Ngoma Inogile: Wapangaji sasa kulipa asilimia 10 ya kodi TRA

Ngoma Inogile: Wapangaji sasa kulipa asilimia 10 ya kodi TRA

Mpangaji unatakiwa kuzuia 10% ya kodi unayolipa. Mfano kodi yako kwa mwaka ni 2m unapeleka tra 200,000/- mwneye nyumba unampa 1.8m na ushahidi kuwa umelipa 10% tra.
Kaka wapangaji ndio inaenda kula kwetu hii kodi ilipaswa mwenye nyumba ndio aiwasilishe baada ya kulipwa

Ukikata hii pesa ukifika kwa mwenye nyumba nae atataka pesa yake yoote kwahyo inakula kwa mpangaji

Ni sawa na hii kodi ya jengo inayokatwa kwenye manunuzi ya umeme wenye nyumba karbu wote haiwahusu inakula kwa mpangaji.
 
Kwa mujibu wa Gazeti la Mwananchi kuptitia Ukurasa wake wa Instagram, imeeleza kuwa;

Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imesisitiza wapangaji kuwa wazalendo na kulipia asilimia 10 ya kodi wanazokuwa wakilipa kwa wenyenyumba ili kulipia kodi ya pango.

Akiwa katika mafuzo ya wafanyabiashara juu ya mabadiliko ya sheria ya kodi mwaka 2022 wilayani Bariadi, Ofisa huduma na elimu mkuu kutoka TRA, Eugenia Mkumbo amesema kifungu cha 82(2) (a) cha sheria ya kodi kimefuta msamaha wa kodi kwa wapangaji binafsi hivyo kuwapa mamlaka wapangaji wote kuzuia kodi ya pango katika nyumba binafsi na zile za biashara ili kurahisisha ulipaji na ukusanyaji wa kodi ya pango.

"Kama umepanga chumba kiwe cha biashara au makazi unajukumu la kukata asilimia 10 na kuilipa TRA na mwenye nyumba utampelekea nakala ambayo inaonyesha umelipia kodi utaambatanisha na pesa iliyobaki unampa mwenye nyumba" amesema Eugenia.

My take
Awamu ya sita inazidi kuupiga mwingi na kuleta furaha katika mioyo na nyuso za watanzania, ama kwa hakika watanzania Mungu awape nini tena ? manataka Rais wa aina gani nyie? nchi inasonga mbele kwa kasi Tozo zinajenga nchi ,matumizi yamebanwa , pesa haziibiwi, mafisadi yamebanwa, raha sana

😁😁😁
 
Nyumba za kupanga sio biashara rasmi sana ndio maana wengi hatujui...

Lakini kwa watu wenye fremu, apartments zenye leseni ya biashara huwa wanafanya withholding tax kwa niaba ya wapangaji...

Hivyo wewe mpangaji utaona umetoa kodi yako kama kawaida, lakini mwenye nyumba anarejesha 10% ya serikali huko 'tiaraei'...
Najua hlo kwa upande wa biashara na kinachofanya huko iwe na wepesi ni kwasababu mfanyabiashara anahitaj idhini ya TRA na hatua hyo ya kulpa hyo 10% ni kigezo kimoja wapo

Ila sasa kwa hizi nyumba za makazi naonelea ni vizur mwenye nyumba ndio angehusika.
 
Hiyo ni kwa Waswahili walala hoi weusi tu, apartments za Wahindi/Waarabu/Irani Oysterbay Upanga au Masaki hawatalipa hata shilingi, na wakigusa hapo mwisho wao umewadia, …
Ndugu yangu, hao wanalipa sana. Tena wapangaji wao(mostly expatriates) wako mstari wa mbele kuhakikisha imelipwa. Shida iko kwetu waswahili.
 
Kwani ukiwaambia ulishalipa kodi ya miaka 7 na pesa yote ulimpa mwenye nyumba naye kaitumia, hapo kikokotoo kinasemaje?
Wewe ndio unatakiwa kisheria kuwasilisha hio kodi.
 
Kwa mujibu wa Gazeti la Mwananchi kuptitia Ukurasa wake wa Instagram, imeeleza kuwa;

Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imesisitiza wapangaji kuwa wazalendo na kulipia asilimia 10 ya kodi wanazokuwa wakilipa kwa wenyenyumba ili kulipia kodi ya pango.

Akiwa katika mafuzo ya wafanyabiashara juu ya mabadiliko ya sheria ya kodi mwaka 2022 wilayani Bariadi, Ofisa huduma na elimu mkuu kutoka TRA, Eugenia Mkumbo amesema kifungu cha 82(2) (a) cha sheria ya kodi kimefuta msamaha wa kodi kwa wapangaji binafsi hivyo kuwapa mamlaka wapangaji wote kuzuia kodi ya pango katika nyumba binafsi na zile za biashara ili kurahisisha ulipaji na ukusanyaji wa kodi ya pango.

"Kama umepanga chumba kiwe cha biashara au makazi unajukumu la kukata asilimia 10 na kuilipa TRA na mwenye nyumba utampelekea nakala ambayo inaonyesha umelipia kodi utaambatanisha na pesa iliyobaki unampa mwenye nyumba" amesema Eugenia.

My take
Awamu ya sita inazidi kuupiga mwingi na kuleta furaha katika mioyo na nyuso za watanzania, ama kwa hakika watanzania Mungu awape nini tena ? manataka Rais wa aina gani nyie? nchi inasonga mbele kwa kasi Tozo zinajenga nchi ,matumizi yamebanwa , pesa haziibiwi, mafisadi yamebanwa, raha sana

Nimesoma na kuelewa ila nimehisi watu wengi hawajaelewa

Nilivyoelewa mm ni kwamba kama nimepanga nyumba na huwa natoka kodi kila mwezi lets say laki 2... then natakiwa nianze kulipa na tra sasa means badala ya kumpatia mwenye nyumba laki 2 nitoe laki na themanini na ile elfu 20 ndionikatoe kodi tra na risit nimrejeshee mwenye nyumba..


