Nenda Sabaya lakini bila wewe haya yasingewezekana kutokea wilaya ya Hai

Jiandae kisaikolojia, hii kesi aliyonayo sasa hivi ni mbaya kuliko hiyo aliyopigwa mvua 30!! Jamaa lako lilivyo jinga liliambatana na Mrosso hadi bank kwenda kumtolesha kwa nguvu mil 90, watu walimuona na camera za benki zilimnasa pia!! Then kuna kesi za ubakaji zinakuja, sasa kubaka nako alitumwa na Jiwe?
 
akija raisi akakomba hela zote benki maana yake mapato ya serikali yakuwa yako juu sana
bila shaka na hiyu Rais wa namna hii mtamsifia kwa kusema hajawahi tokea raisi akakusanya mapato makubwa kiasi hiki
hizi ndii akili zenu Uvccm
 
Nenda kaolewe nae huko gerezani
 
Hayo ni majukumu ya kazi yake na hayatoshi kuhalaalisha yeye awe muahalifu. Sabaya ukumbuke hakuyafanya hayo mazuri kwa hisani bali alilipwa mshahara, alipewa nyumba ya kuishi bure na pia gari la kumrahisishia yeye namna ya kufanya kazi na tena lilijazwa mafuta full tank buree.

Saanyingine wema wa mtu ambaye ni mtumishi usiwe unatetewa sana 7bu kodi zetu ndiyo zinazomlipa yeye na majukumu yake ya kazi yapo kimaandishi. Watanzania tumezidi sana hasa hizi nyakati kutetea mazuri ili yafunike mabaya wakati inaaminika kwamba angefuata miongozo ya kazi yake na majukumu yake bila kuzidisha wala haya yasingemkuta
 
Hiyo namba mbili mbona ilitokea TZ nzima, ila kitu ambacho uneshindwa kung'amua ni kuwa hayo uliyotaja ni kama 1% compared to 99% ya uhuni na kuumiza watu.
 
Ujumbe wako hauna uzito wowote wa kumfanya Sabaya aitwe mzalendo.

Unawezaje kumuita mzalendo mtu ambae amekiri mwenyewe kutenda makosa makubwa kiasi kile kwa kisingizio cha kwamba alikuwa anatekeleza maagizo?

Mahakama imemkuta na hatia, muache atumikie kifungo chake bila chokochoko.

Ni ujasiri wa ajabu kiasi gani aliupata wa kuvamia na kuumiza wenzake kwa kutumia kigezo cha upinzani? je wapinzani ndo wanastahili kuvamiwa, kuteswa, kupigiliwa misumari au kuporwa?

Eti mzalendo kisa kaisaidia CCM kushinda viti vya nafasi mbalimbali wilayani Hai kwenye uchaguzi mkuu!!! Hii ni aibu kubwa! nani alikufundisha kwamba kuisaidia CCM kubaki madarakani ni kigezo kinachotumiwa kupima uzalendo wa mtu? Kama hizi ndizo akili tunazotegemea ziongoze nchi tumekwisha.

Ungemuita mzalendo endapo tu angeweza kusimamia haki na kuheshimu utashi wa wananchi kwa kukemea na kuzuia uporaji wa kura.
Mtu mzalendo ni yule anaeshimu maamuzi ya wananchi na sio anaepora haki yao.
 
Acha uongo wewe yani Halmashauri ya Hai itoke mwisho hadi kuwa wa 4 kwa kitu gani cha kiuchumi kilichopo Hai.
Yaani anaokoteza okoteza vijihabari kama anayejisaidia vichakani na kuleta hapa.
Najiuliza kwa nini wanao mtetea Sabaya uwezo wao wa akili uko chini sana?
Maana kama ni uchama mbona ndani ya CCM wenye akili wakiwamo viongozi wa juu walikasirishwa kabisa na tuhuma hizo?
 
At last nimemu hurumia sana huyu dogo, yaani CCM wamemtumia ili kufanikisha mambo yao na mwishoni wamemfunga, wanasiasa watu wabaya sana
 
Hujasahau kusema hata ubambikiaji, na kuvuruga biashara na bustani kusingefanikiwa na kuupora ubunge wa mtu.
 

Wewe ndiye yule ambaye jambazi sabaya alijitetea ameshakutolea mahari?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…