Ngorongoro hatarini kupoteza uhai na umaarufu wake kutokana na kukithiri kwa shughuli za binadamu

Ngorongoro hatarini kupoteza uhai na umaarufu wake kutokana na kukithiri kwa shughuli za binadamu

Watu wanaishi katika eneo walilochagua kuishi zamani sana kabla ya ukoloni. Kabla ya ukoloni hakukuwepo na hifadhi.
Waacheni watu waishi na wanyama kama walivyozoea.
Kama hamtaki kuona kondoo na mbuzi, mkatembee Kisutu, Upanga, Kivukoni na Oysterbay.
Walikuwa wangapi ?, na walikuwa wanaishi kama part ya ecosystem na viumbe wengine au walikuwa wanaishi kama sasa kwa kuharibu mazingira na kuwafanya hao viumbe wengine watoweke / kupotea ?

Hili sio tatizo la Tanzania tu, ni tatizo la kidunia..., sababu tumeshindwa kuishi kwa kutegemeana na mazingira yetu its just a matter of time kabla hatujapay the price (ingawa tumeshaanza kufanya hivyo)

“When the last tree has been cut down, the last fish caught, the last river poisoned, only then will we realise that one cannot eat money,”

By the way huo ulikuwa ni msemo wa wahenga fulani kabla ya ukoloni....
 
Ata kama uliishi kabla ya dunia kuumbwa serikali inaweza kuamua kupanga wakazi wake upya.kwasababu ni wajibu wa serikali kuhudumia mambo ya msingi ya wananchi wake.huduma kama mashule,hospital na miundombinu mbali mbali ni wajibu waserikali na inapobidi kuhamisha wakazi flani kwa ajili ya rasilimali za nchi inaweza kufanya ivyo pia.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Hakuna kitu kama hicho. Wakiondolewa wamaasai pale basi Ngorongoro itakuwa na hadhi sawa na pori la akiba la Maswa tu basi.
Unadhani umaarufu wa Ngorongoro ni wanyama tu? Mbona Selous, Mikumi, Tarangire na Manyara zina wanyama lkn hazina umaarufu wa Ngorongoro?
 
Mwaka 1959 Wamaasai waliondolewa kwenye plains za Serengeti na serikali ya wakati huo. Na makubaliano mojawapo ni kubaki kwenye mfumo mzima wa Ngorongoro.
Mifugo inayofugwa na Wamaasai haina madhara kwa wanyamapori.
 
Hakuna kitu kama hicho. Wakiondolewa wamaasai pale basi Ngorongoro itakuwa na hadhi sawa na pori la akiba la Maswa tu basi.
Unadhani umaarufu wa Ngorongoro ni wanyama tu? Mbona Selous, Mikumi, Tarangire na Manyara zina wanyama lkn hazina umaarufu wa Ngorongoro?
Serengeti nayo inawatu!?
 
Mwaka 1959 Wamaasai waliondolewa kwenye plains za Serengeti na serikali ya wakati huo. Na makubaliano mojawapo ni kubaki kwenye mfumo mzima wa Ngorongoro.
Mifugo inayofugwa na Wamaasai haina madhara kwa wanyamapori.
Aidha hujafuatilia au umeamua kuwa biased.
Ile mifugo inapeleka maradhi kutoka kwa mifugo ya kufugwa mpaka kwa wanyapori.
Watu wanaongezeka kila uchao pale Ngorongoro ni kweli hawezi kuishi nje ya Ngorongoro
na maisha yakaendelea!?
 
Aidha hujafuatilia au umeamua kuwa biased.
Ile mifugo inapeleka maradhi kutoka kwa mifugo ya kufugwa mpaka kwa wanyapori.
Watu wanaongezeka kila uchao pale Ngorongoro ni kweli hawezi kuishi nje ya Ngorongoro
na maisha yakaendelea!?
Ndio akili yako ilipoishia? Hayo magonjwa ya wanyama wafugwao yanatoka kwa binadamu? Mbona pointi yako haina maana.
Wanyama pori ndio wanaambukiza magonjwa kwa wanyama wafugwao kwa wingi. Acha ujinga.
Ninyi mnajisikiaje mkiambiwa mhame Same, Makanya na Hedaru, kisa kuna wanyama wa Mkomazi. Hifadhi ndio iliwafuata Wamaasai.
 
