategemea mbeleko ya vyombo vya dola mnaona ccm ni bonge la chama?
Hakika
 
Hahaha . Hivi wale vijana alishawapeleka USA kweli kama alivyoahidi?
Zile boat za wavuvi alishanunua kweli pale kawe na ununio?
Hamna mbunge Hpo huyo ni TAPELI TU
Akiona sehemu kuna shida kama mecco anaenda kuhubiri injili na mazuzu yanajazana kusikiliza.
 
Kumtumikia Mungu na Fedha havijawahi kwenda sambamba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…