Nimekuelewa vema kabisa. Si sahihi kuwapa polisi ruhusa ya kuua maana wataua waliomo na wasiokuwemo. Si sahihi kupewa ruhusa ya kuua!Saizi baada ya Panya road kuua raia wengi wa wananchi wanasupport POLISI wawaue hao watoto.
Wakati njia sahihi ni kuwauliza POLISI kwann hawafanyi doria mitaani au kuhakikisha mifumo imara ya kiulinzi na kiusalama inaimarika ktk JAMII.
Ilikuwa ni wakati sahihi wa JAMII kushinikiza IGP, waziri wa Ulinzi KUJIUZULU, RPC na DED husika.
POLISI wasipewe RUHUSA kuua raia, wachunguze na kuiachia mahakama Kutoa HUKUMU.
Sijui umenielewa???
Hapana, kuna wasiohusika watatajwa kuwakomoa kutokana na chuki binafsi tu. Maana hadi wanathibitishwa kuwa hawana hatia wameshalika sana.Mimi nadhani uanzishwe Uzi maalumu was kuwataja hap Panya road na maeneo yao itasaidia Sana kuwabaini. Kwa polisi kuwaanzisha upepelezi hao washukiwa
Binafsi nawa Nitatoa ushirikiano ktk hili
Kwahyo mtoto wako akienda ua raia wasio na hatia na kuwaibia wewe kama baba unafurahia? Akiua naye auliwe period. Uchungu unaoutaja ndo huo mzazi wa mwingine anaupata sababu ya mtoto wako acheni kutetea upumbavuKesho yake utakuwa na mtoto kama huyo, ngoja tuone kama akipigwa shaba utafurahi kuwa UA maana naye ameua.
All in all, umeandika vizuri ila sweeping action/operations wataingia waliomo na wasiomo, kuzuia hilo unafanyaje?
InafikirishaMkono wa chuma ulisha enda zake, sasa tuko na mkono wa hina na pete.
Hata sasa wakiamua kuwasaka na kuwakomesha wote watatokomea..Kwema Wakuu!
Kutawala Kwa Mkono wa chuma Kwa faida na hasara zake. Moja ya faida ya kutawala Kwa Mkono wa chuma ni nadra Sana kusikia vikundi vya kipuuzi kama sijui panyaroad sijui nini. Ni ngumu Sana!
Watu wenye akili za kimabavu kikawaida hawapendi kushughulika na ishu ndogondogo Kama hizo. Kiufupi hawapendi kupoteza muda na vitu vya kijinga.
Ni tamko Moja tuu kutoa tahadhari kuwa vikundi na watoto HAO waache mara Moja vinginevyo kitakachofuata ni Ghadhabu ambayo haitazingatia Haki za Binadamu.
Dawa ya ku-deal na vikundi vya namna hiyo ni Moja tuu ambayo ukishawapata wa mfano basi wengine wanajifunza.
Mtu Kama hafuati haki za Binadamu hakuna haya ya kumpa haki za Binadamu.
Jino Kwa jino.
Kama wazazi na walezi watapiga kelele nao wawekwe ndani hata mwezi Kwa kushindwa Kulea watoto wao na kuletea taifa matatizo.
Ni kawaida wahalifu kutumia sheria vibaya hasa zile zinazowalinda. Ndio maana watu wanaotawala Kwa Mkono wa chuma kamwe sheria hawazizingatii Sana Kwa sababu huwezi zingatia sheria Kwa watu wasiozingatia sheria Kwa makusudi wakitegemea sheria hizo adhabu zake ni ndogo.
Hata NYUMBANI, Baba asipokuwa Anaongoza familia Kwa upole upole ni rahisi watoto kuharibika, lakini Baba akiwa mkora lazima familia inyooke. Yaani Kwa hiyari au Kwa lazima, watachagua wenyewe wanatakaje. Huwezi leta sheria za demokrasia katika nchi ya watu wajinga na watu Masikini Hilo nilishasemaga.
Hata hivyo, Watawala wanayohaja ya kuangalia namna watoavyo hukumu kulingana na Nia ya mkosaji au mtu anayetofautiana na Nchi. Kama ni Nia nzuri basi itajulikana lakini Kwa upande wa panya road au vitu vya namna hiyo kimsingi hapo ni Shaba.
