Uchaguzi 2020 NEC: Tulifanya uteuzi wa wabunge wa viti maalum baada ya orodha ya majina hayo kuwasilishwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA 19 Novemba 2020

Uchaguzi 2020 NEC: Tulifanya uteuzi wa wabunge wa viti maalum baada ya orodha ya majina hayo kuwasilishwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA 19 Novemba 2020

Tume wameshajichanganya wenyewe,Tarehe 20 kupitia chombo cha habari walikiri kutokupokea majina Chadema,leo wanasema walipokea majina tarehe 19-wamejiaibisha kiukweli na kikubwa internet haidanganyi.

Atajisahihisha na kusema waliipokea tarehe 21. Lakini nayo itamtia kwenye matatizo ya namna Nusrat alivyoteuliwa, na kujaza fomu na kuwahi kwenye uapisho! Wakati mwingine ni bora kujinyamazia. Labda aseme ilipokewa masjala tarehe 19 na wakati anaongea ilikuwa haijafika mezani kwake.

Amandla...
 
Hakuna kosa kubwa Tz kama kugushi sahihi ya mtu sasa kama NEC wamegushi mimi naomba Chadema wafungue kesi ya kugushi sahihi.

CHADEMA WAKIFUNGUA KESI NAOMBA MNITAG.
Umethibitisha
 
kwani hao wabunge wa chadema mna maslahi gani kwann msiteue hata kutoka jeshi la polisi kwanini lazima chadema..,kwahiyo mnyika anaesema hajawasilisha majina ni mpumbavu na hajielewi.??
Yote yanaweza kuwa majibu sahii
 
Hawa Nec nao vinyonga.
20201127_172806.jpg
 
Hi nchi tumefika hapo; Taasisi ya umma inagushi barua?? Pole Tanzania umepatikana.
 
Kwa mlolongo wa matukio mbali mbali tata ya hii Tume ya Mahera, naelekea kumuamini Mnyika kuliko Mahera. Kuna JINAI imefanyika kughushi sahihi ya J.J.Mnyika ili kuhalalisha HARAMU! Yajayo yanatia KICHEFUCHEFU sana.
Mahera ni tapeli.
 
Mbona NEC walikataa kupokea majina toka Chadema!
Ile iliyokana kupokea majina ni NEC,
Hii iliyopokea majina tarehe 19/11/2020 ni Tume, huoni hata matamshi ni tofauti kabisa hapo mkuu.
 
Hata kama umenyofolewa ubongo basi hata kupapasa huwezi ? hivi Unajua kwamba Nusrat alitolewa gerezani tarehe 23 usiku na Mdee akishirikiana na mfumo ? ni wapi katibu mkuu wa Chadema alimsainisha fomu Nusrat aliyewekwa selo tangu july 2020 ? halafu hata kama kichwani umewekwa udongo tangu lini ccm na Ndugai wakawa watetezi wa wabunge wa Chadema ?
Mbona mmewasamehe Kama hakusaini form
Acha ujinga wewe
 
Kama ulimsikiliza JJ Mnyika, then ukamsikia Halima Mdee akisema Mbowe aliwapigia simu wabunge wote na kuwapongeza kwa kuteuliwa utagundua kuwa mwenyekiti wa kamati kuu Freeman Mbowe na Mkurugenzi wa NEC wanaongea lugha moja.

Swali ni kwamba kama Mnyika amekana kuandika barua NEC kwanini Mbowe aliwapongeza wabunge?

Mbowe na Mnyika wanapaswa kuhojiwa na Tume ya maadili ya viongozi.
Hapo kwenye Freeman Mbowe na mkurugenzi wa NEC wanaongea lugha moja nataka kukubaliana na wewe. Ili tuwekwe vizuri kwenye mwanga juu ya hili, NEC waweke hadharani form za wabunge walioteuliwa na kuapa ili umma uone signature ya aliyebariki hiyo orodha kupelekwa tume. Kama ni signature ya Mbowe ijulikane na kama ni ya Mnyika ijulikane na hata kama ni ya mwingine yeyote katika CHADEMA ijulikane. Pia ndugu johnthebaptist yafaa ujiulize maswali haya. Tume ilipata orodha ya "wabunge" 19 wa CHADEMA tarehe 19/11/2020 wakati huo ndani ya orodha hiyo kuna jina la mmoja akiwa mahabusu/gerezani Singida, Nusrat, sijui CHADEMA walikosa watu kabisa kumuorodhesha mtu aliyewekwa ndani kwa muda wa zaidi ya siku 180, walikua na uhakika gani kwamba angepitishwa na tume ya Charles Mahera huku akiwa anatuhumiwa na Jamhuri. Baada ya orodha kupokelewa, CHADEMA walivyo na nguvu, waliweza kumshawishi DPP amfutie mashtaka mtuhumiwa aliye gerezani na 23/11/2020 usiku akaweza kutolewa na kusafirishwa kwenda Dodoma kuapishwa kuwa mbunge. Hii inaacha maswali ambayo unaweza kusaidia kuyajibu.
 
Back
Top Bottom