Ndugu Polepole, nitajie kituo Cha mabasi cha Wilaya au mkoa chenye Hoteli yenye hadhi Kama hoteli binafsi zinazohusu abiria wa safari ndefu

Kuna siku kwa mara ya kwanza natoka dar kwenda igunga tabora, aisee tulifika hotel kile kitu cha bei ya chini 5000 sasa tupo wa tatu, nikabaki kuwa mtazamaji tu
 
Haka katoa mada katakuwa hakajitambui! Juzi tu watu wamelia kwamba wanapigwa kwenye hizo hotel sasa sijui kanatakaje?
 
Unaijua Vieitee wewe?? 5 tena hadi bei ya Korie ifike laki kwa lita 5, nasema uongo ndugu zangu?
 
Mabasi yasimame stand.hili halina mjadala na ndio msimamo wa wengi.asietaka ahamie nchi
 
mahotelini msosi kwa bufee... watavibeba walete stendi wenye hela zao wale ila wakina sisi Wa Dona Mandondo tutakua tumesaidiwa sana.. na iwe hivyo.. sio kulazimishwa kula tusivyovilaga katika maisha yetu ya kila siku labda hadi siku kuu.
 
Watabaki wale wenyewe naunga mkono serikali kuboresha stendi na vyoo na huduma nyinginezo maana Zita boost uchumi wa wajasiriamali kuliko uhuni wa hzo hotel za maporini, halafu toilet nyingi za stendi huwa Safi maana unalipia
 
Inawezekana ni wewe ni mpishi kwenye hizo hotel za njian mfano dar Mbeya ile ya waarabu nyama mbichi kabisa bora tule stand tu
La sivyo toa ushaur achana na uzwazwa wa lawama
 
Tena napendekeza tuwe tunasimama zaidi ya nusu saa nzima jamani watu wapumzike kidogo mana ni safari ya km zaidi ya 1000 kama Sie Mza dar. Ila jamaa ni dakika kumi tu sijui wanawahi nini.
Bora tuchelewe ila tusiwe tumesafiri kwa presha.. Unanipangia pa kula huku Hela ni yangu mbona hukunipangia kuitafuta
 
Mbona unatupangia kama Hela unatusaidia kuitafuta ndugu. Ina mana tukiwa safarini ndo unatujali sana. Mbona abiria anaweza akapata shida kidogo ila hamsisikilizi.
Acha tubanane hivyo2 tundu chache mkuu usituogopeshe mbona who na wazungu wote wametuogopesha kwenye korona.
Magonjwa ya mlipuko kwani yakitokea wewe kuna kitu unagharimika ama nini.
Ikiwezekana muwe mnaandika ni wapi mtasissima kwa chakula kama safari yenu inavyoonyeshaga.
Kwa iyo wewe ni waziri Wa afya Wa abiria. Kweli Leo tunapendwa. Hivi chakula mnakiuzaga kama mmeakiagiza Brazil ama Argentina binafsi nanuaga matunda tu nakula tena stendi na Katanga na maji mpaka mwisho Wa safari. Nikiwa na familia chakula kinatengenezwa jiko ninalolijua mie LA nyumbani ila sio kisa niuziwe chakula 10k eti ndo Niko LA kuaminika.
Yaani nyie mie Nilikuwa nawapimia kama vile mko mgodini ama Sie ni watalii jamani.
Hata huko stendi zitakuwepo hotel za hadhi zote kila MTU mfuko wake unavyomruhusu na roho yake.
Nikijisikia kunywa soda kwa mura shop sh 500 sawa na wewe ukitaka ukanywe malaika sh 3500 wakati mie huku kwa mura Napata soda 7 ni uamuzi ni ako mana kila MTU ana namna anavyotafuta Hela yake.
 
Mtoa post atakuwa anakahotel kake Chipsi kipande kuku alikuwa anawapiga buku 8
 
Nliwahi pita hotel za korogwe pale nkawanunulia chips kuku mtoto. Kipaja na chips bei elfu nane. Nkajaribu kupiga mahesabu nkagundua kuku mmoja waliomnunua bei ya juu kbsa elfu kumi akiuzwa anatoa shio chini ya elfu 30.
 
Vyakula vinavyouzwa kwenye hizo hotel ni Gharama kubwa halafu haviendani na ubora wa bei ya chakula wanachouza there is no quality and quantity of the food. Soda ya elfu 1000 watakuuzia hata 3000 . Chips za 2000 watakuuzia elfu 7000 . Bei zipo juu mno kiasi kwamba hakuna uhakika
 
Wenye mahoteli wameongea nao. Kumbe tatizo ni madereva wanataka hela nyingi - wastani wa buku kwa kila siti cash, na msosi na vinywaji bure kwa staff wote. Sasa mwenye hoteli akishapigwa hiyo buku kwa kila kichwa lazima na yeye kwenye bei yake aongeze buku mbili kufidia. Ndo hapo chipsi mayai ya Tshs. 2,500/- inapogeukwa kuwa Tshs. 5,000/- (maana akisema Tshs. 4,500/- chenji zitasumbua).

 
Inawezekana wewe hufanya safari kwa ajili ya kula njiani, sisi wengine hufanya safari kwa ajili ya kufika tuendako, hata hivyo wapo abiria wengine hawapendi kula kwenye hizo hoteli za njiani. Unapounga mkono eti mabasi yasimame kwa muda mrefu ili kila mtu akatafute chakula anachokitaka! Hiyo safari ni ya lengo la kula tu njiani na si kufika kwa wakati waendako. Inaonekana wewe haujawahi kuziona hoteli husika, baadhi yake zimejengwa na wenye mabasi jambo ambalo ni jema kwani zimezingatia usafi wa huduma za vyoo ambazo hutolewa bure na sehemu za chakula. Wanaofanya usafi wa vyoo hulipwa kutokana na mauzo ya chakula, sasa unataka bei ya chakula ipunguzwe na vyoo viwe vya kulipia? Ujue si abiria wote wanaotumia vyoo wanakula kwenye hoteli hizo, wapo wasiopenda kula njiani. Hoteli hizo hupata wateja kati ya saa sita na tisa mchana muda ambao mabasi ya toka pande mbili hukutana, na baada ya hapo biashara hukata mpaka kesho tena. Wafanyakazi wa hoteli hizo ni wakudumu hivyo muda abiria hawapo wao mshahara wao unaingia!
Nashauri, kwa kuwa CCM inamapesa bwerere ijenge hoteli za bei nafuu kwa wanyonge ambazo zitasababisha hizi za sasa zijifunge zenyewe kwa kukosa walaji, hata sasa CCM fursa hiyo ichangamkieni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…