Nelson Mandela alihalalisha uporwaji wa Ardhi ya Afrika Kusini kwa Boers halafu anaitwa Baba wa Afrika. Afrika tumerogwa na nani?

Kuna watu wana akili za ajabu sana,wao hutaka maendeleo na mafanikio kwa kufa au kudhurika kwa wengine
 
Mleta mada na watu wa namna yako ni wapuuzi sana, Kwahiyo mulitaka SA iwe kama Zimbabwe?
Acha upuuzi wako wewe mbilikimo wa akili..

Harakati za kudai ukombozi huko South Afrika zilikuwa ni za kumtoa jela Mandela kwa gharama ya damu na ardhi ya watu wake?

Angola,Msumbiji na Nchi zingine zilidai haki yao ya Ardhi badala ya uhuru wa bendera kama wa South Africa na Zimbabwe..

Zimbabwe imefeli kwa sababu hawakudai haki sawia wakati Mugabe anapewa uhuru wa bendera kama Mandela ,so walivyokuja kunyakua kwa nguvu ndio wameharibikiwa ila wangenyakua from bugging wala wasingekuwepo walipo sasa.
 
Unasema hivyo sababu unaweza kununua kiwanja dar es sallam au arusha au mwanza ai mikocheni ili mradi pesa yako. Wenzio weusi huko SA hawaruhusu hata kudhuru fukwe za miji wanayoishi makaburu.
 
Duh kwa ambavyo nimekua namkubali Mandela, mngesubiri kizazi chetu kiondoke kabla kuanza kumsema...
Wengi wanamkubali kwa hisia tu. Mandela aliyeingia jela si mandela aliyetoka jela.

Sawa na mbowe aliyetoka ikulu si mbowe aliyeingia ikulu.
 
Hujamalizia mwambie hao viongoz wote waliopora mashamba na Mali za wazungu walikuwa na mwisho mbaya Sana
 
Kabla ya kumlaumu mtu hata kama waona una haki jaribu hata kidogo kuvaa uhusika au viatu vya huyo unaayemlaumu then ndio uendelee kumlaumu..
~Anonymous
 
Usikimbilie kutukana jibu hoja,uchawa wako Kwa Samia anakutoa ufahamu unatukana kila anayemkosoa.
Rotten mind,kuna hoja gani hapo?

Anzisha hiyo mnayoita mada tutakuja kujibu,hapa tuko kwenye mada ya Mandela aliyewauza watu wake Ili atoke jela.
 
Habari hizi zina fikirisha Sana.

Mara kadhaa nimekuwa nawaza Sana na nakosa majibu muhimu.

(1) Mandela aliifanyia nini Afrika kuzidi akina Nyerere mpaka jina lake lionekane lipo ju zaida ya wengine??

(2) Mandela alikubali vipi kuona wazungu wamegawana aridhi na rasilimali asili za Nchi hiyo? Ambapo mpaka sasa waafrika wengi maisha yao ni mabovu kuliko wazungu.
 
Too harsh...

Miaka 27 gerezani sio kitu kidogo, isitoshe baada yake wamepita marais weusi kama 3, kwanini hawajapigania hiyo ardhi?.....ilikuwa lazima kazi zote azifanye peke yake ?

Kwanini yeye ndiye awe wakubeba lawama ?
 
Ilikuaje akawauza wenzio from all such sufferings?

Narudia tena kuna waliokufa kwa ajili ya harakati ,kwa nini auze Nchi Ili tuu atoke jela?
Alikuuzia wewe? Kama nia ilikuwa ni kutoka jela angetoka 1985 lakini alikataa. Alitoka 1990 baada ya De Klerk kukubali utawala wa walio wengi.
Muwe na adabu.

Amandla....
 
Kwa wakati ule alikuwa sahihi kwani hata angekomaa wazungu wakaacha ardhi bado wangeweza kumkwamisha kama yaliyotokea Zimbabwe.
Ila Sasa nadhani ni muda muafaka wa kuwa na mazungumzo ya kitaifa ili wazungu waachie baadhi ya ardhi wapewe weusi japo hii rangi yetu sidhani kama wataifanyia lolote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…