NECTA yatangaza matokeo ya Darasa la Saba 2019. Ufaulu waongezeka kwa asilimia 3.78

NECTA yatangaza matokeo ya Darasa la Saba 2019. Ufaulu waongezeka kwa asilimia 3.78

hata kumi bora haipo-ila nadhani kaizerege ni O level
Ahahahaaaa mtani [emoji28][emoji23][emoji1787] safari hii mambo yako Mara usipopapenda
Kaizirege English medium boarding schools ndo kemebos ni ya tatu kitaifa.

Na huwa haukosagi ten best kwenye matokeo yoyote yale.

IPO bukoba tz
shule%2Bbora.jpeg
FB_IMG_15686126438981483.jpeg
 
Nina furaha mnoo leo, yaani sijui nisemeje hakika Mungu ni mwema hakuacha kusikiliza kilio changu, mwanang kafaulu vzr pamoja na changamoto nyingi mnoo nilizopitia juu yake,yaani nimejikuta nalia hakika Mungu hajawahi kutosikiliza maombi ya watoto wake
 
Ana ufaulu gani, miaka ya hivi karibuni kufaulu mtoto darasa la 7 si jambo la ajabu anaweza asiende shuls mwaka mzima na akafaulu.
Tujuze ufaulu wake kiujumla na pole kwa changamoto
Mazingira ya mwanang na matokeo aliyopata Mamaake namshukuru Mungu n mengi amepitia mnooo ikiwepo na ugonjwa na mengine mengi mnoooo
 
Ana ufaulu gani, miaka ya hivi karibuni kufaulu mtoto darasa la 7 si jambo la ajabu anaweza asiende shuls mwaka mzima na akafaulu.
Tujuze ufaulu wake kiujumla na pole kwa changamoto
Hujui utamu wa mtoto mkuu,kufaulu ni kufaulu tu haijalishi wamefaulu wengi au wachache...
 
Nina furaha mnoo leo, yaani sijui nisemeje hakika Mungu ni mwema hakuacha kusikiliza kilio changu, mwanang kafaulu vzr pamoja na changamoto nyingi mnoo nilizopitia juu yake,yaani nimejikuta nalia hakika Mungu hajawahi kutosikiliza maombi ya watoto wake
Usisahau kumtolea Mungu sadaka ya shukrani, sana sana kuwasaidia wasiojiweza. Wape chochote kadri Roho wa Mungu atakavyokuongoza ila kubwa zaidi ni kuishi maisha matakatifu.
 
NECTA imetangaza Matokeo ya Darasa la Saba 2019 na kusema kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 3.78. Waliofaulu ni asilimia 81.50 ya watahiniwa 933,369. Pia Watahiniwa 909 wamefutiwa matokeo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kufanya udanganyifu
*****

Baraza la Mtihani la Taifa (Necta) limesema katika Mtihani wa Darasa la saba uliofanyika Septemba 11, 2019 wamebaini walimu Wakuu, Wasimamizi na walinzi walihusika kufanya udanganyifu

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde ameyasema hayo leo wakati akitangaza matokeo ya darasa la saba na kueleza kuwa katika kikao kilichokaa leo tayari wameshazitaarifu mamlaka za ajira na sheria ili ziwachukulie hatua waliohusika na udanganyifu huo. Ambapo kwa sasa udanganyifu kwa ujumla umepungua ambapo mwaka 2011 ulikuwa 9,736 na mwaka huu umefikia 900.

Amesema kuwa katika matokeo hayo asilimia 81.50 ya watahiniwa 933,369 wamefaulu huku watahiniwa 909 wakifutiwa matokeo kwa sababu ya udanganyifu, matokeo ya jumla yanaonyesha ufaulu umeongezeka kwa asilikia 3.78.

"Ufaulu katika somo la Kiingereza unaendelea kuimarika mwaka hadi mwaka hivyo juhudi za makusudi zinahitajika kuendelea kufanyika ili kuinua kiwango cha ufaulu katika somo hili," amesema Dk Msonde.

Aidha katika matokeo hayo, Grace Imori Manga wa shule ya msingi Graiyaki ya mkoani Mara ametangazwa kuwa wa kwanza kitaifa akifuatiwa na Francis Gwani wa shule ya msingi Paradise ya mkoani Geita na namba tatu imeshikiliwa na Loi Kitundu wa Shule ya msingi Mbezi ya Dar es Salaam.

Wengine katika orodha ya 10 bora ni Victor Godfrey wa shule ya msingi Graiyaki, Azizi Yassin wa Graiyaki goldie Hhayuma wa Graiyaki, Daniel Daniel wa shule ya msingi Little Mkoani Shinyanga, Hilary Nassor wa Peaceland ya Mwanza, Mbelele Mbelele wa Kwema Modern ya Shinyanga na Nyanswi Richard wa Graiyaki ya Mara.

Shule 10 bora kitaifa ni Graiyaki ya Mara, Twibhoki ya Mara, Kemebos ya Kagera, Little Treasures ya Shinyanga, Musabe ya Mwanza, Tulele ya Mwanza, Kwema Morden ya Shinyanga, Peaceland ya Mwanza, Mugini ya Mwanza na Rocken Hill ya Shinyanga.

Kimkoa, Mkoa wa Dar es Salaam umeshika namba moja ukifuatiwa na Arusha, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Mbeya, Simiyu, Njombe na Pwani.

Halmashauri 10 bora zimeongozwa na Arusha jiji, Ilemela, Kinondoni, Mwanza jiji, Ilala Manispaa, Moshi Manispaa, Bukoba Manispaa, Iringa Manispaa, Biharamulo na Arusha.
Me nataka kujua tu, ivi shule za serikali wanachukua mwisho wastani upi
 
Naona necta wameyafungulia sasa bhandugu hapa sielewi kitu nimeona ndugu yangu masomo 3 kapata C mawili kapata D na ana wastani wa C hapa kafaulu au ndo aanze kulima mpunga?
 
Nina furaha mnoo leo, yaani sijui nisemeje hakika Mungu ni mwema hakuacha kusikiliza kilio changu, mwanang kafaulu vzr pamoja na changamoto nyingi mnoo nilizopitia juu yake,yaani nimejikuta nalia hakika Mungu hajawahi kutosikiliza maombi ya watoto wake
Kufaulu la 7 siku hizi ni deal?maana naona wanaomaliza karibu wote ninaowafahamu wanafaulu
 
Back
Top Bottom