Nehemia Mchechu bila ya ‘speed governor’ ni tatizo. Ndugu zangu wa mitaa ya ‘Al Muntazir’ Upanga mjipange

Nehemia Mchechu bila ya ‘speed governor’ ni tatizo. Ndugu zangu wa mitaa ya ‘Al Muntazir’ Upanga mjipange

Hilo shirika lilianzishwa kutoa unafuu wa makazi kwa wafanyakazi na watu wa kawaida wakazi wa mjini, lakini tunashanga limebadilika kuwa la kuwajengea matajiri nyumba na sasa wanataka kumilikisha matajiri maeneo wanayoita prime areas kwa kujificha kwenye kichaka cha ubia.​
Ndugu zama zimebadilika, mazingira yamebadilia na maisha yamebadilika. NHC ya zama hizo ya sera za kijamaa ilishakufa kitambo sana. Watanzania hatuhitaji tena kuwa na NHC ya kutujengea nyumba walalahoi maana NHC haiokoti pesa, tunataka NHC ya kusaka pesa za matajiri wanaotaka kuishi sehemu chache specho, ili hizo pesa tukajengee madarasa, zahanati, vyoo vya shule nk.

Watanzania walalahoi huenda tuko karibu milioni 40, sasa NHC itajenga nyumba ngapi ili sote tukae?
 
Embu tuwaze tu kisayansi.
Kuna jengo la ghorofa mbili la kizamani (chakavu!)la NHC lipo Upanga ambalo lina wapangaji watatu, kwa mwezi linaipa NHC jumla ya kodi ya shilingi laki tatu tena kwa kushikana mashati!

Anatokea mwekezaji anataka hilo eneo ili kujenga jengo jipya la kisasa kwa ubia na NHC. Atavunja hilo jengo na ndani ya mwaka mmoja Atajenga jengo jipya lenye urefu wa ghorofa 15, ghorofa tano za juu atawapa NHC (ambazo zitapangishwa kwa wapangaji 20, kwa mwezi wapangaji hao kwa jumla watailipa NHC wastani wa shilingi 10milioni bila longolongo!).


Sasa utawashauri NHC wabakie na jengo lao la kizamani ili kuvuna laki tatu kwa mwezi, au waingie ubia ili kuvuna milioni 10 kwa mwezi?
Afu mpangaji anajiita mnyonge
Wakuambiea wajenge hawataki
 
Sasa km unataka kukwepa mikataba unakua unaukataa uhalisia na haya ni malalamiko baseless kabisa
We mtu anaweza kukupangia nyumba yako uifanyeje/uitumie vipi?

Cha kuazima hakistiri matako jmn mjenge..waliojenga Boko Bunju nk si kwamba UN Road AlMuntazir hawakupaona
Kwani hizo nyumba ni mali ya mchechu au ni za umma, hao matajiri kwa nini wasiende kujenga huko boko na bunju..
 
Hii operation mbona ni ya nchi nzima mkuu?
Lengo lake ni kuondoa majengo ya kizamani yanayo milikiwa na NHC, City Centres nchi nzima na ku replace na mapya ya kisasa yenye kuendana mandhali ya kisasa na eneo husika, kama gorofa ndefu zaidi.

By the way the man is my Role Model.
 
Kwani hizo nyumba ni mali ya mchechu au ni za umma, hao matajiri kwa nini wasiende kujenga huko boko na bunju..
Kwa urahisi mngehama tu
Mana sijui mtamshinda NHC/Mchechu kwa hoja gani

Wewe mpangaji ndo ukajenge Bunju
Hapo NHC ni kwako?
Bunju kwa R.O.I ipi?
 
Ndugu zama zimebadilika, mazingira yamebadilia na maisha yamebadilika. NHC ya zama hizo ya sera za kijamaa ilishakufa kitambo sana. Watanzania hatuhitaji tena kuwa na NHC ya kutujengea nyumba walalahoi maana NHC haiokoti pesa, tunataka NHC ya kusaka pesa za matajiri wanaotaka kuishi sehemu chache specho, ili hizo pesa tukajengee madarasa, zahanati, vyoo vya shule nk.

