Ndugu zangu, kwa mwenye kibarua chochote unikumbuke

Ndugu zangu, kwa mwenye kibarua chochote unikumbuke

Assalam Allaykum,

Mpka sasa sijala na sjajua siku inaisha vipi, sina pesa wala mpango wa kupata hata buku kwa siku ya leo ukizingatia nimedamka asubuhi kutafuta vibarua viwandani na kwingineko lakini hola nimezurura hadi nimeona ntakuja anguka njiani bure nimekimbilia geto kujilaza nisikilizie tumbo linavyounguruma taratibu ndo nimekumbuka ningekuwa jela muda huu nna uhakika ningekuwa nimeshatia chochote mdomoni.

Daaah maisha haya. Nisimalize maneno ndugu zanguni kwa mwenye kibarua chochote unikumbuke. mawasiliano 0711406248

NB: Kuhusu bando natumia tunnel vpn
Una smartphone ww bado una hela
 
Ndugu zangu natumaini wale wa kwenye mihangaiko mliokuwa bize nyakati za mchana mmerejea nawakaribisha kutoa mawaza yenu pia mwenye connection na fursa yoyote anijuze. Natanguliza shukran zangu kwenu familia
 
Me; Habari mkuu nilikua nashida ya kazi hivo nimeona nikutafute maana uliacha namba pale jf

Yeye; Salama ndio kweli kuna kazi lakini wewe upo wapi kwa sasa maana hii kazi ni kwa watu wa dar

Me; Mkuu mimi nipo hapa tabata na nina uhitaji kweli wa kazi maana maisha magumu

Yeye; Hapana kaka usiseme maisha magumu ila ni vile ujapata tu sehemu sa hihi kama hapa..

Sasa sikia naomba kesho sa mbili uje hapa majumba sita si unaweza kusoma na kuandika

Me; ndio mkuu sio kusoma na kuandika tu pia nina vyeti vya form 6 maana nilisoma PCB na.....

Yeye; oky kesho uje haina shida........

Tuendeleee na kesho sasa....

Kuna watu humu watachomwa moto wa kijani
 
Sasa mkuu siuko na smart phone na internet ya VPN hebu Fanya kukopa kwenye hii mitandao mara pesa x,pesa fasta,etc kampuni ziko nyingi sana huko hukosi 300,000 halafu kesho amkia karume asubuhi na mapema wakiwa wanafungua mizigo ya mtumba pick za kutosha rudi getto Ka tulie ikifika jioni mida ya watu kutoka mahangaikoni jisogeze sehemu ya stendi penye movement ya watu weka mzigo hata kwa kutandaza kwenye mtaro ikiwezekana uwe na taa zile za kucharge mkuu utakuja kunishukuru mbele ya safari Nguo uliyoipick kwa 5,000 unauza Mpaka 10,000 kulaza 50K kama faida nikugusa achana na wazo LA kutafuta Kazi utaenda kutumikishwa tu huko na kugombana na watu
 
Sasa mkuu siuko na smart phone na internet ya VPN hebu Fanya kukopa kwenye hii mitandao mara pesa x,pesa fasta,etc kampuni ziko nyingi sana huko hukosi 300,000 halafu kesho amkia karume asubuhi na mapema wakiwa wanafungua mizigo ya mtumba pick za kutosha rudi getto Ka tulie ikifika jioni mida ya watu kutoka mahangaikoni jisogeze sehemu ya stendi penye movement ya watu weka mzigo hata kwa kutandaza kwenye mtaro ikiwezekana uwe na taa zile za kucharge mkuu utakuja kunishukuru mbele ya safari Nguo uliyoipick kwa 5,000 unauza Mpaka 10,000 kulaza 50K kama faida nikugusa achana na wazo LA kutafuta Kazi utaenda kutumikishwa tu huko na kugombana na watu
Tuwe tunatoa ushauri ambao ni realistic,
 
Kesho asubhi na mapema
Namba ngeni

Yeye : halloh vipi kaka mi ni frank yule jamaa wa jana.. ushaamka

Me; nimeamka mkuu habari yako.

Yeye; salama vipi mkuu mda huu ushaanza kuja nikuelekeze

Me; hapana mkuu ila sio mda nakuja

Yeye: sawa ukifika hapa majumba sita nistue nakusubiri..

Badaaaeee

Me ; kaka kaka nishafika

Yeye:; njoo mpaka huku mwisho wa mwendokasi

Me; sawa kaka nakuja.

Kidogo nakutana na kijana smart kachomekea na kunipokea kwa bashasha la tabasamu..

Yeye; karibu kaka karibu sana

Me; aaaah ahsante ndgu yangu nishakaribia aiseee...

Tunaanza kutembea .. naona nakutana na watu wengi alafu wana kama vipeperushi.. hapo kitaa chekundu kilicheza kichwani nikaona kabisa hapa leo nitatukana mtu.

