Ndugu yangu anafanya na kuongea mambo ambayo hayaeleweki

Huyo atakuwa mgonjwa wa akili na atakuwa anasumbuliwa na ugonjwa ambao kwa kitaalamu unaitwa "Schizophrenia ". Mpeleke hospitali kama Mirembe, Dodoma au Kigoma kuna kituo cha Brothers of Charity (wakatoliki) kiitwacho Kasaka mental health center. Atasaidiwa huko vizuri kuliko hospitali za kawaida. Pole.
 
Peleka hospital huyo ni michanganyiko ya vant na ganja
 
Kashalogwa huyo mkuu........wala usihangaike kumpeleka hospitalini


Maofisini Kuna Mambo ya ajabu
 
UPDATE;
nimempeleka mgonjwa wangu hospitali amegundulika na ugonjwa wa, Delirium tremens

Also called: DTS, alcohol withdrawal delirium.
Ana ALCOHOL DEPENDENCY SYNDROME.

Severe alcohol withdrawal symptoms such as shaking, confusion and hallucinations.

Delirium tremens usually starts two to five days after the last drink and it can be fatal.

Yupo level four.
Atapewa dawa za detoxication kwanza.

Amepimwa ini ,Full blood picture Na vipimo vya figo amechukuliwa.
Hali yake hadi sasa iko vile vile na anaendelea na dozi mpaka siku tano.
 
Amwone daktari wa magonjwa ya akili haraka sana (psychiatrist).
Ugonjwa unatibika vizuri tu.
 
Wanasema maumivu ya kichwa yanaanza polepole,kama ukiendelea kutegemea ushauri wa madaktari fake wa JF soon huyo ndugu yako atakuwa mwehu kamiki
 
Wanasema maumivu ya kichwa yanaanza polepole,kama ukiendelea kutegemea ushauri wa madaktari fake wa JF soon huyo ndugu yako atakuwa mwehu kamiki
Ushauri unaofatwa hapa ni first aid assistance. Hii ni sawa upate tatizo, unauliza watu wa karibu. Dunia ya sasa kwa utandawazi uliokua. Unaweza kupeleka mada na kupata mawazo mbalimbali. Kupitia hapa. Nimepata solution na nimeifanyia kazi mkuu. Nina miaka nane sasa jf. Nashauri watu. Ila hili limenikuta kwann na mimi nisiombe ushauri.
 
Nimeku pm mkuu
 
Kazia hapo hapo msiache kutumia dawa.

Kupona inachukua hata miezi 6 ni swala la kumfariji na kuwa naye karibu tu.

Asiache kunywa dawa pia kwa sasa mwekeni mbali na pombe...
 
Pole mkuu

ila tukisema Pombe haifai muwe waelewa usisubiri yakufike ndio uzinduke

ushauri tu huo
 
Mkiwa sebuleni mmekaa angalia sehemu ya ukuta, halatu mwambie hivi "hebu angalia huyo mtu anachungulia ni nani?," Ukiona amenyenyuka halafu akaenda kumuangalia huyo mtu ukutani, basi muwahishe hospitali akapate tiba ya akili.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…