Watanzania walalahoi huenda tuko karibu milioni 40, sasa NHC itajenga nyumba ngapi ili sote tukae?
Kwa hiyo malengo ya NHC yamebadilika kuwa shirika la kuwajengea matajiri nyumba......kwani matajiri wana shida katika kujenga nyumba zao wenyewe hadi NHC ianze kuwajengea.
 
Hapo hakuna cha mikataba inasemaje, shirika linakusanya kodi kwa nini lisikarabati na kujenga nyumba badala ya kutaka kuwapa matajiri hizo nyumba kwa kisingizio cha kuingia ubia, yanajengwa mazingira ya upigaji na rushwa nono nono.​
Kwa mfano halisi unaweza kukuta, Kodi inayokusanywa na NHC kwenye jengo moja chakavu lillopo prime area labda ni wastani wa shilingi laki tano kwa mwezi (kwa miaka mitatu: 500,000 x 12 x 3 = 18milioni) wakati gharama za maintenance kwa mwezi ni wastani wa shilingi laki tatu (kwa miaka mitatu: 300,000 × 12 x 3 = 10.8milioni), na kulifanyia ukarabati muhimu hilo jengo (kama kupiga rangi, sewage system, umeme, vitasa, milango, vioo, madirisha, sakafu) kila baada ya miaka mitatu ni shilingi milioni 20. Sasa piga mahesabu.
Mapato: 18milioni
Maintenance+Ukarabati: 30.8milioni
Hasara: 10.8milioni

Kwanini NHC isiwaze uwekezaji wenye ubia katika mazingira hayo?
 
Wewe ni mpangaji tu, hupaswi kumpangia mwenye nyumba nini cha kufanya kwenye nyumba zake.

Kama NHC wameamua kuingia ubia na watu wengine ili kuvunja hizo nyumba ili wajenge kitu kingine, wewe mpangaji unakuhusu nini?

Kama unaona NHC wanakuzingua si uhame tu, kwanini ung'anganie hapo hapo kama kwako hapo?
 
Hivi hii sera ya ubia ya NHC ilipelekwa kabisa kwenye baraza la mawaziri, wakailewa na kusema sawa.

Mtu ana mpango wa kwenda kuvunja majengo kadhaa kisa tu yapo prime areas na kuwatoa wapangaji sio tu hana hela ya kuendeleza yeye mwenyewe bali the immorality of it all is beyond me.

Kama hela kila kitu basi sasa hivi kusingekuwa na nyumba za ovyo Mikocheni, Msasani, Tetegeta, Kariakoo, Ilala na prime areas zingine za bongo.

Kila mwenye nyumba tokea miaka ya 80 isiyoendana na nyumba zinazojengwa leo maeneo hayo sasa hivi ingekuwa keshahama kitambo kwa kuuza.

Uwezi kunyanyasa watu kwa sababu eneo ni prime na serikali ina miliki nyumba kwa hivyo vunja tu.

Juzi raisi Samia katoka kwenye msiba uingereza eneo alilopanda basi maeneo ya ‘Marble Arch’ mbele kidogo tu ‘Oxford Street’ sidhani kama kuna prime area duniani kama hapo (labda Tokyo) na kuna council flats zilijengwa zamani. Safari yake ya mile mbili kufika msibani mpaka Westminster njia nzima ina sehemu kuna nyumba za serikali in short ‘west end’ yote ina maeneo yana council flats ambazo ingelikuwa ni matakwa ya matajiri tu wangeshanunua zote na kuzivunja. Lakini hata kwa nchi za mabeberu it’s immoral and inhumane uwezi fanya ivyo.

Na ndio sera inayofanya watu matajiri watafute maeneo mengine ya kuendeleza na kutengeneza future prime areas.

Ni hivi huyu Nehemia hana uwezo na nafasi anayopewa hapo NHC alianza Tibaijuka kumfunga speed governor alizuia huu mpango alipokuwa waziri, Lukuvi nae akamfunga tena speed governor kwenye kuwapandishia kodi wapangaji kwa asilimia 200% na kumtaka aache tena kupandisha kodi ovyo (hizo zilikuwa zama za J.K) na Magufuli ndio akamtibua kabisa kwa kutaka kuendelea serikali kumpatia dhamana ya mikopo ambayo inaishia kuhudumiwa na walipa kodi badala ya miradi anayojenga.

