General Mangi
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 15,303
- 23,064
Upigaji tu humu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unatafuta uteuzi au??unatujazia server humuWanabodi,
Niko Standby kuwaletea link ya uzinduzi huu.
====
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo ashiriki kwenye uzinduzi wa makala maalumu iitwayo ‘Royal Tour’ jijini New York nchini Marekani.
Makala hayo maalumu ambayo mchakato wake umefanyika kwa takribani mwaka mzima umemshirikisha moja kwa moja Rais Samia akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii nchini Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.
Uzinduzi huo wa aina yake unahudhuriwa na takribani watu 400 unafanyika kwenye Jumba Mashuhuri la Makumbusho liitwalo Guggenheim kuanzia saa moja na nusu za usiku za Marekani, sawa na saa nane na nusu usiku kwa Afrika Mashariki.
Miongoni mwa washiriki ni pamoja na wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, viongozi wa kisiasa, mashirika ya kimataifa, waandishi wa habari na Watanzania waishio Marekani.
Pia wafadhili na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za uhifadhi kama TANAPA, NCAA, TTB, TAWA, TFS na makundi ya wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Tanzania wakiwakilishwa na CTI, TBA, TPSF, TATO na CEOrt wahudhuria.
Shughuli hiyo inaoneshwa mubashara kupitia televisheni za Marekani kwenye mfumo wa utangazaji wa umma (PBS) kupitia kituo cha televisheni cha WTTS yenye watazamaji takribani milioni 3.5 na baadaye makala hayo itaoneshwa kwenye zaidi ya chaneli 300 zinazowafikia takribani asilimia 86 ya Wamarekani.
Makala hayo yatazinduliwa pia jijini Los Angeles, Aprili 21, mwaka huu na baada ya matukio hayo mawili, filamu hiyo pia itarushwa kwenye mtandao wa kidijitali wa Amazon na Apple TV.
Kwa Tanzania, filamu hiyo itazinduliwa kwanza jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili na baadaye visiwani Zanzibar tarehe 7 Mei.
Taarifa zaidi soma;
Uzinduzi wafanyika New York
Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour umefanyika usiku wa kuamkia leo Aprili 19, 2022 Jijini New York Nchini Marekani na kuhudhuriwa na watu wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.
Filamu hiyo maalumu ilitengenezwa kwa mwaka mzima ikimshirikisha Rais Samia kama mhusika mkuu akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii #Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na zaidi ya watu 400 katika Jumba la Makumbusho la Guggenheim, baadhi ya waliohudhuria ni wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, wanasiasa, mashirika ya kimataifa.
View attachment 2192524View attachment 2192525View attachment 2192528
View attachment 2192558
View attachment 2192538
Paskali
DSM
Tanzania
Sasa wewe unazila saa ngapi,pesa mama anatafuta ila zinaishia mifukoni mwa wadau wasio na huruma,wanazitumbua.Wewe ni chadema nini ? naona unalia lia kweli ...
Kijana wangu Paskali kwa hili umepuyangaUpdate.
Event hii ya uzinduzi wa filamu ya Royal Tour haiko live.
Kama kuna member wetu yoyote uko ukumbini, please share, na mimi will share the few clips that I have
P
Anafunika legasiDaaah Bora asingetumia ngeli kuzungumza, ngeli mbovu au wangemwandikia akawa anasoma tu, Huyu Na Mzee Baba Hawana Tofauti [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
JF ya sasa hivi imejaa siasa za propaganda za vyama na chuki tu, nothing seriousSijui hii if ya siku hizi imekuwaje?!. Ingekuwa ni ile JF ya enzi zile, saa hizi ungekuta tuna updates zaidi ya members 10!.
Yaani unamaanisha kati ya hao waalikwa zaidi ya 400, hakuna mwana JF yoyote kutu update!.
P
mangi punguza tamaa ya wizi, utabinuliwa siku moja.Kuna sehemu kuna liboss jinga kweli kweli linajifanya liaminifu linadhibiti halina hata gari linapanda daladala huku linakula kwa mama lishe hovyo Sana linajifanya liaminifu wenzake juu wanaenda kuzila tu bila hata huruma.
Halafu likistaafu masikini litajutia linadhani litazikwa na tuzo.
Unalipa kodi juu wanaenda zila.Then Hakuna hatua zozote zinachukuliwa
Hisia za uzalendo waliziharibu mboga mboga ikawa ni taifa la wanufaika wachache huo uzalendo utatoka wapi?Mkuu Paskal,usidanganyike na uzalendo katika taifa hili.Trust me hata URUSI akituvamia na kutupiga TZ, bado wa TZ tutamshangilia PUTIN na kufurahia wanajeshi wa SAMIA wanavyopelekewa moto (ambao ni ndugu zetu)
Shida zinaenda liwa wakati chini wakiteseka kukusanya hata kumi awapati.mangi punguza tamaa ya wizi, utabinuliwa siku moja.
