TANZIA Nguli wa Soka Duniani, Mbrazili Pele afariki dunia

TANZIA Nguli wa Soka Duniani, Mbrazili Pele afariki dunia

View attachment 2462793
giphy.gif
Alikuwa bado ana agent?au agent huwa ana kazi nyie wanasoka mnijuze.
 
View attachment 2462887
Mnamo 1977, vyombo vya habari vya Brazil viliripoti kwamba Pele alitolewa figo yake ya kulia.

Mnamo Novemba 2012, Pele alifanyiwa upasuaji wa nyonga. Mnamo Desemba 2017, Pelé alionekana kwenye kiti cha magurudumu kwenye droo ya Kombe la Dunia la 2018 huko Moscow ambapo alipigwa picha akiwa na Rais wa Urusi Vladimir Putin na Diego Maradona.
View attachment 2462888
Mwezi mmoja baadaye, alianguka kutokana na uchovu na kupelekwa hospitali.

Mnamo 2019, baada ya kulazwa hospitalini kwa sababu ya maambukizi ya njia ya mkojo, Pele alifanyiwa upasuaji wa kuondoa mawe kwenye figo.

Mnamo Februari 2020, mwanawe Edinho aliripoti kwamba Pelé hakuweza kutembea kwa kujitegemea na kusita kuondoka nyumbani, akihusisha hali yake na ukosefu wa ukarabati kufuatia upasuaji wake wa nyonga.

Mnamo Septemba 2021, Pele alifanyiwa upasuaji wa kuondoa uvimbe upande wa kulia wa koloni yake.

Ingawa binti yake mkubwa Kely alisema "anaendelea vyema", inasemekana alirudishwa kwenye uangalizi maalum siku chache baadaye, kabla ya kuachiliwa mnamo 30 Septemba 2021 ili kuanza matibabu ya kemikali.

Mnamo Novemba 2022, ESPN Brasil iliripoti kwamba Pelé alikuwa amepelekwa hospitalini akiwa na "uvimbe wa jumla", pamoja na masuala ya moyo na wasiwasi kwamba matibabu yake ya kidini hayakuwa na athari inayotarajiwa; binti yake Kely alisema "hakukuwa na dharura".

Mnamo Desemba 2022, Hospitali ya Albert Einstein ambako Pelé alikuwa akitibiwa, ilisema kwamba uvimbe wake ulikuwa umeongezeka na alihitaji "huduma zaidi inayohusiana na matatizo ya figo na moyo".

Alikufa hospitalini kutokana na kushindwa kwa viungo vingi, tatizo la saratani ya utumbo mpana, tarehe 29 Desemba 2022, akiwa na umri wa miaka 82.
Matibabu ya kidini yanakuwaje?
 
tatizo huko anakoenda sasa! hawaujui mpira wanataka ibada! huku ameondoka shujaa ila sasa kisago atakacho kumbana nacho huko! amewafanya waache kwenda kusali washinde kutwa kwenye luninga wakiangalia pasi na tobo za maudhi ,mungu anauchukia sana mpira,nikama sanamu yenye nguvu sana kwa sasa hapa duniani namuonea huruma maana jehanum ndio mahala pake!
Mungu anauchukia mpira?kivipi?na hii ni kwa imani ya upande upi?
 
Pumzika kwa amani mwamba wa Soka,umefanya kazi iliyotukuka duniani kwa upande wa Soka.
 
yule ni nguli wa soka duniani, wapenda soka wanafuatilia rekodi zake, vyombo vya habari duniani vinamuandikaje baada ya kuondoka duaniani. Kama si mshabiki wa mpira wa miguu hutamuelewa Pele alikuwa nani kwenye ulimwengu wa soka

Mimi nawaelewa only Messi na Diego Armando,usipowaelewa hawa basi wewe sio mwanamichezo..
 
Waislam bana[emoji23] mnapenda sana kuchangiwa changiwa, si mtoe sadaka za kutosha na kuweka vitega uchumi mjijengee wenyewe?

Gadaffi na wengine kawajengeeni, bado mnataka na Pele awajengee???

Poor you.
Sasa madrasa Pele yanamhusu nini? Waislam jamani!!
 
Mimi nawaelewa only Messi na Diego Armando,usipowaelewa hawa basi wewe sio mwanamichezo..
Ukiwataja hawa huwezi kumuacha Pele katika ubora wake. Messi ni wa kizazi hiki cha soka na Pele alikuwa wa kizazi chake, kwa hiyo hao wote ni kitu kimoja katika ulimwengu wa soka
 
Ni kweli mkuu, Wala hukudanganywa. Na Kuna mengine mengi tu hujasimuliwa yote
Alishawahi kupiga shuti likagonga mwamba juu mpaka bomba ikakatika vipande viwili
 
Back
Top Bottom