NEC: Jina la Tundu Lissu liko mwisho wa karatasi ya kupiga kura kwasababu alirejesha fomu akiwa wa mwisho

NEC: Jina la Tundu Lissu liko mwisho wa karatasi ya kupiga kura kwasababu alirejesha fomu akiwa wa mwisho

Ila Lisu ni genius aisee yeye ata haongerei sjui jina lake lipo wapi amewaachia NEC ndo waelezee.

Yeye anawabana NEC tu ndo wanaelezea
 
Wqambie kuna option za kusort data kwa excel, washamba hao wazee
 
Hivi wagombea wote(15) wa kiti cha Urais waliweza kupata wadhamini na kukidhi vigezo vyote kiurahisi kasoro Mh Lissu pekee? Hii nchi chini ya ccm ni tatizo sana

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Mpaka kumpokea Lissu kuingia na kuzipokea fomu kulikuwa na mjadala mrefu na giza lilipoingia wakampokea, lakini wakatengenezs kigezo kingine kipya duniani kigezo cha kuliondoa Nina la mgombea kwenye orodha endapo atafanya kosa, sasa utaliondoaje ndipo ikabuniwa njia hii, tulishuhudia akiadhibiwa kama mwanafunzi wa shule ya msingi.
 
Apo pako poa kabisa maana angekuwa wa pili ingekuwa ngumu kutambua kura ya jiwe na ya kwake apo Tina wapa hongera ole wenu muibe kura
 
Ni sababu ya kipumbavu kabisa.
Huyo afisa wa tume aliyetoa hiyo sababu apelekwe hospitali akapimwe akili.

Sote tunajua wagombea walipaswa kurejesha fomu siku moja, na utaratibu wa nani aanze na nani afuate uliwekwa na tume yenyewe, hivyo kama kusudio lilikuwa ni kuwahi kurejesha fomu ili uwekwe kwenye fomu wa kwanza basi wagombea na wapambe wao wangepigana vikumbo kugombea hiyo nafasi ya kwanza, ama mzee wa ubwabwa (Hashimu Rungwe) huenda angewahi kufika ofisi ya tume saa 11 alfajiri.

Miaka yote tunajua, tume imekuwa ikitumia mfuatano wa Alphabet, ambao ulikuwa na sense of logic, otherwise basi tume ingeweza hata kutumia mfumo wa bahati nasibu yenye kutoa nafasi kwa yoyote kupewa position yoyote katika karatasi ya kupigiwa kura.
 
Akihojiwa na kituo cha redio Kagera Community Radio(KCR FM) leo asubuhi Ofisa elimu kwa umma kutoka Tume ya uchaguzi (NEC Bw Titus Mwanzalila amesema kigezo kilichotumika ni urejeshwaji wa fomu za wagombea Urais ambapo mgombea wa Urais kupitia CCM John Magufuli alirejesha fomu akiwa wa kwanza na Tundu Lissu alirejesha akiwa wa mwisho.

Ameongeza kuwa kwa ngazi za ubunge na udiwani wagombea walipangwa katika karatasi za kura kwa maelekezo ya Tume

Hata hivyo amesema hiyo si sababu ya mpiga kura kutompigia kura mgombea anayemtaka.

Katika hatua nyingine amesema tume imejipanga kikamilifu kuondoa changamoto katika mchakato huu wa uchaguzi.

Nikipata nafasi nitawawekea audio clip
mbarikiwe

Byabato
Bukoba.
Sababu ya kijinga kabisa. Karne ya leo unatoa upupu huu? Kwanza si kweli eti aliwasilisha fomu akiwa wa mwisho. Rekodi zinaonyesha Lissu alifika Tume majira ya saa 4 Asubuhi. Utopolo wa Tume wa kushindwa kutafsiri sheria za Uchaguzi na maelekezo yao wenyewe ndiyo yaliyofanya awe wa mwisho. Huwezi kumwadhibu yeyote kwa ujinga wako mwenyewe. Pili, karne hii, hata mfumo wa kompyuta unafahamu utaratibu wa alphabet kutoka A-Z. Kwanini utaratibu huu haukutumika? Unapoongoza chombo nyeti na wakati nyeti ni vema ukawa na akili za ziada kubuni maswali ya ziada yatakayotosheleza bongo zenye upeo wa ziada. La sivyo, wewe ni poyoyo tu na nafasi uliyopewa ni hisani kwa hasara yako.
 