Mtu Kama hataki mtoto wake asipigwe Shaba basi amfundishe vizuri. Au amwambie afanyie upanyaroad wake Kwa Baba au Mama yake. Akifanyia wengine aliwe kichwa. Wakipatikana wa mfano tuu hata watatu tuu. Huwezi sikia huo ujinga.
Ukatekate wenzako alafu ukikamatwa ATI haki zako zizingatiwe😀😀 labda watakaokukamata ni Baba zako.
Yaani Ukate wake na Watoto wa watu alafu uchekewe, embu kuweni serious kidogo.
Yaani uue watu alafu ati haki zako zizingatiwe, hizo sheria hata mbinguni hazijawahi kuwepo.
Mawazo haya ni Kwa wale wenye akili za mfumo wa Mkono wa chuma, wafuasi WA AZAZEL 😀😀
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Narudia tena wakikamatwa wooote wakatwe miguu asitikee hata mmoja atakaeweza kutembea..Tufuate Sheria Ili Mungu asitupige Kwa mapigo makuu.
Hayupo anayefurahia Damu ya raia kumwagika. Damu Si kitu kinatakiwa kizoeleke kumwagwa.Kwahyo mtoto wako akienda ua raia wasio na hatia na kuwaibia wewe kama baba unafurahia? Akiua naye auliwe period. Uchungu unaoutaja ndo huo mzazi wa mwingine anaupata sababu ya mtoto wako acheni kutetea upumbavu
Wahalifu kama panya road wakifanya uhalifu asasi za haki za binadamu kimya ila wahalifu wakishughulikiwa asasi hizo hizo zinaamka kuwatetea. Makes you wonder wapo kwa maslahi ya nani?
Umeongea vyema. Mtoto akihasi, huyo ni adui hata kwa wazazi wake. Watoto kama hawa hawaoni hatari kuwadhuru au hata kuwaua wazazi pindi wakizuiwa kupata wanachotaka. Miaka ya nyuma kidogo, maeneo ya Kimara Mwisho, mtoto mmoja alimvizia baba yake na kumuua, kisa hakumpa alichohitaji kwa wakati aliotaka yeye. Nyie mnaoshupalia haki za binadamu naombea yawakute haya mambo ili akili iwakae sawa! Unateteaje ujinga?!Ishu ya kuwa na watoto wa Aina hiyo Hilo sio shida.
Mtoto kama halitaki kusikiliza maonyo ya Baba yake unataka Mimi kama Baba nifanyeje?
Apigwe Shaba hata kama nitaumia lakini No way.
Tabia za kuonea huruma matoto maasi Kama mashoga ni Dalili ya ushetani ambao wanaume tutalaumiwa.
Mama ndiye anapaswa na anayohaki ya kuwa na huruma na watoto lakini Baba, Kama toto linaendekeza ujinga ni Kupiga Shaba lisiendelee kukutia aibu.
Hizi sheria za siku hizi ndizo zinalea haya mambo
Ilikua unakamatwa afu unapoteza maisha ukiwa unapelekwa hospitali bada ya kupigwa risasi ya paja..wakati unataka kutoroka ulipoenda kuonesha ulipoficha silaha...MBONA WAKATI WA MAGU HAYA MAMBO HAYAKUWEPO? ALIFANYAJE MZEE JOHN?
Umeongea vyema. Mtoto akihasi, huyo ni adui hata kwa wazazi wake. Watoto kama hawa hawaoni hatari kuwadhuru au hata kuwaua wazazi pindi wakizuiwa kupata wanachotaka. Miaka ya nyuma kidogo, maeneo ya Kimara Mwisho, mtoto mmoja alimvizia baba yake na kumuua, kisa hakumpa alichohitaji kwa wakati aliotaka yeye. Nyie mnaoshupalia haki za binadamu naombea yawakute haya mambo ili akili iwakae sawa! Unateteaje ujinga?!
Nitajieleza bila kigugumiz na nitaeleweka,Mimi sikuuingi mkono! suppose it were you caught in the operation web while coming from the shop?