Hata sasa hivi sheria hakuna popote inaposema kukosea kujaza fomu ni kigezo cha kumuengua mgombea.Kwenye mabadiliko ya katiba yanayohitajika ni pamoja na kuweka bayana muundo na utendaji wa hii tume. Katiba itamke wazi kuwa moja ya kazi za tume iwe ni kusaidia wagombea kwenye ujazaji fomu, na kwamba kukosea kujaza kamwe halitakuwa kosa la mtu kukosa sifa. Pia fomu zijazwe na kutumwa kimtandao ili kuwatia adabu wanaofunga ofisi na wale wanao temper na hizo fomu.
Jambo la msingi kuliko yote ni kwenda kuwatimua kwenye ofisi yetu ya umma.
Ofisi zetu hazitakiwa kutiwa najisi na washenzi wanaojiita tume ya uchaguzi.
Haikubaliki.
Taratibu zipi za kisheria wakati Sisi siyo wateuzi wao ?Tanzania ni yetu sote, na watanzania wote ni ndugu.
Hakuna haja ya kufanya fujo kuwaondoa, taratibu za kisheria zitumike.
Wapinzani kweli wanajeruhiwa. Wanarudishwa wale ambao ni dhaifu kupita. Kweli tume inatumika kuwanyima haki wapiga kura!