Nguvu za giza na mizimu ya ukoo

Nguvu za giza na mizimu ya ukoo

Ila nilichokiona humu kwenye haya matatizo ya kiroho kila mtu anaona hayana ujuzi kwa maana kila mtu anatoa tu maoni yake binafsi kwa mitazamo yake na si kwa uelewa au uzowefu.
 
Utapigwa zaidi hasa ukichanganya Mungu na Mizimu...

Chagua kubaki kwa Mungu...
 
Kwanini unaamini vitu vya kuambiwa na hisia za ajabu? Hapo tatizo ni wewe na wala hayo mambo hayapo mahali popote.fanye setting yako ya mind upya na nenda hospital.
 
Habari wana JF, mimi ni new member ningependa mnikaribishe katika Jukwaa letu.

Mimi Ni kijana wa miaka 30’s, kwa mda wa miaka 3 nimekua nikisumbuliwa na Nguvu za giza na Mizimu ya ukoo ambayo imepelekea kuharibu dira ya maisha yangu, nilianza na kuumwa homa za ajabu ajabu, mwili kuchoka, dalili za homa ya Presha.

Nilihangaika sana ikiwemo kwenda kwa waganga wa kienyeji, nikawa napata nafuu lakini baada ya mda hali inarudi palepale, nikajaribu na makanisani ikawa ni vita kali, nako nikawa napata nafuu ila hali inarudi pale pale ikiwa kuhisi mwili unaumwa, kuchoka, macho kuhisi yana kiza na Moyo kuuma sana.

Nilihangaika pia na maombi binafsi ya kujiombea mimi mwenyewe pamoja na watumishi wa Mungu, nikafanikiwa kupunguza hii hali kwa kiasi chake nikapata nafuu.

Kuja kwenu wanaJF ninaomba ushauri kwa sababu nimefungwa upande wa uchumi, akili yangu imefungwa.

Inafika hatua ya kukata tamaa na kuona kila kitu hakiendi na pia kila ninapopata ishu ya kazi au dili lolote hua inafika sehemu mambo yanaharibika, nimekua na roho ya kukataliwa, kila ninapoenda ninadharauliwa na kubezwa, nilishaenda sehemu nikahisiwa mimi ni Mwizi, kiukweli ni kama nina mikosi au gundu.

Siku Moja niliwasiliana na ndugu wa baba ambao wao ni wasukuma, wakaniambia hio kawaida kuna mizimu inabidi kwenda kutambika kwa sababu ukoo wetu tangu enzi ni wa mambo hayo ya kimizimu.

Nipo kwenye dilema nikubaliane na mambo ya kutambika au niendelee huku niliko upande wa Makanisa, japo kiukweli napata vita kubwa kila napopigana na hizi nguvu makanisani.

WanaJF kiukweli nimefika hatua nachanganyikiwa, kila kitu hakiko sawa, nakosa kujiamini kwa kila jambo nalotaka kufanya, ninaomba ushauri wenu na mawazo yenu.

Najua Jukwaa hili lina watu wenye maarifa na maono. Nitashukuru sana

Cc MshanaJR
Yesu Kristo ndio kiboko ya yote hayo. Tatizo ulienda kanisani kwaajili ya kuponywa na si kunyoosha njia zako baada ya uponyaji. Ukiamua kumtumikia Yesu kikamilifu hakika hayo yote yatakukimbia.
 
Benil Mizimu inatesa mno ingia YouTube tafuta Bishop Elibariki Sumbe my dear masomo yote ya mizimu na utendaj kaz wake utaelewa.. Hutobaki kama ulivyo
Sana kwa ambao hawajapata changamoto hii ni ngumu kuelewa,
 
Kama kijana wa miaka 30 anaenda kwa mganga vipi akifikisha miaka 50 huko?

