NEMC wekeni utaratibu wa ibada; huku mtaani leo hakukaliki kwa sababu ya kelele!

NEMC wekeni utaratibu wa ibada; huku mtaani leo hakukaliki kwa sababu ya kelele!

Ungeweka na kaushahidi ka picha tuone namna ulivyozungukwa na nyumba za ibada [emoji4]
 
Hata kama serikali haina dini lakini hapa tulipofika sasa kuna haja ya serikali kuingilia kati. Hapa mtaani kwangu leo hakukaliki kwa sababu ya kelele za maspika ya ibada. NEMC walisema wataweka utaratibu wa kufanya ibada lakini sijui wanakwama wapi mpaka sasa hawajachukua hatua zozote. Hadi natamani niuze nyumba hii nihamie mkoa mwingine.

Kuna nyumba nne za ibada kuzunguka makazi yangu na kila nyumba ina spika nne – kila spika imetazama upande mmoja wa dunia (kusini, kaskazini, magharibi na mashariki). Jumla ya maspika ni 16 na wote wanahubiri kwa wakati mmoja, tena kwa sauti kubwa sana. Wewe fikiria maspika 16 yamekuweka kati na yote yanaunguruma kwa wakati mmoja! Kuna kusikilizana hapo?

Halafu leo ni kama vile wameamua kuongeza sauti kwa makusudi ili kutukomesha. Nipo hapa nafanya kazi zangu za kujenga taifa lakini nahisi kichwa kinawaka moto. Sasa kama watu wanaohubiriwa wapo ndani ya nyumba ya ibada kuna haja gani ya kuning’iniza maspika juu ya paa kama sio ukorofi?

Na hapo bado kesho na keshokutwa wenzetu watakapoungurumisha mavinanda na kuimba mapambio. Na wao nyumba zao za ibada zipo hapa hapa jirani. Ni kero kubwa sana kwa kweli, hasa unapokuwa unafanya kazi inayohitaji utulivu.

Naomba NEMC waingilie kati mara moja kwa kuweka utaratibu wa ibada wa kiistarabu badala ya huu utaratibu wa ovyo wa kuhanikiza kelele mtaa mzima.
Pole sana ndugu yangu,hawa jamaa wanakera sana. Mie moja ya sifa ya kiwanja cha kujenga ni kutokuwa karibu na makanisa au misikiti. Huwa sipendi kelele kabisaa nikipumzika
 
Pole sana ndugu yangu,hawa jamaa wanakera sana. Mie moja ya sifa ya kiwanja cha kujenga ni kutokuwa karibu na makanisa au misikiti. Huwa sipendi kelele kabisaa nikipumzika
Asante mkuu. Hawa watu wanatusumbua sana aisee
 
Waumini karibu wote wanamiliki simu. Alarm zipo kwenye kila simu. Wawe wanaset hizo alarm kwenye simu zao muda ukifika zinalia na kuwaamsha kwenda ibadani badala ya kutumia maspika yanayochafua hewa mtaa mzima.
Hili la Waumini kuweka Alarm kwenye simu zao au Kuamshana kwa kipigiana simu inapofika muda wa ibada ni jambo la MUHIMU SANA kwa Waislam na Wakristo pia

Hakuna sababu ya kuwapigia kelele na kuwanyima usingizi na utulivu wengine ambao yamkini sio waimini wa dini hizo

Hivi kuamshana kwa Alarm au kwa kupigiana simu ni Dhambi???

Msaada tafadhali
 
Hili la Waumini kuweka Alarm kwenye simu zao au Kuamshana kwa kipigiana simu inapofika muda wa ibada ni jambo la MUHIMU SANA kwa Waislam na Wakristo pia

Hakuna sababu ya kuwapigia kelele na kuwanyima usingizi na utulivu wengine ambao yamkini sio waimini wa dini hizo

Hivi kuamshana kwa Alarm au kwa kupigiana simu ni Dhambi???

Msaada tafadhali
Inabidi wawe wastaarabu, wawe wanapigiana simu na kuweka alarm. Wanatusumbua sana hawa viumbe aisee!
 
Hata kama serikali haina dini lakini hapa tulipofika sasa kuna haja ya serikali kuingilia kati. Hapa mtaani kwangu leo hakukaliki kwa sababu ya kelele za maspika ya ibada. NEMC walisema wataweka utaratibu wa kufanya ibada lakini sijui wanakwama wapi mpaka sasa hawajachukua hatua zozote. Hadi natamani niuze nyumba hii nihamie mkoa mwingine.

Kuna nyumba nne za ibada kuzunguka makazi yangu na kila nyumba ina spika nne – kila spika imetazama upande mmoja wa dunia (kusini, kaskazini, magharibi na mashariki). Jumla ya maspika ni 16 na wote wanahubiri kwa wakati mmoja, tena kwa sauti kubwa sana. Wewe fikiria maspika 16 yamekuweka kati na yote yanaunguruma kwa wakati mmoja! Kuna kusikilizana hapo?

Halafu leo ni kama vile wameamua kuongeza sauti kwa makusudi ili kutukomesha. Nipo hapa nafanya kazi zangu za kujenga taifa lakini nahisi kichwa kinawaka moto. Sasa kama watu wanaohubiriwa wapo ndani ya nyumba ya ibada kuna haja gani ya kuning’iniza maspika juu ya paa kama sio ukorofi?

Na hapo bado kesho na keshokutwa wenzetu watakapoungurumisha mavinanda na kuimba mapambio. Na wao nyumba zao za ibada zipo hapa hapa jirani. Ni kero kubwa sana kwa kweli, hasa unapokuwa unafanya kazi inayohitaji utulivu.

Naomba NEMC waingilie kati mara moja kwa kuweka utaratibu wa ibada wa kiistarabu badala ya huu utaratibu wa ovyo wa kuhanikiza kelele mtaa mzima.
Hii nchi hivi sasa imevaa chupi kichwani, NEMC wanajitahidi sana ila watu jamii ya Chalamila na Makala ndiyo shida kubwa, mbaya zaidi mamlaka ya uteuzi inawachekea badala ya kuwakemea
 
hakuna mtu yoyote ataweza kupiga marufuku adhana nyinyi mliee humu mitandaoni mpaka mfe
 
hakuna mtu yoyote ataweza kupiga marufuku adhana nyinyi mliee humu mitandaoni mpaka mfe
KKKT wameonesha nia. Na nyie kuweni wastaarabu, tuondoleeni maspika misikitini.
 
Back
Top Bottom