Ndugu zangu, nipeni neno la faraja

Ndugu zangu, nipeni neno la faraja

Oooh baby! Maisha ndio haya haya usijekubali lolote likuletee stress. Songa mbele bibie pia usipende kukaa peke yako muda mwingi tembelea marafiki nenda michezoni nenda club kula ushibe kunywa maji mengi moyo ueleeee sawa mamaa. Pls usijipe stress kama umeachwa tulia kwanza soma upepo maana ukiingia kwenye relation mapema utateseka bado mwisho wa siku utatumika kama mpira.
 
Pole sana dada yangu.. Matatizo ni sehemu ya maisha ya kila binadamu hapa duniani, usije ukajiona kama vile wewe pekee wapitia hayo, hapana.

Usiziendekeze stress yapokee matatizo yako, kubaliana nayo tu then tafuta namna ya kuyatatua. Ongea na watu unaowaamini, kaa na watu wanaokupa faraja usiwe mtu wa kukaa pekeako mda mwingi.

I pray for you [emoji120]
Amen mpendwa
 
Ndugu zangu, nimekuwa kwenye stress za muda mrefu kiasi cha kupata panick attacks mara kwa. Nimekuwa mtu wa kunywa antidepressants sasa. Naombeni mnipe neno la faraja angalau nione kuwa dunia bado ina watu wema.
Kuna siku nilikua nafikiria na huwa nawaambia rafiki zangu kwamba hizi changamoto nazopitia ,nitakuja niandike kitabu vijana waje labda kujifunza kwamba life c simple as they think....

ofcourse sometimes mambo Fulani huwa yanaumiza kwenye maisha sababu Sisi sote ni binadamu tuna roho ya kuumia pia....LAKINI nilikuja kufikiria kwamba hata nikikaa na stress na kuwaza snaa hakuna kinachobadilika na nabaki kama nilivyo na changamoto zote.

maamuzi yangu ni kutokaa kabisaa nafikiria vitu vinavyonifanya niwe na stress sababu nimeamua kuchukulia ni sehemu ya maisha na wacha niishi nazo kikubwa uhai upo ....

saivi naishi Kwa Amani Tu japo haimaanishi sina changamoto zinazoeza kunipelekea kupata stress ....nimeamua kuishi na changamoto zozote sababu hatuwezi kufanana NEVER....

Usiviwaze vitu vinavyokupa stress ...maana hata ukifanya hivyo pengine haviondoki wala haviwi solved na vinazid kukuumiza BALI jifunze kuishi navyo tu maana u need to survive na kuendelea na maisha kama kawaida.

pole Sana ila usijipe muda wa kuyawaza ivoo hayo machangamoto bali ishi nayo Tu na unayoweza kuyaeka Sawa fresh ...kama huwezi ishi nayo.... Kama ni mpenzi wa mpira kachek, movies cheki , kama kifurushi kimeisha nunua uchek sinema huko, tembelea marafiki zako mpige pige stories hata za enzi mpo shule......

kumbuka kuna watu tunakutana nao njiani au maofisini au popote pale wengine Wana matatizo kuliko yetu or yako ....lakini Wana nyuso za tofauti na kilichomo mioyoni mwao why? ni kwa sababu wanajua maisha lazima yaendelee hivyo wamejifunza kuishi na hayo matatizo or changamoto na maisha yanaendelea mbadala wa kujifungia ndani na kuwaza, kunywa mpk dawa nk...

hakuna changamoto isio na mwisho ....piga moyo konde ,endelea na life ,mambo yatakua Sawa Tu usihofu.
 
There is nothing in this world that can trouble you as much as your own thoughts!!