Ndivyo nilivyoelewa hivyo..

Na sio mbaya kulipa kodi ni muhimu ingawa tunatakiwa kuona impact ya kodi zetu..
 
Hii wala sio mpya wamekuwa wakiichukua kila mtu akienda kukata leseni (issue labda ni vipi kumpata mpangaji wa kuishi na sio biashara)

Anyway tatizo langu ni kwenye hata hizo wanazozikata / walikowa wanazikata / Mikopo wanayotutwisha...., yote hayo hakuna value for money...., Tatizo kubwa sio kwenye ukusanyaji ni matumizi, kwa rasilimali na vivutio wala tusingehitaji kukabana na wananchi (je wasio na rasilimali kama sisi na sisi wenye nazo tuna tofauti gani)
 
Nimekaa nikawaza pamoja na kuumizwa na tozo mbalimbali na sasa kodi hii mpya inayotaka kuanza. Inawezekana ikawa ni kwa ustawi na faida ya nchi yetu zaidi ya kufanya kazi za maendeleo. Nitafafanua.
Watanzania wengi wamekuwa sio walinzi wa mali za umma wakiamini ni za serikali na haziwahusu. Mali nyingi za umma zimekuwa zikihujumiwa sana kwa mfano watu kuiba vyuma kwenye daraja la busisi au kuiba cement kwenye ujenzi wa madarasa au mabarabara. Inawezekana kabisa hii ilisababishwa na misaada na mikopo hivyo watu wakaona vinakuja tu na vingine vitakuja. Nyumba ya kujenga mwenyewe utaidhamini na kuitunza vivyo hivyo kwa gari binafsi uliyoinunua kwa jasho lzm uwe na uchungu nayo. Sasa hoja yangu ni ipi? Hizi tozo na kodi pengine zitabadilisha mtazamo juu ya mali ya umma watu wajue ni ya kwao. Itasaidia watu kuwa wakali wakiona matumizi mabaya ya pesa zao. Itakuwa sio Rais katoa pesa itakuwa ni serikali ya watu imetoa pesa....pesa ni ya serikali......ni ya watu.......tunaumia lkn mentality zitabadilika na kuanza kuwa wafuatiliaji wazuri wa miradi ya maendeleo na kujali mali ya umma. Adios...
 
Mpangaji unatakiwa kuzuia 10% ya kodi unayolipa. Mfano kodi yako kwa mwaka ni 2m unapeleka tra 200,000/- mwneye nyumba unampa 1.8m na ushahidi kuwa umelipa 10% tra.
Mwenye nyumba hatokubali
 
Bora mpitie kwenye umeme ila kwa live bila chenga mtaisoma namba
Nyumba iko kinondoni mfano
Kodi kwa mwezi Ana charge 700,000×12=8,400,000/ kwa mwaka

Kodi ya jengo kwa mwaka analipa 10000/ hapo

Ova
 
Nyumba za kupanga sio biashara rasmi sana ndio maana wengi hatujui...

Lakini kwa watu wenye fremu, apartments zenye leseni ya biashara huwa wanafanya withholding tax kwa niaba ya wapangaji...

Hivyo wewe mpangaji utaona umetoa kodi yako kama kawaida, lakini mwenye nyumba anarejesha 10% ya serikali huko 'tiaraei'...
Wenye apartment wote wanalipia hiyo
Na hata nyumba kama umuiweka kibiashara lazima ulipe
Sema wengi wanakausha hawalipi

Ova
 
Nimekaa nikawaza pamoja na kuumizwa na tozo mbalimbali na sasa kodi hii mpya inayotaka kuanza. Inawezekana ikawa ni kwa ustawi na faida ya nchi yetu zaidi ya kufanya kazi za maendeleo. Nitafafanua.
Watanzania wengi wamekuwa sio walinzi wa mali za umma wakiamini ni za serikali na haziwahusu. Mali nyingi za umma zimekuwa zikihujumiwa sana kwa mfano watu kuiba vyuma kwenye daraja la busisi au kuiba cement kwenye ujenzi wa madarasa au mabarabara. Inawezekana kabisa hii ilisababishwa na misaada na mikopo hivyo watu wakaona vinakuja tu na vingine vitakuja. Nyumba ya kujenga mwenyewe utaidhamini na kuitunza vivyo hivyo kwa gari binafsi uliyoinunua kwa jasho lzm uwe na uchungu nayo. Sasa hoja yangu ni ipi? Hizi tozo na kodi pengine zitabadilisha mtazamo juu ya mali ya umma watu wajue ni ya kwao. Itasaidia watu kuwa wakali wakiona matumizi mabaya ya pesa zao. Itakuwa sio Rais katoa pesa itakuwa ni serikali ya watu imetoa pesa....pesa ni ya serikali......ni ya watu.......tunaumia lkn mentality zitabadilika na kuanza kuwa wafuatiliaji wazuri wa miradi ya maendeleo na kujali mali ya umma. Adios...
Wananchi wanasahau kuwa nchi zinaendelea kwasababu ya kodi. Hatutakiwi kugomea kodi, tunatakiwa kupaza sauti kodi zetu zitumike vizuri kwa maendeleo yetu.
 
Ahahahahah kwahio kama kodi ni laki 6 unazuia elfu 60 au sio? 😂😂😂 wacha nijiandae kuhamia burundi sasa. Maana sahizi sehemu za kulala zimegeuzwa fremu za biashara

Wanaokaa bure kwa takrima nao itakuwa je?
 
Back
Top Bottom