Kigoma Region Tanzania
JF-Expert Member
- May 25, 2021
- 230
- 611
Ngorongojo ni usafiri uliokuwa ukitumika enzi za nyuma na hadi hivi sasa hapa mkoani Kigoma. Ngorongojo huundwa kwa miti migumu, hivyo mchakato wake wa utengenezaji unaanzia maporini ambapo ni lazima kwenda kutafuta miti migumu kwenye mapori.
Ngorongojo ina mpini "kishikio" ambapo hutegemea kupakwa mafuta ya mawese ili kuwezesha kuteleza na kukimbia kwa kasi zaidi. Mara nyingi huwa hazina breki, na nirahisi kukurusha na kukuacha na makovu kama sio kukutoa meno, (Ukiumia na ngorongojo unatakiwa kuficha makovu usifahamike nyumbani). Kusimama kwake hutegemea muinuko wa mlima, kwani Ngorongojo husaidia kwenye safari za maporomoko na mishuko.
Ngorogojo zingine huwekewa breki kwa kutumia kipande cha gamba la tairi ya gari au baiskeli ambapo ili usimame unabidi kukanyaga mzunguko huo wa tairi. Hivi sasa usafiri huu muhimu umekuwa adimu tofauti na enzi za nyuma.
Usafiri huu unaundwa kwa kutumia miti, na ndio chanzo kikuu cha kamptula za watoto kuchanika makalioni, ngorongojo inaongoza kwa kumaliza kamptula.
Huu ni ubunifu wa watoto wa Kigoma zinaitwa baiskeli za asili au ngorogojo ni katika hatua za makuzi ya kijana, gharama za kununua ngorongojo kwa asiyeweza kutengeneza ilikuwa ni kati ya Tsh 150 hadi 250 kipindi hicho. Kuikodisha ilikuwa ni kati ya Tsh 5 hadi Tsh 50.
Ngorongojo ina mpini "kishikio" ambapo hutegemea kupakwa mafuta ya mawese ili kuwezesha kuteleza na kukimbia kwa kasi zaidi. Mara nyingi huwa hazina breki, na nirahisi kukurusha na kukuacha na makovu kama sio kukutoa meno, (Ukiumia na ngorongojo unatakiwa kuficha makovu usifahamike nyumbani). Kusimama kwake hutegemea muinuko wa mlima, kwani Ngorongojo husaidia kwenye safari za maporomoko na mishuko.
Ngorogojo zingine huwekewa breki kwa kutumia kipande cha gamba la tairi ya gari au baiskeli ambapo ili usimame unabidi kukanyaga mzunguko huo wa tairi. Hivi sasa usafiri huu muhimu umekuwa adimu tofauti na enzi za nyuma.
Usafiri huu unaundwa kwa kutumia miti, na ndio chanzo kikuu cha kamptula za watoto kuchanika makalioni, ngorongojo inaongoza kwa kumaliza kamptula.
Huu ni ubunifu wa watoto wa Kigoma zinaitwa baiskeli za asili au ngorogojo ni katika hatua za makuzi ya kijana, gharama za kununua ngorongojo kwa asiyeweza kutengeneza ilikuwa ni kati ya Tsh 150 hadi 250 kipindi hicho. Kuikodisha ilikuwa ni kati ya Tsh 5 hadi Tsh 50.