Huyo mtu hana uwezo wa kufanya miradi ya kibiashara inayohitaji mbinu anataka vitu rahisi tu kutekelezeka.

Hiyo sera inaenda waumiza watu kwa sababu ambazo hazina msingi wa kibiashara ya shirika la umma ata kidogo.
Katiba baba achana na Nehemia. Mkiambiwa katiba mnaona watu ni wasaliti. Tulia wembe ukate
 
Kwa hiyo malengo ya NHC yamebadilika kuwa shirika la kuwajengea matajiri nyumba......kwani matajiri wana shida katika kujenga nyumba zao wenyewe hadi NHC ianze kuwajengea.
NHC haijawahi kuwa na sera ya kuwapangisha wanyonge (maskini), sera zao za zamani zilikuwa kutoa huduma kwa watanzania wote na sio kufanya biashara, kwa sasa sera zao zimejikita kufanya biashara na watu wote.

Matajiri hawana shida ya kujengewa nyumba na NHC, wao wana shida ya kufanya biashara na NHC katika sekta ya makazi. Matajiri wana pesa (lakini hawana maeneo prime) na NHC hawana pesa (lakini wana maeneo Prime), lakini wote wawili wanataka kufanya biashara. Nini kitatokea? Watakaa mezani na kufanya deals, mwisho wa siku maisha yanakwenda.
 

Hiyo ni moja ya sheria amongst several others inazo regulate hilo shirika jinsi litakavyoendeshwa na right of occupancy za wapangaji.

Mimi sio mwanasheria wa wapangaji kusema nipitie zote ila kwa kuwa ni nchi ya kufanya copy and paste ya sheria; ukipitia zote hitimisho litakuwa ni hilo hilo sio sahihi kutoa watu kiholela holela.

Kuna angle nyingi huu mjadala ungeweza ongelewa financial appraisal ya hiyo miradi au uhalali wa sheria kuvunja nyumba na kuwatoa watu kama mbwa.

Binafsi sikuwa na shida na ya angle hizo; isopokuwa ethics za hiyo sera ni shida na za unyanyasaji hakuna serikali makini inayoheshimu watu wake au CSR demands za dunia ya leo inayoweza ruhusu ata private business kuvunja mikataba ya wapangaji na kubomoa nyumba bila ya kuelewa tenants wanaenda wapi.

Mimi sitakuwa muhanga wa hilo zoezi isipokuwa hiyo sio approach sahihi ya uwekezaji wa serikali ni watu waliokosa ubinifu na utu ndio wanapenda suluhisho za ivyo zenye kuwaumiza wengine.

As for me usiku mwema and thanks all for your input.
Mkuu, watu wanajitoa ufahamu tu na huenda wengine ni machawa wanatumika, hapo kuna uonevu ulio wazi ili kuwanufaisha wajanja wachache. Kuwasemea wanaoonewa siyo lazima kwamba sisi ni wapangaji kwenye hizo nyumba, wengine tunaishi kwenye nyumba zetu lakini hatupendi watu wa hali ya chini waonewe.
 
Bora zivunjwe, muhame mkajenge zenu.
Mmejisahau sana nyinyi wapangaji wa Upanga. Hela zenu mnanywea bia, hamjengi. Mkifa, watoto wenu watarithi nini?
 
Kinachofuata ni kuhamisha walimu woote wa SUA, Mzumbe na UDSM. Nyumba ziwe mabweni ya wanafunzi. Walimu wote 'wanapaswa' kuwa na nyumba zao katika umri huu.
Hizi nyumba za chuo zinafanya wengi wanabweteka. Wanastaafu wanaenda tena kupanga.
Kuanzia sasa nyumba za staff wa vyuo inatakiwa wakae wanafunzi wa Masters na phD.
Walimu wakajenge zao.
 
