Ngongo anatarajiwa kufika mbele ya kikosi kazi wakati wowote kuanzia kesho

Ngongo anatarajiwa kufika mbele ya kikosi kazi wakati wowote kuanzia kesho

Kama kuna jambo la muhimu kuliko hili, sijui jambo hilo ni lipi!

Mkuu 'Monk', ninakukumbuka sana katika mikwaruzano yetu humu JF, lakini hili hapa naondoa kofia na kuonyesha kipara mbele zako. Hongera sana!

Hata kama siyo mipango ya taifa ya miaka hamsini/hamsini; ishirini hadi thelathini inatosha kama kweli serikali zitalazimika na kuwajibika kutimiza mipango hiyo kikamilifu katika muda uliopangwa.
Na kama kuna dharura, basi patakuwepo na utaratibu mahsusi utakaotumika kuchepuka bila kuathiri malengo ya mwanzo.

Ahsante Kwa kuwa muungwana ndugu yangu, kama binadam inatokea kutofautisha, ila kuziweka kando tofauti zetu na kuendelea na maisha ndio kunaleta thamani ya utu.

Nashukuru pia Kwa kuongeza mfumo wa kupitia mwenendo wa utekelezaji wa huo mpango wa maendeleo. Hata kama Kuna mabadiliko au Kuna dharura, katiba inakua imeweka wazi ni namba Gani Hilo jambo litashughulikiwa.

Hii Kila Rais au awamu kuja na ilani yake haitatufikisha popote, ni upotevu wa rasirimali za taifa.

Lakini muhimu zaidi, itaongeza uwajibikaji Kwa viongozi wetu. Mtu ambae hawezi kuonyesha katika kipindi alichokua kwenye nafasi yake hatoweza kuthubutu kutaka kuendelea Tena. Na anaetaka kjiingiza huko, atajitafakari na kujipima kama anaweza kupelekea mbele utekelezaji wa huo mpango.

Uwe na wakati mwema mkuu
 
Akili huna
Tanganyika na Zanzibar zinakuwa nchi moja au mbili kwenye muungano?

Kwanini usitoe ya moyoni Kwa staha mkuu?
Jamaa ameweka bayana, haya ndio yanamfurukuta hawezi kupata usingizi Wala kutulia Hadi akayatoe mbele ya kikosi kazi. Amesisitiza mengine wataongezea wengine.

Muundo wa Muungano ni miongoni mwa mengine ambayo wewe unaweza kutaelezea. Kumbuka Zanzibar Wana serikali Yao na katiba Yao, kwanini usitoe maoni Yako kuhusu Hilo swali lako badala ya kumshambulia mleta mada?
 
Napendekeza mikataba yote itakayohusu rasilimali za nchi lazima ipite bungeni na wananchi wajulishwe.

Hapo kwenye bunge ndio mushkeli wangu unapoanzia, ukiangalia uwekezaji na fedha inapotea kuhudumia bunge na thamani tunayoipata kama taifa, ni biashara kichaa kama haliwezi kuboreshwa kuisomamia serikali, halina tija. Bora kuwa na kamati za wataalam walioajiriwa na wanapata hizo nafasi Kwa ushindani.

Mikataba itapitiwa na wataalam, wakihusisha mwanasheria mkuu wa serikali.
 
Kaseme tena Chama kikitoa ahadi za uchaguzi kiitekeleze kwa 90+. Kisipotekeleza kifutwe maana tunadanganywa sana
 
Pendekezo Moja liwasilishe pia, watahakikisha vipi hii katiba mpya haikiukwi/ kusiginwa kama ilivyo ya Sasa?

Kuwa na katiba nzuri ni jambo Moja, utekelezaji ilete tija ni jambo lingine.

Binafsi sioni umuhimu wa bunge kabisa, ni kitu tumerithi tu au tumeiga Kwa wengine. Tunahitaji kamati yenye wabobezi wa mambo ya sheria kusimamia mchakato wa mambo ya kisheria.

Uwaziri uwe ni nafasi ya kitaalam. Unaomba kuwa waziri wa Nishati, vigezo vinaangaliwa, mnashindanishwa na unaeleza kwanini upewe hiyo nafasi. Inakua ni kazi ya mkataba unaongezewa muda Kwa kadri unavyotekeleza Kwa ufanisi majukumu Yako kulingana na matarajio na malengo mliyojiwekea. Kwanza hapa tunaweza kuwa na Wakurugenzi na makaribu wakuu tu. Waziri wanini? Tunaongea gharama tu.

Waruhusu wagonbwa huru wasiokua na chama.

Mwisho, tuwe na mpango wa maendeleo wa miaka hamsini ambao ndio unaongoza jitihada, juhudi na nguvu zetu zote kuutekeleza kama taifa, viongozi wote akiwepo Rais, watapimwa Kwa namna wanavyotekeleza huo mpango. Haitajalisha chama Gani kinashoka Dola, ili kibaki madarakani ni lazima kithibitishe na kuweza kuleta mabadiliko kadri ya mpango wa taifa unavyoongoza.
Nchi gani uliwahi kuiona ina mpango wa maendeleo wa miaka 50?
 
Nchi gani uliwahi kuiona ina mpango wa maendeleo wa miaka 50?
Sasa hayo si maoni yangu? Weka Yako hapa. Pia Kuna post inayofuatia nimeeleza kuwa na Chombo Cha kuratibu mwenendo wa utekelezaji na kuona kama mabadiliko yanahitajika kutokana na mahitaji. Hatuwezi kuwa tunachezea rasirimali kisa ilani ya chama au mawazo ya Kiongozi anayeingia madarakani.

Mwisho wa siku sio Kila jambo lazima lifanane nchi zote, ndio maana tumejitumbukiza kwenye gharama zisizo na ulazima kisa tunataka kuwa kama wengine, tunadonoadonoa tunapoona Kuna unafuu wakati huko wanapofanya hivyo ni mfumo kamili unaotegemeana.

Mbona sie kesi ya uchaguzi ya matokeo ya Rais haiendi mahakamani wakati nchi zingine ni jambo la kawaida?

Pia kwanini ukomo wa rais uwe miaka kumi? Kwanini isiwe mitano tu au ikawa zaidi kama anafanya mambo ya kulinufaisha taifa na wananchi Kwa ujumla?
 
Back
Top Bottom