Ndio akili yako ilipoishia? Hayo magonjwa ya wanyama wafugwao yanatoka kwa binadamu? Mbona pointi yako haina maana.
Wanyama pori ndio wanaambukiza magonjwa kwa wanyama wafugwao kwa wingi. Acha ujinga.
Ninyi mnajisikiaje mkiambiwa mhame Same, Makanya na Hedaru, kisa kuna wanyama wa Mkomazi. Hifadhi ndio iliwafuata Wamaasai.
Hivi huelewi hata maaradhi yanayo wapata binadamu yanaweza wapata wanyama?
waliposema ukimwi umetokea kwa nyani ulikuwa hujazaliwa?
Hamna namna mtahama tu huko...
Maisha bila ngorongoro hamyawezi ama!?
Uoto wa asili wa kila siku unalalamikiwa kutoweka nyie hamtaki kuhama tu hameni kwa hiari
kabla shuruti haijaanza.
Watu wanahama kupisha migodi, wawekezaji ije kuwa urithi wa dunia?
 
Shame,
Nimeona mtalii Richard Branson billionaire muingereza, akizungukia mlima Kilimanjaro na hot air balloon, IPO kwenye page yake ya Instagram,

Sisi huku Ngorongoro tumeigeuza Machinga na machungaji complex, shaabaashhh!

Watakuja kweli kuangalia full suti za mabati, ng'ombe, mbuzi na kondoo?

TANAPA NGORONGORO CONSERVATION wanakula miposho Tu ya vikao!
 
Hivi huelewi hata maaradhi yanayo wapata binadamu yanaweza wapata wanyama?
waliposema ukimwi umetokea kwa nyani ulikuwa hujazaliwa?
Hamna namna mtahama tu huko...
Maisha bila ngorongoro hamyawezi ama!?
Uoto wa asili wa kila siku unalalamikiwa kutoweka nyie hamtaki kuhama tu hameni kwa hiari
kabla shuruti haijaanza.
Watu wanahama kupisha migodi, wawekezaji ije kuwa urithi wa dunia?
Tuhame kwenda wapi? Hatuondoki. Hatuhami. Utaendelea kuota hivyo lkn hatuhami. Acheni ujinga bana.
 
HATARI NGORONGORO
- Siku za uhai wa Hifadhi ya Taifa hiyo yenye sifa za kipekee Duniuani zinahesabika

- hali ya muingiliano wa shughuli za binaadamu, mifugo, uhifadhi na utalii yazidi kuwa mbaya

- Makundi ya Mifugo mamia kwa maelfu yatanda kila kona ya hifadhi, magari ya watalii yapishana na Ng’ombe na kondoo barabarani badala ya Wanyama pori

- Matajiri wajenga majumba ya kifahari Hifadhini kinyume cha sheria iliyounda hifadhi hiyo huku wakitumia neno umasikini kama kinga

- Mabilioni ya shilingi yatengwa na asasi kutoka nchi jirani kuhakikisha hifadhi hiyo inapoteza umashuhuli wake



Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro ipo hatarini kupotea na kupoteza uhai na umashughuli wake kutokana nna kukithiri kwa shughuli za kibinaadamu ikiwemo ufugaji uliopitiliza kiasi, ujenzi wa nyumba zisizofuata taratibu za kihifadhi na shughuli nyingine za kibiashara

Mwaandishi wa habari hizi ameshuhudia bmakundi makubwa ya mifugo ikiwemo Ng’ombe, mbuzi, kondoo, punda, kuku, na mingineyo ikichukua eneo kubwa kuliko Wanyama wa asili wanaopendwa kufuatiliwa na watalii

Pamoja na kuzingatia ukweli kuwa Ngorongoro ni hifadhi ni hifadhi ya kipekee inayowahusisha Wanyama binaadamu na mifugo kwa pamoja lakini hali ilivyo kwa sasa inatisha kiasi cha kutishia usalama wa hifadhi na wananchi husika wa asili wanaoishi katika eneo hilo

Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili imezitafiti ni kuwa mwaka 1959 wakati wakazi walioruhusiwa kuishi katika hifadhi hiyo kwa mchanganyiko wao na Wanyama pori, wakazi hao hawakuzidi watu elfu 9 tofauti na sasa wakazi hao wamefika zaidi ya laki moja na mifugo yao bwanayoimiliki ikikadiriwa kuwa zaidi ya laki6

‘’kwa mujibu wa taarifa wanasema kuna mifugo laki 2 na nusu, nadiriki kusema sio kweli, mifugo hii haipungui haipungui laki saba hadi laki nane…hebu angalia tangu tumeanza kuanza makundi ya ng’ombe, mbuzi na kondoo sasa hivi ni zaidi ya masaa mawili tunazunguka tunawaona tu…hii maana yake kuwa hata kama watu hawa wapo kisheria lakini inahitajika jitihada za makusudi kunusuru tatizo hili…hili ni tatizo kwa kweli’’. Alisema Paul Schenzern Raia wa ujerumani aliyekuwa katika safari za kitalii

Schezern ameongeza kuwa kwao wanavyoifahamu Ngorongoro nin kuwa eneo bora zaidi la kiutalii na kamwe hakuwaza kama angepita barabani akipishana na ng’ombe na mifugo mingine japokuwa alikuwa anaufahamu kuwa Ngorongoro wanaishi binaadamu na Wanyama lakini si kwa kiwango alichokiona

‘’nimetembea hifadhi kadhaa Duniani ambazo Wanyama na binaadamu wanaishi kwa asili, kwa kweli zinavutia n ahata kuishi kwao kunaemndana na uhifadhi wa mazingira, tofauti na hapa Ngorongoro…ntapata shida san akumshawishi mtu atakayeniomba ushauri juu ya kutaka kuja hapa. Nafikiri watetezi wa haki za binaadamu, mifugo, Wanyama na mazingira wanapaswa kupaza sauti ya pamoja kuinusuru hifadhi hii muhimu na bora’’. aliongezq

‘’unajua watu wanaweza kulalamika kwamba wanaishi humu na haipaswi kupangwa vizuri, lakini sio sahihi watetezi makini wa binaadamu wanatakiwa watetee kwanza usalama wa mazingira, usalama wa mazingira ya Ngorongoro ndio usalama wa Arusha, usalama wa Arusha ndio usalama wa Tanzania na ndio maana Dunia nzima kunakuwa na sheria kali zinazolinda mazingira…..kujazana kwa watu na mifugo hifadhini sio haifai tu kwa mifugo bali haifai zaidi kwa binaadamu wanaoishi nhumo kwani kuishi kwao kunategemea zaidi ikolojia nya hifadhi husika’’. Alisema Habibu Mchange, Mratibu wa mtandao wa wanahabari wanarasilimali asilia na taarifa alipoombwa kutoa maoni yake

Mchange alisema kuwa hata yeye alikuwa Ngorongoro mwishoni mwa mwaka jana na ameshuhudia ujenzi uliokithiri na unaovunja kabisa sheria na kanuni za uhifadhi na kuongeza kuwa anaandaa ziara ya wanahabari wanarasilimali asilia na taarifa kwenda kujionea hali ilivyo na kuuhabarisha umma na kuwataka wanaharakati kushirikiana kuokoa kivutio hicho muhimu

‘’hata mimi nilitembbea tembea mwishoni mwa mwaka, niliyoyaona Ngorongoro kwa kweli yanatisha na hayafai kusimuliwa hata kidogo, wadau nwa utalii, uhiofadhi na mazingira tusipochukua hatua na kupaza sauti, Ngorongoro itapotea kama upepo…..kwa kifupi tu nikuambie ndugu mwandishi kuwa NGORONGORO IPO HATARINI KUPOTEA’’. Aliongeza Mratibu Mchange

Taarifa na uchunguzi zaidi kuhusu kuharibika kwa ikolojia Ngorongoro na mitazamo ya wahusika wa pande zote muhimu tutawaletea katika matoleo ya siku zijazo
Acha wivu, baba ako angekuwa na mifugo humo ungeandika?
 