Mkuu, watu wanajitoa ufahamu tu na huenda wengine ni machawa wanatumika, hapo kuna uonevu ulio wazi ili kuwanufaisha wajanja wachache. Kuwasemea wanaoonewa siyo lazima kwamba sisi ni wapangaji kwenye hizo nyumba, wengine tunaishi kwenye nyumba zetu lakini hatupendi watu wa hali ya chini waonewe.
Halafu watu wa aina hii kesho watatatea kwa nguvu zote bunge la ulaya likitunga uongo serikali imetoa wananchi kwenye njia ya bomba la EACOP na kuweka ushahidi sio kweli wamelipwa fidia na kujengewa nyumba kuonyesha ethical credentials za serikali mbele ya mabeberu. Bila ya kuelewa morally hakuna tofauti na hiki wanachotaka kufanya NHC ni kitu hiko hiko na kina stahili equal treatment kwa wapangaji wao.

Nilichojifunza kwa watetezi wa hii sera ya NHC awafahamu right of occupancy ya mikataba ya NHC au public housing yoyote duniani. Wao wanadhani tenants agreement za public housing ni sawa na nyumba za kupanga mitaani. So awawezi ona mfanano wa kuwa treat sawa wapangaji wa NHC na raia waliofidiwa njia ya bomba ni kitu sawa.

Watu wanaongea bila ya kuzingatia mikataba ya NHC si ajabu ata huyo mkurugenzi mwenyewe aelewi rationale ya mikataba yao ni sheria zilizopo kuhusu uendeshwaji wa hilo shirika ndio maana kumtoa Mbowe billicanas ilikuwa mbinde pamoja na madeni aliyokuwa nayo.

Tofauti ni kwamba Mbowe ana hela na public influence ya ku challenge watanzania wengi hawana hizo resources wala mbinu za ku mobilise support and fight their course.
 
Hivi hii sera ya ubia ya NHC ilipelekwa kabisa kwenye baraza la mawaziri, wakailewa na kusema sawa.

Mtu ana mpango wa kwenda kuvunja majengo kadhaa kisa tu yapo prime areas na kuwatoa wapangaji sio tu hana hela ya kuendeleza yeye mwenyewe bali the immorality of it all is beyond me.

Kama hela kila kitu basi sasa hivi kusingekuwa na nyumba za ovyo Mikocheni, Msasani, Tetegeta, Kariakoo, Ilala na prime areas zingine za bongo.

Kila mwenye nyumba tokea miaka ya 80 isiyoendana na nyumba zinazojengwa leo maeneo hayo sasa hivi ingekuwa keshahama kitambo kwa kuuza.

Uwezi kunyanyasa watu kwa sababu eneo ni prime na serikali ina miliki nyumba kwa hivyo vunja tu.

Juzi raisi Samia katoka kwenye msiba uingereza eneo alilopanda basi maeneo ya ‘Marble Arch’ mbele kidogo tu ‘Oxford Street’ sidhani kama kuna prime area duniani kama hapo (labda Tokyo) na kuna council flats zilijengwa zamani. Safari yake ya mile mbili kufika msibani mpaka Westminster njia nzima ina sehemu kuna nyumba za serikali in short ‘west end’ yote ina maeneo yana council flats ambazo ingelikuwa ni matakwa ya matajiri tu wangeshanunua zote na kuzivunja. Lakini hata kwa nchi za mabeberu it’s immoral and inhumane uwezi fanya ivyo.

Na ndio sera inayofanya watu matajiri watafute maeneo mengine ya kuendeleza na kutengeneza future prime areas.

Ni hivi huyu Nehemia hana uwezo na nafasi anayopewa hapo NHC alianza Tibaijuka kumfunga speed governor alizuia huu mpango alipokuwa waziri, Lukuvi nae akamfunga tena speed governor kwenye kuwapandishia kodi wapangaji kwa asilimia 200% na kumtaka aache tena kupandisha kodi ovyo (hizo zilikuwa zama za J.K) na Magufuli ndio akamtibua kabisa kwa kutaka kuendelea serikali kumpatia dhamana ya mikopo ambayo inaishia kuhudumiwa na walipa kodi badala ya miradi anayojenga.

Huyo mtu hana uwezo wa kufanya miradi ya kibiashara inayohitaji mbinu anataka vitu rahisi tu kutekelezeka.

Hiyo sera inaenda waumiza watu kwa sababu ambazo hazina msingi wa kibiashara ya shirika la umma ata kidogo.
Wivu wa kitoto unakusumbua
 
Back
Top Bottom