Ni unabii unatimia, wa kwanza atakuwa wa mwisho na wa mwisho atakuwa wa mwisho. Angewekwa katika isingekuwa na maana ya kinabii, kila Jambo lipo calculated japo waliopanga awakufikiria wanatimiza unabii.
Pili imesaidia wapiga kura wengi tayar wanajua ni namba ngapi
 
Tena wamerahisisha sana kazi wakati wa kuchinja bila kutafuta naenda 1 kwa 1 mwishoni
 
Ni unabii unatimia, wa kwanza atakuwa wa mwisho na wa mwisho atakuwa wa mwisho. Angewekwa katika isingekuwa na maana ya kinabii, kila Jambo lipo calculated japo waliopanga awakufikiria wanatimiza unabii.
Pili imesaidia wapiga kura wengi tayar wanajua ni namba ngapi
Mbeba maono Lissu ana ujumbe mzito. Kila dhuluma anayotendewa inabadilika kuwa neema yenye baraka na maelezo kwenye vitabu vitakatifu. NEC/WATAWALA hawajalitambua hili. Biblia inasema kuwa Mungu alimfanya Farao (utawala wa dhuluma wa Misri) awe na moyo mgumu ili ukuu wake (Mungu)udhihirike. Ndivyo Farao alivyofanya. Akawazuia Waisraeli wasiende Kanaani nchi ya asali na maziwa (Haki , Uhuru, na Maendeleo ya watu). Mungu akawaua wazaliwa wote wa kwanza wa Wamisri awe binadamu au mnyama. NEC/WATAWALA hawalijui andiko hili bado mpaka pale watakapoona vifo vya wazaliwa wao wa kwanza.
 
Utawala huu dhalimu umemkufuru Sana Mungu nae ameuondolea kibali machoni pa Mbingu na wanadamu. Nao unakwenda futika
 
Huyu jamaa hajielewi kabisa...Eti nae ametokea kwenye ualimu wa sekondari kabla ya kulamba teuzi..Tanzania kama Taifa tuna safari ndefu sana kwenye maendeleo aseee
 
Ni jambo jema!

Katika ulimwengu wa roho nafasi za mwisho mwisho siyo za kupuuza!

Yohana Mbatizaji naona siku hizi akili ziinaanza kukurejea.
Umenza kuona ukombozi wa kweli wa taifa letu si CCM bali ni Lissu mbeba maono
 
Akihojiwa na kituo cha redio Kagera Community Radio(KCR FM) leo asubuhi Ofisa elimu kwa umma kutoka Tume ya uchaguzi (NEC Bw Titus Mwanzalila amesema kigezo kilichotumika ni urejeshwaji wa fomu za wagombea Urais ambapo mgombea wa Urais kupitia CCM John Magufuli alirejesha fomu akiwa wa kwanza na Tundu Lissu alirejesha akiwa wa mwisho.

Ameongeza kuwa kwa ngazi za ubunge na udiwani wagombea walipangwa katika karatasi za kura kwa maelekezo ya Tume

Hata hivyo amesema hiyo si sababu ya mpiga kura kutompigia kura mgombea anayemtaka.

Katika hatua nyingine amesema tume imejipanga kikamilifu kuondoa changamoto katika mchakato huu wa uchaguzi.

Nikipata nafasi nitawawekea audio clip
mbarikiwe

Byabato
Bukoba.
Walikosea sana hiyo kwa Tundu ni advantage mnooooo
 
Oooh jibu zuri. Wa kwanza wa kwanza na wa mwisho wa mwisho

Kwahiyo orodha iliandaliwa kadri wagombea walivyokua wanirudishe form😍👍
Wewe waache wamesahau ile kanuni inasema wa mwisho atakuwa wa kwanza na wa kwanza atakuwa wa mwisho.....
 
Back
Top Bottom