New York: Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour Tanzania - Starring Samia Suluhu Hassan, President of The United Republic of Tanzania

New York: Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour Tanzania - Starring Samia Suluhu Hassan, President of The United Republic of Tanzania

Wanabodi,

Niko Standby kuwaletea link ya uzinduzi huu.

====

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo ashiriki kwenye uzinduzi wa makala maalumu iitwayo ‘Royal Tour’ jijini New York nchini Marekani.

Makala hayo maalumu ambayo mchakato wake umefanyika kwa takribani mwaka mzima umemshirikisha moja kwa moja Rais Samia akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii nchini Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.

Uzinduzi huo wa aina yake unahudhuriwa na takribani watu 400 unafanyika kwenye Jumba Mashuhuri la Makumbusho liitwalo Guggenheim kuanzia saa moja na nusu za usiku za Marekani, sawa na saa nane na nusu usiku kwa Afrika Mashariki.

Miongoni mwa washiriki ni pamoja na wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, viongozi wa kisiasa, mashirika ya kimataifa, waandishi wa habari na Watanzania waishio Marekani.

Pia wafadhili na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za uhifadhi kama TANAPA, NCAA, TTB, TAWA, TFS na makundi ya wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Tanzania wakiwakilishwa na CTI, TBA, TPSF, TATO na CEOrt wahudhuria.

Shughuli hiyo inaoneshwa mubashara kupitia televisheni za Marekani kwenye mfumo wa utangazaji wa umma (PBS) kupitia kituo cha televisheni cha WTTS yenye watazamaji takribani milioni 3.5 na baadaye makala hayo itaoneshwa kwenye zaidi ya chaneli 300 zinazowafikia takribani asilimia 86 ya Wamarekani.

Makala hayo yatazinduliwa pia jijini Los Angeles, Aprili 21, mwaka huu na baada ya matukio hayo mawili, filamu hiyo pia itarushwa kwenye mtandao wa kidijitali wa Amazon na Apple TV.

Kwa Tanzania, filamu hiyo itazinduliwa kwanza jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili na baadaye visiwani Zanzibar tarehe 7 Mei.

Taarifa zaidi soma;

Uzinduzi wafanyika New York
Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour umefanyika usiku wa kuamkia leo Aprili 19, 2022 Jijini New York Nchini Marekani na kuhudhuriwa na watu wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.

Filamu hiyo maalumu ilitengenezwa kwa mwaka mzima ikimshirikisha Rais Samia kama mhusika mkuu akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii #Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na zaidi ya watu 400 katika Jumba la Makumbusho la Guggenheim, baadhi ya waliohudhuria ni wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, wanasiasa, mashirika ya kimataifa.

View attachment 2192524View attachment 2192525View attachment 2192528
View attachment 2192558
View attachment 2192538
Paskali
DSM
Tanzania
Unatafuta uteuzi au??unatujazia server humu
 
Sijui hii if ya siku hizi imekuwaje?!. Ingekuwa ni ile JF ya enzi zile, saa hizi ungekuta tuna updates zaidi ya members 10!.
Yaani unamaanisha kati ya hao waalikwa zaidi ya 400, hakuna mwana JF yoyote kutu update!.
P
JF ya sasa hivi imejaa siasa za propaganda za vyama na chuki tu, nothing serious
 
Hata wakiongezeka watalii wengi namna gani, unadhani tutaambulia kitu hapo?
List iliyorudishwa kwenye mfumo ni ile ile iliyokuwepo mpaka mwaka 2015. Ni List hatari kabisa kwa maendeleo ya Nchi.
Kwa issue ya maendeleo, kwa sasa Watanzania tusahau kabisa labda utokee mwujiza wa Mwenyezi Mungu.
 
Kuna sehemu kuna liboss jinga kweli kweli linajifanya liaminifu linadhibiti halina hata gari linapanda daladala huku linakula kwa mama lishe hovyo Sana linajifanya liaminifu wenzake juu wanaenda kuzila tu bila hata huruma.
Halafu likistaafu masikini litajutia linadhani litazikwa na tuzo.
Unalipa kodi juu wanaenda zila.Then Hakuna hatua zozote zinachukuliwa
mangi punguza tamaa ya wizi, utabinuliwa siku moja.

Yaaani unamchukia mtu kwasababu kakudhibiti usiibe
 
Sijaona sababu ya mama kutumia hela za walipa kodi kwenda kuzindua hiyo filamu huko kwa Biden, hayo ni matumizi mabaya ya kodi.

Mbaya zaidi hata Biden mwenyewe kapotezea huo uzinduzi jicho lake lipo kwa putin tu.
 
Mkuu Paskal,usidanganyike na uzalendo katika taifa hili.Trust me hata URUSI akituvamia na kutupiga TZ, bado wa TZ tutamshangilia PUTIN na kufurahia wanajeshi wa SAMIA wanavyopelekewa moto (ambao ni ndugu zetu)
Hisia za uzalendo waliziharibu mboga mboga ikawa ni taifa la wanufaika wachache huo uzalendo utatoka wapi?
 
mangi punguza tamaa ya wizi, utabinuliwa siku moja.

Yaaani unamchukia mtu kwasababu kakudhibiti usiibe
Shida zinaenda liwa wakati chini wakiteseka kukusanya hata kumi awapati.
Uzoefu waliojifanya Kazi kwa3 uaminifu baada ya kustaafu wametupwa jongoo wanajutia bahati
 
CCM bana, mnaitangaza nchi yetu kwa mabeberu ili waje waendelee kutuibia raslimali zetu.
 
Wanabodi,

Niko Standby kuwaletea link ya uzinduzi huu.