Kufika sasa...

Mama mmoja; frank nilikuambiaje kuja na mgeni mda kama huu mbona kachelewa hivi aujui mwisho saa tano

Yeye: hapana bahati mbaya ila kashafika

Mmama; haya anza kumuelekeza akitoka hapo aje huku

Yeye: sawa

Darasa likaanza kachukua peni na kuanza kunipa darasa....

Ahahahaha mimi kimoyo moyo nasema "" hawa *** kweli an yale yale niliyokutana nayo mbezi ngoja tuone"""

Akaanza kutoa darasa kidogo

Yeye;; aaaah karibu sana Fundi manyumba hapa kiufupi tunajihusisha na tiba hasili/tiba lishe..

Wewe hutouza dawa ila wewe kazi yako itakua ni kupeleka hivi vipeperushi kwa watu ili watumie dawa zetu.

Mshahara upo hivi ukiwa daraja la kwanza utapata ....
Ukiwa daraja la pili utapata.....
Ukiwa daraja la tatu utapata...
Uki..... Daraja la 10 unapata nyumba na gari.

Ila pia ukiwa na team yako ya watu 6 na wao wakaleta sita wewe unakua una daraja la....

Kamisheni inapanda mpaka daraja la.....

* Jamaaa. Akaanza kuandika na formula za * pale *** yuleeee mi namchora tuu ....

Mwisho akasema kujiunga ni elfu 72 ila hata kama nina 30 naweza toa nyingine wataongezea wao

Ila all in all jamani tutafute pesa aiseeee yaani watu wanapendeza ila kichwani ni utapeli tuuu facvken sana
 
Assalam Allaykum,

Mpka sasa sijala na sjajua siku inaisha vipi, sina pesa wala mpango wa kupata hata buku kwa siku ya leo ukizingatia nimedamka asubuhi kutafuta vibarua viwandani na kwingineko lakini hola nimezurura hadi nimeona ntakuja anguka njiani bure nimekimbilia geto kujilaza nisikilizie tumbo linavyounguruma taratibu ndo nimekumbuka ningekuwa jela muda huu nna uhakika ningekuwa nimeshatia chochote mdomoni.

Daaah maisha haya. Nisimalize maneno ndugu zanguni kwa mwenye kibarua chochote unikumbuke. mawasiliano 0711406248

NB: Kuhusu bando natumia tunnel vpn
Jifunze ujuzi ambao unafundishika kwa muda mfupi mfano kinyozi halafu angalia ndugu zako mwenye hali nzuri muombe akusaidie, ajira ni ngumu sana kama hauna connection au sio kipaji maalumu kwenye field yako.
 
Sasa mkuu siuko na smart phone na internet ya VPN hebu Fanya kukopa kwenye hii mitandao mara pesa x,pesa fasta,etc kampuni ziko nyingi sana huko hukosi 300,000 halafu kesho amkia karume asubuhi na mapema wakiwa wanafungua mizigo ya mtumba pick za kutosha rudi getto Ka tulie ikifika jioni mida ya watu kutoka mahangaikoni jisogeze sehemu ya stendi penye movement ya watu weka mzigo hata kwa kutandaza kwenye mtaro ikiwezekana uwe na taa zile za kucharge mkuu utakuja kunishukuru mbele ya safari Nguo uliyoipick kwa 5,000 unauza Mpaka 10,000 kulaza 50K kama faida nikugusa achana na wazo LA kutafuta Kazi utaenda kutumikishwa tu huko na kugombana na watu
pesa X ndo wakupe laki3
 
Jifunze ujuzi ambao unafundishika kwa muda mfupi mfano kinyozi halafu angalia ndugu zako mwenye hali nzuri muombe akusaidie, ajira ni ngumu sana kama hauna connection au sio kipaji maalumu kwenye field yako.
Shukran
 
Pesa x mkopo
Finloan app
Branch
Okoa maisha
M safi loan
Fair loan
Nikopeshe
Twiga loan
Okoa maisha
Eagle cash
Kopa fasta

mkuu kote huko ukiokoteza okoteza hukosi hela uoga wako ndio umaskini wako
 
Kuna wakati fulani nilijifunza ili mwanaume uishi maisha mazuri kuna mambo mawili baba yake aliteseka sana kujenga kesho yake na yako au wewe mwenyewe uteseke sana tena sana,nasema hivi kuna kipindi nilikula msoto mpaka nikajisemea kwanini nilikuja duniani na baada ya miaka kadhaa ule msoto uliisha kwa sasa si haba lundo la maokoto halikauki kwenye kibubu.
 
Sasa Nabii atakufaje?? Au kapaa mbinguni!!? Ha ha ha ha hatareee!!
 
Omba Dua Kisha Usichoke Yatatimia, Weka yako Nia Mungu wako anakusikia RIZIKI MAFUNGU SABA
 
Back
Top Bottom