Ndiyo!
Nguvu ya matajiri ikiilemea serikali hii mpya, wanyonge watalitaja Jina la JPM Kwa uchungu mkubwa na hakuna atakayewazuia
Pale rushwa itakapowafanya wanyonge, wamachinga, wamama ntilie, bodaboda, bajaji n.k ambao idadi Yao ni kubwa mno Kwa sasa katika nchi hii kuanza kufukuzwa kwenye maeneo Yao ya kazi aliyokuwa amewaruhusu Jembe Lao JPM R.I.P kufanyia biashara zao,
Ndipo sauti zao zitapazwa wakimlilia Kwa upya tena JPM na Jina lake litatawala Kwa upya kwenye vyombo mbalimbali za habari kote Tanzania na hata duniani
Pale majambazi ya kupora muda wowote yatakapojitokeza iwapo serikali hii haitasimama Kiume, sauti za wananchi wengi watakapoanza kumlilia JPM Kwa upya na watu watasema ni Bora alipokuwepo Jembe
Pale matajiri wakubwa watakapoizidi serikali ujanja aidha Kwa rushwa Ili wasilipe Kodi na Kodi nyingi kuelekezwa Kwa wafanya biashara wadogo wadogo, watu hawa wataanza kumlilia upya Jembe lao, watasema, ni Kwa sababu hayupo JPM ndio Maana wananyanyaswa?
Ingawa Nina Imani kuuubwa Sana na Raisi wetu Madame SHS, kwamba ni jemedali na jasiri asiyeogopa na asiyerudishwa nyuma, Kwa kuwa pia ufanisi wa serikali hii Naamini ni Kwa sababu mama alisimama nyuma yake kuhakikisha tunakuwa hapa tulipo
Mbali na hayo, Sisi ni binadamu tunaweza kujisahau yakarudi hayo na yakawa sababu ya Jina la Jembe kutajwa kila pahala kuwa yeye alikuwa ndiye na kimvuli chake kutawala midomo mwa watu wanyonge
Mh Raisi Madame Samia suluhu Hasan Tunakuombea, kwani tunajua ilivyongumu kuongoza nchi bila ya Mungu Kusimama Mbele yako
Wasalaam