====

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo ashiriki kwenye uzinduzi wa makala maalumu iitwayo ‘Royal Tour’ jijini New York nchini Marekani.

Makala hayo maalumu ambayo mchakato wake umefanyika kwa takribani mwaka mzima umemshirikisha moja kwa moja Rais Samia akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii nchini Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.

Uzinduzi huo wa aina yake unahudhuriwa na takribani watu 400 unafanyika kwenye Jumba Mashuhuri la Makumbusho liitwalo Guggenheim kuanzia saa moja na nusu za usiku za Marekani, sawa na saa nane na nusu usiku kwa Afrika Mashariki.

Miongoni mwa washiriki ni pamoja na wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, viongozi wa kisiasa, mashirika ya kimataifa, waandishi wa habari na Watanzania waishio Marekani.

Pia wafadhili na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za uhifadhi kama TANAPA, NCAA, TTB, TAWA, TFS na makundi ya wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Tanzania wakiwakilishwa na CTI, TBA, TPSF, TATO na CEOrt wahudhuria.

Shughuli hiyo inaoneshwa mubashara kupitia televisheni za Marekani kwenye mfumo wa utangazaji wa umma (PBS) kupitia kituo cha televisheni cha WTTS yenye watazamaji takribani milioni 3.5 na baadaye makala hayo itaoneshwa kwenye zaidi ya chaneli 300 zinazowafikia takribani asilimia 86 ya Wamarekani.

Makala hayo yatazinduliwa pia jijini Los Angeles, Aprili 21, mwaka huu na baada ya matukio hayo mawili, filamu hiyo pia itarushwa kwenye mtandao wa kidijitali wa Amazon na Apple TV.

Kwa Tanzania, filamu hiyo itazinduliwa kwanza jijini Dar es Salaam tarehe 28 Aprili na baadaye visiwani Zanzibar tarehe 7 Mei.



Taarifa zaidi soma;

Uzinduzi wafanyika New York
Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour umefanyika usiku wa kuamkia leo Aprili 19, 2022 Jijini New York Nchini Marekani na kuhudhuriwa na watu wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.

Filamu hiyo maalumu ilitengenezwa kwa mwaka mzima ikimshirikisha Rais Samia kama mhusika mkuu akiwa katika vivutio mbalimbali vya utalii #Tanzania kwa lengo la kuongeza watalii na kuvutia wawekezaji.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na zaidi ya watu 400 katika Jumba la Makumbusho la Guggenheim, baadhi ya waliohudhuria ni wakuu wa taasisi za biashara za kimataifa, waongoza utalii wa kimataifa, wanasiasa, mashirika ya kimataifa.

View attachment 2192524View attachment 2192525View attachment 2192528

View attachment 2192538
Paskali
DSM
Tanzania
Channel ten,imeonyeshwa live
 
tushee na hii hapa
1650353209387.png
 
Sijaona sababu ya mama kutumia hela za walipa kodi kwenda kuzindua hiyo filamu huko kwa Biden, hayo ni matumizi mabaya ya kodi.

Mbaya zaidi hata Biden mwenyewe kapotezea huo uzinduzi jicho lake lipo kwa putin tu.
Mkuu Kambi ya Fisi , tuna tatizo kidogo kwenye eneo la upashanaji habari. Safari ya Marekani sio tuu ni kuzindua filamu, bali kila mwezi April ya kila mwaka ndio muda wa vikao vya maamuzi vya wakubwa wakubwa wa pesa Duniani, yaani IMF, IFC na WB, hivyo Mawaziri wa fedha wa dunia na Magavana wanakutana kudefend maombi ya mikopo, marais wa nchi wakiwepo wanatia uzito, hivyo Mama Samia yuko huko kwa mikutano hiyo, hivyo hiyo ratiba imefanywa kuoanishwa tuu.

Na kila mwishoni mwa September na Mwanzoni mwa October, ni kikao cha UNGA, New York inafurika marais, Samia ndani.

Hivyo wewe ungelijua hili wala usingeuliza.
P
 
USA siyo bongo, hawana sifa za kujulikana na kufahamiana.
Kwani siku ile hukumuona kavaa t-shirt ya Diaspora akimpokea Mama?
Shughuli hiyo inamhusu mama, itashangaza sana kama 'diaspora' mtegemewa kama Da Mange atakuwa hatambuliki kabisa na mgeni wake mashuhuri wakati huu!
 
Kuna sehemu kuna liboss jinga kweli kweli linajifanya liaminifu linadhibiti halina hata gari linapanda daladala huku linakula kwa mama lishe hovyo Sana linajifanya liaminifu wenzake juu wanaenda kuzila tu bila hata huruma.
Halafu likistaafu masikini litajutia linadhani litazikwa na tuzo.
Unalipa kodi juu wanaenda zila.Then Hakuna hatua zozote zinachukuliwa
Mkuu 'kalunya', nimekusoma mara mbili, lakini bado nashindwa kuelewa hasa lengo lako ni nini na andiko lako hili.

Unataka na hilo libosi liachane na uaminifu, au siyo? Liache 'kudhibiti' watu wale kwa urefu wa kamba zao!

Umekosea sana kuweka haya mawazo yako katiika andiko langu hapo juu.
Hilo 'libosi' kwangu ni jitu linalostahiri pongezi sana, pamoja na matatizo yanayolikabili.

Kwangu mimi, huyo ndiye mTanzania mzalendo, anayelitakia taifa hili mema, bila ya kujali vishawishi vingi vinavyomkabili.

Kama wewe kweli unasimamia mawazo uliyoyaweka hapa, basi wewe ni mmoja wa maadui wa nchi hii mnaostahili kabisa kunyongwa na kufa.
 
Back
Top Bottom