Ile Taasisi bora ya akina mama barani Africa , na ambayo inatajwa kushika namba 3 kwa ubora duniani kwa sasa , BAWACHA , Imeishika Nchi kwa kiganja kimoja cha mkono wa kushoto.
Pamoja na kwamba Bawacha ni Taasisi ya wanawake , lakini nguvu kubwa inayotumiwa na Jeshi la Polisi kuwadhibiti bila kufuata PGO , tena bila Mafanikio inazidi kuipaisha Taasisi hiyo
View attachment 1961227
Kwa kifupi ni kwamba hoja za Polisi za kujaribu kuhusisha Jogging za Bawacha na harakati za kisiasa HAZINA MASHIKO , BAWACHA ni Taasisi ya kisiasa , chochote watakachokifanya hauwezi kukitenganisha na siasa , kiongozi wa kisiasa hawezi kubadilika kwa mavazi , hata akiingia Kanisani au Msikitini atabaki kuwa mwanasiasa tu , hata akihudhuria msiba bado TAITO yake ya uanasiasa haitapotea , udiwani wake , ubunge au uenyekiti wake hautaondoka kwa vile yuko kwenye mazishi .
Kwahiyo kuwazuia BAWACHA kufanya mazoezi kwa vile ni viongozi wa kisiasa , au labda kutaka wanasiasa hao wafanye mazoezi yao au Jogging zao huku vyeo vyao wameviacha nyumbani ni KITUKO kisichowezekana , Polisi ni lazima iseme ni namna gani kiongozi anaweza kujitokeza kama raia huku akiacha cheo chake nyumbani , na ni wakati gani ambao anapaswa kutembea na cheo chake , Kwa mfano , ni wakati gani Waziri labda Jenister Mhagama anakuwa Waziri ni wakati upi anakuwa Raia ? bila shaka si rahisi .
Bali Polisi wanapaswa kulinda amani na usalama tu , wakianza kupiga ramli na kuzuia wengine kukimbia barabarani kwa Visingizio vya kichovu watajidhalilisha tu , uonevu duni kama huu hautasaidia Polisi katika lolote na wala HAUTAFANIKIWA , zaidi utatengeneza Uhasama wa Kudumu .