Baadhi ya Picha za hifadhi ya ngororo zinazoonyesha namna muingiliano baina ya watu, mifugo na shughuli nyingine za kibinaadamu ikiwemo ujenzi zinavyoathiri Ikolojia na uhifadhi. Hatua muhimu na za haraka zinapaswa kuchukuliwa kuikoa hifadhi hii bila kuathiri maisha ya wenyeji wa asili.View attachment 2095940View attachment 2095943View attachment 2095941View attachment 2095942View attachment 2095944View attachment 2095945View attachment 2095946View attachment 2095947
Acha kutumika na CCM kwa nia ovu
 
Kwa akili tu za kawaida iko wazi kua hiyo hifadhi baada ya miaka kadhaa mbele haitakua tena hifadhi.na hilo kosa lilifanywa na serikali yenyewe kuendekeza siasa zaidi badala yakuweka sera na mikakati madhubuti kwaajili ya rasilimali za nchi.kama serikali haitafanya maamuzi magumu yakunusuru ilo eneo hali itakua mbaya zaidi uko mbele,hili lakutaka kushikilia vyote kwa pamoja nikitu ambacho kamwe hakitawezekana.Ningekua mimi ndiye rais wa nchi ningefanya maamuzi magumu yafuatayo,(1)Ningetafuta eneo jingine la malisho la hao wananchi waliopo ndani ya hifadhi kwasababu hii nchi bado ni kubwa na bado kuna maeneo mengi sana(2)Ningetenga pesa za fidia kwa wananchi hao(3)Ningetoa muda wawao kuhamia eneo jipya kwa utaratibu wa serikali baada ya hapo ningepitisha operesheni yakijeshi yakusafisha eneo lote la hifadhi(4)Ningevunja mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro na kuiunganisha na TANAPA na eneo la hifadhi ningeliunganisha na hifadhi ya serengeti nakutengeneza hifadhi moja matata sana duniani.ningehakikisha inakua hifadhi moja yakisasa ambayo dunia nzima ingehamia kuja kuitembelea.Ningehakikisha kwa kipindi cha miaka mitano pesa ambayo ningekusanya hapo ingekua haielezeki.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Hifadhi yenyewe inatusaidia nini zaidi ya watawala kugawana pesa?
 
Lakini wajue tu kwamba wanatafuta crisis ambayo haijawahi kutokea.
 
Pendo lyimo nimeona picha moja lakini kama nakumbuka hapo ni makao ambapo kuna ishi watu na sio crater.
Hifadhi inayo shida nakumbuka 2004-2005 kulikuwa na mkakati wa kupunguza idadi ya magari na watu yanayoingia kwa wakati mmmoja.Eidhaa ingekuwa kwa zamu au kwa siku idadi maalum.Pia mkakati mwingine ikawa wanawatoa staff wanaoishi makao ili wawe wanatoka karatu kwenda ngorongoro kila siku na jioni wanarudi karatu.
Mkakati huo pia ulilenga na wafanyakazi wa mahotelini lakini ikawa ni ngumu kwa sababu wageni wanaolala kwenye mahoteli ndani ya Hifadhi watataka huduma za usafi na chakula kwa hiyo ikawa kuna kipengele
Hoteli kipindi hicho zilikuwa Serena,CCA Africa (Conscorp)Ngorongoro Crater Lodge)Wildlife Lodge, Baadaye ikaja Rhino.Kwa hiyo hapo kuna wafanyakazi ambao lazima waishi ndani ya Mgodi!
Kwa hiyo Wafanyakazi wa Hifadhi wametolewa nje wengi wanaishi karatu nje ya mji kidogo kuna Maghorofa yao pale karibu na barabara!Waliona wafanyakazi wa Hotelini italazimu watoke alfajiri kwenda hifadhini na wakahofia ajali za magari pamoja na wanyama kugongwa!Hifadhi kuwa safi ki ecologia ni watu kutoka au kupungua na magari ipangwe idadi kwa siku.
Hali ya sasa ni mbaya mbaya mbaya sana.
 
Back
Top Bottom