Nenda hospitalini kwanza acha ilani za kijinga
mkuu unapofikwa na majanga makubwa hasa hasa homa ambayo inakukatisha tamaa. Chochote utakachoambiwa tiba utakubali tu ili mradi ukae sawa, sio kwamba nilivyoanza kuumwa sikwenda hospitali, nilienda na Hakuna homa, ilifikia hatua Daktari ananipa ushauri nikanywe maji mengo zaidi, nifanye mazoezi na kula matunda mana homa haionekani. Mimi binafsi kwa niliyopitia siwezi kurudi tena kwa waganga wa kienyeji
 
Habari wana JF, mimi ni new member ningependa mnikaribishe katika Jukwaa letu.

Mimi Ni kijana wa miaka 30’s, kwa mda wa miaka 3 nimekua nikisumbuliwa na Nguvu za giza na Mizimu ya ukoo ambayo imepelekea kuharibu dira ya maisha yangu, nilianza na kuumwa homa za ajabu ajabu, mwili kuchoka, dalili za homa ya Presha.

Nilihangaika sana ikiwemo kwenda kwa waganga wa kienyeji, nikawa napata nafuu lakini baada ya mda hali inarudi palepale, nikajaribu na makanisani ikawa ni vita kali, nako nikawa napata nafuu ila hali inarudi pale pale ikiwa kuhisi mwili unaumwa, kuchoka, macho kuhisi yana kiza na Moyo kuuma sana.

Nilihangaika pia na maombi binafsi ya kujiombea mimi mwenyewe pamoja na watumishi wa Mungu, nikafanikiwa kupunguza hii hali kwa kiasi chake nikapata nafuu.

Kuja kwenu wanaJF ninaomba ushauri kwa sababu nimefungwa upande wa uchumi, akili yangu imefungwa.

Inafika hatua ya kukata tamaa na kuona kila kitu hakiendi na pia kila ninapopata ishu ya kazi au dili lolote hua inafika sehemu mambo yanaharibika, nimekua na roho ya kukataliwa, kila ninapoenda ninadharauliwa na kubezwa, nilishaenda sehemu nikahisiwa mimi ni Mwizi, kiukweli ni kama nina mikosi au gundu.

Siku Moja niliwasiliana na ndugu wa baba ambao wao ni wasukuma, wakaniambia hio kawaida kuna mizimu inabidi kwenda kutambika kwa sababu ukoo wetu tangu enzi ni wa mambo hayo ya kimizimu.

Nipo kwenye dilema nikubaliane na mambo ya kutambika au niendelee huku niliko upande wa Makanisa, japo kiukweli napata vita kubwa kila napopigana na hizi nguvu makanisani.

WanaJF kiukweli nimefika hatua nachanganyikiwa, kila kitu hakiko sawa, nakosa kujiamini kwa kila jambo nalotaka kufanya, ninaomba ushauri wenu na mawazo yenu.

Najua Jukwaa hili lina watu wenye maarifa na maono. Nitashukuru sana

Cc MshanaJR
Usifanye mazindiko yoyote ya kimila ni hatari zaidi, endelea kuamini kuwa Mungu anaweza yote Mungu ndiyo jibu la uzima wa milele, ukiingia huko kutoka ni ishu zaidi maana utakua umeingia kwenye maagano ya nguvu za giza
 
Hebu nenda kajipatanishe na ndugu zako. Hizi dini tumeletewa tu. Unaacha miongozo ya asili yako unaanza kuhangaika na mungu wa Israel!!!... You are not serious.
 
Hapana HIV sina mkuu nilishapima
Sawa mkuu , ila badilisha mtazamo wako kuhusu hiyo hali , utakua poa tu, hali kma hyo inampata kila mtu tu , chukulia kawaida.
 
Mateso yalikuandama pale ulipooanza sana kuamini uganga kuliko mambo mema ya Mungu, Mungu huwa haziakiwi, nachukuia sana kuona mtu anapambana kweli na mambo ya giza, uganga, uchawi, ushirikina
 
Back
Top Bottom