Pre GE2025 NEC yabadilishwa jina sasa kuitwa Tume Huru ya Uchaguzi

Pre GE2025 NEC yabadilishwa jina sasa kuitwa Tume Huru ya Uchaguzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tuwape imani, mabadiliko ni mchakato. Kuanza tu kwa jina zuri inatosha kuanza kuwapa ujasiri hata wale maafisa wa tume.
 
View attachment 2959711
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema jina la Tume ya Uchaguzi (NEC) litabadilika Ijumaa Aprili 12, 2024 na kuwa Tume Huru ya Uchaguzi.

Katika taarifa iliyotolewa leo katika mitandao ya kijamii ya ofisi hiyo imesema:

“Tunapenda kuvitaarifu vyombo vyote vya habari kwamba, kufuatia tangazo la Serikali namba 225 la Machi 29, 2024 Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi namba 2 ya mwaka 2024, itaanza kutumika rasmi Aprili 12, 2024.

“Hivyo, kuanzia Aprili 12, 2024 jina la Tume litabadilika na litakuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi au kwa kiingereza Independent National Electoral Commission,”imesema taarifa hiyo.

Chanzo: mwananchi digital
Kwani Watanzania walikuwa na Tatizo na Jina la Tume au Mchakato mzima wa Uchaguzi? Maana kubadilisha jina bila kubadili mfumo mzima wa uendeshaji wa Tume hadi namna ya kuwapata Watendaji wa Tume Itakuwa tu sawa na Abdallah kumuita Dullah au Mohamed Kumuita Mudi a.k.a MO. HAPO HAKUNA UHURU BALI JINA LIMEBADILISHWA
 
Wananchi tunataka tume huru siyo kibadilisha jina kujiita huru wakati wasimamizi wakiwa wateule wa rais.Kwa mwendo Huu Hadi tutwangane makondendiyo muheshimu matakwa ya wanachi
 
1. Nani anateua wajumbe wa Tume hii?
2. Utaratibu wa kuwateua upoje?
3. Wanawajibika kwa nani?
 
Uhuru upi inayo hii tume??
Hata Korea kaskazini inaitwa Democratic peoples republic of korea 😄 🤣 😂 😆
 
Hivi majina ya walioomba kusimamia uchaguzi yameshatoka au bado yamekaliwa na Tume?
 
Back
Top Bottom