Yaaani unamchukia mtu kwasababu kakudhibiti usiibe
Channel ten,imeonyeshwa liveWanabodi,
Niko Standby kuwaletea link ya uzinduzi huu.
====
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo ashiriki kwenye uzinduzi wa makala maalumu iitwayo ‘Royal Tour’ jijini New York nchini Marekani.
Makala hayo maalumu ambayo mchakato wake umefanyika kwa takribani mwaka mzima umemshirikisha moja kwa moja Rais Samia akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii nchini Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.
Uzinduzi huo wa aina yake unahudhuriwa na takribani watu 400 unafanyika kwenye Jumba Mashuhuri la Makumbusho liitwalo Guggenheim kuanzia saa moja na nusu za usiku za Marekani, sawa na saa nane na nusu usiku kwa Afrika Mashariki.
Miongoni mwa washiriki ni pamoja na wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, viongozi wa kisiasa, mashirika ya kimataifa, waandishi wa habari na Watanzania waishio Marekani.
Pia wafadhili na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za uhifadhi kama TANAPA, NCAA, TTB, TAWA, TFS na makundi ya wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Tanzania wakiwakilishwa na CTI, TBA, TPSF, TATO na CEOrt wahudhuria.
Shughuli hiyo inaoneshwa mubashara kupitia televisheni za Marekani kwenye mfumo wa utangazaji wa umma (PBS) kupitia kituo cha televisheni cha WTTS yenye watazamaji takribani milioni 3.5 na baadaye makala hayo itaoneshwa kwenye zaidi ya chaneli 300 zinazowafikia takribani asilimia 86 ya Wamarekani.
Makala hayo yatazinduliwa pia jijini Los Angeles, Aprili 21, mwaka huu na baada ya matukio hayo mawili, filamu hiyo pia itarushwa kwenye mtandao wa kidijitali wa Amazon na Apple TV.
Kwa Tanzania, filamu hiyo itazinduliwa kwanza jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili na baadaye visiwani Zanzibar tarehe 7 Mei.
Taarifa zaidi soma;
Uzinduzi wafanyika New York
Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour umefanyika usiku wa kuamkia leo Aprili 19, 2022 Jijini New York Nchini Marekani na kuhudhuriwa na watu wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.
Filamu hiyo maalumu ilitengenezwa kwa mwaka mzima ikimshirikisha Rais Samia kama mhusika mkuu akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii #Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na zaidi ya watu 400 katika Jumba la Makumbusho la Guggenheim, baadhi ya waliohudhuria ni wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, wanasiasa, mashirika ya kimataifa.
View attachment 2192524View attachment 2192525View attachment 2192528
View attachment 2192538
Paskali
DSM
Tanzania
Na ndio point yangu ilipo mkuu.Huwezi jitesa uzalendo halafu wenzako wanatafuna tuHisia za uzalendo waliziharibu mboga mboga ikawa ni taifa la wanufaika wachache huo uzalendo utatoka wapi?
Mkuu Kambi ya Fisi , tuna tatizo kidogo kwenye eneo la upashanaji habari. Safari ya Marekani sio tuu ni kuzindua filamu, bali kila mwezi April ya kila mwaka ndio muda wa vikao vya maamuzi vya wakubwa wakubwa wa pesa Duniani, yaani IMF, IFC na WB, hivyo Mawaziri wa fedha wa dunia na Magavana wanakutana kudefend maombi ya mikopo, marais wa nchi wakiwepo wanatia uzito, hivyo Mama Samia yuko huko kwa mikutano hiyo, hivyo hiyo ratiba imefanywa kuoanishwa tuu.Sijaona sababu ya mama kutumia hela za walipa kodi kwenda kuzindua hiyo filamu huko kwa Biden, hayo ni matumizi mabaya ya kodi.
Mbaya zaidi hata Biden mwenyewe kapotezea huo uzinduzi jicho lake lipo kwa putin tu.
Kwani siku ile hukumuona kavaa t-shirt ya Diaspora akimpokea Mama?USA siyo bongo, hawana sifa za kujulikana na kufahamiana.
Mkuu 'kalunya', nimekusoma mara mbili, lakini bado nashindwa kuelewa hasa lengo lako ni nini na andiko lako hili.Kuna sehemu kuna liboss jinga kweli kweli linajifanya liaminifu linadhibiti halina hata gari linapanda daladala huku linakula kwa mama lishe hovyo Sana linajifanya liaminifu wenzake juu wanaenda kuzila tu bila hata huruma.
Halafu likistaafu masikini litajutia linadhani litazikwa na tuzo.
Unalipa kodi juu wanaenda zila.Then Hakuna hatua zozote zinachukuliwa