Pole sana ; imewahi kunitokea miaka mi3 iliyopita kwakweli kidogo niandike wosia, ilinitokea baada ya kuwa depressed,ikanifanya nikapata anxiety disorder nilipigana vita vikuu mno niliwahi kuona maisha hayana maana maana ila Mungu ni mwema nilishinda japo ni ngumu sana kujishinda ila naamini utakua sawa itabaki story, vipindi kama hivyo vipo kwenye maisha na vinatupitia wengi sana!! tambua hauko peke yako mkuu
 
Antidepressants zinaongeza mawazo ya kujiuwa na wala hazipunguzi na kuondoa depression
Achana kabisa na madawa Bali ikatae hiyo hali na hata badili sehemu uliopo na kwenda sehemu tofauti kabisa na kupata maisha mapya

Kama huwezi na unaishi mbali na wazazi nenda kwao kwa muda ukapumzike
 
kwanza fanya kuanza kuondoa sumu ya unachokula , anza kula vyakula vyenye kukupa afya bora kuanzia asubuhi mpka jioni anza tartbu mpaka uzoee, asubuhi kula mboga mboga, maziwa, na kiazi/gimbi/ndizi/ usiweke vyakula vya mafuta mengi au wanga uliokobolewa, mchana unaweza kupata mlo wako kwa kiasi kama unakula sanaa punguza kiasi cha chakula usisahau matunda na mbogamboga kwenye mlo wako ila mlo usiwe mwingi sana, hapa kwa mchana unawez kula ugali/wali/ndizi kwa kiasi kdgo , jioni hakikisha huli chakula chochote zaidi ya mchanganyiko wa matunda na maziwa ukiweza na mboga mboga kula, kwa mwanzo anza kula matunda ushibe maana tumbo linakuwa halijazoea kula hata sahani mbili, usisahau kunywa maji asubuhi mchana nA jioni kadri uwezavyo, kumbuka maziwa fresh kwa usiku ni kama ant depression maana yanakupa feeling ya utotoni na unapata mood ya kulala kirahisi bila mawazo yoyote, kitu cha pili ni kuondoa sumu ya kwenye akili cha kwanza kabisa ukiamka asubuhi anza kwa kumuomba Mungu na kutamka kwamba wewe ni mbarikiwa, umezaliwa ni mshindi na unashinda zaidi ya kushinda, Mungu anaishi ndani yako, kila kitu kwako kinawezekana, mpe Mungu nafasi ndani ya moyo wako, amini kuna jambo Mungu yupo tayari kukutendea leo kwenye afya, mahusiano, kazi, huduma, wabariki wengine, wafurahie wengine na anza kuona Mungu yupo upande wko ndo maana amekuokoa na kila jambo na upo hapo sio kwa bahati mbaya, jione wewe ni mtu mwenye kibali na kimstart.... kama una mziki kwako fungulia sauti isiyoweza kuwasumbua majirani anza kucheza tafuta ma amapiano ucheze, singeli kata mauno kama hujui jifunzee, cheza mziki wowote unaokuchangamsha kwa mda wa dakika 30 nk mpka uone hapa mwili mzima unatoka jasho, ukitoka hapo kujiandae uende misele kama huna kazi fanya kazi za nyumbani huku ukiendelea na imani yako Mungu ameanza kubadilisha maisha yako na chochote kinachotokea ni mpango wa Mungu kwako na anakuanda kwa jambo kubwa zaidi, pia achana na marfki ndugu wanaokufanya kujiona hufai, mnyonge, ukose amani, watoe kwenye akili na moyo wako, weka nguvu kwenye kuboresha maisha yako, hakikisha unaishi kwa amani bila wao, usifanye mtu kuwa ngao ya maish yakooo, jishughulishe na maisha yKo acha mbwembwe jifurahie, jisherekeeee jua wewe ni wa thamani sana...ukirudi jioni usisahau kucheza mziki tena, kama unaweza kukimbia kimbia ila zoezi la mziki ni zuri kwa afya ya akili, kama unaona una nguvu mda hauna kitu cha kufanya jifunze vitu online kama ni msomi jikumbushe masomo yako ya chuo uendelee kuwa bora kwenye fani yakoo.....

kwa mtiririko huo wa maisha naona kabisa ukibadilika na ukirejea kwenye tumaini kuuu.
 
Back
Top Bottom