NHIF huwezi katia bima wategemezi waliopo kisheria mfano mama akibadili jina

NHIF huwezi katia bima wategemezi waliopo kisheria mfano mama akibadili jina

Kwa hiyo mtoa mada unataka umukatie Mama Mkwe wako bima,utakuwa umelogwa sio bure
Ukishalipia Bima inaruhusu kuwaunganisha watu 6 kwa gharama hiyo hiyo uliyokatwa kwenye mshahara kwa maana hata ukiwabania hao wakwe bado utakatwa kiasi kilekile cha pesa haipunguzi wala haiongezi kitu
 
NHIF ni tatizo lingine watumishi wa nchi hii, ni kichaka cha kurudisha nyuma maendeleo ya watumishi wa nchi hii.

Kwanza waruhusu mtumishi hata kama una watoto kumi wote waweze kupata huduma.

Hili NHIF kuwa na idadi ya wategemezi hasa upande wa watoto ni tatizo na ni janga kwa mtumishi, ni vyema NHIF waliangalie hili
 
Umeleta jambo zuri sana kujadiliwa hapa na wengi tutapata abcd kutoka kwa wenye kujua jambo hili vizuri
 
Mchango wenye manufaa makubwa huu kwa jamii.

Lakini kama ilivyo kawaida, mada za aina hii hazipati wachangiaji.

Hongera mkuu 'Mulokole'.

Acha niulize swali la pembeni mwa mada husika: hivi wewe ni 'Mulokole' kweli?
Yes, mimi ni mulokole na mtumishi kabisa wa Mungu. Nilianza kujiita jina hilo hapa JF mwaka 2007, nikaja kuokoka mwaka 2015. So nilijitabiria neema hii
 
Affidavit haitambiliki huko.. tafuta kitu kinaitwa deed pool umemaliza mchezoo, hyo ndo yenye mamalaka ya kutambua majina yote. Jpo ni gharama zaid
Nilienda na deed pool nabado walinikatalia
 
Tatizo watanzania wako negative sana. Hawajui hata maana ya insurance. Ukiacha vitu hivi vikawa havina taratibu utaua mfuko. Watu wanalalama kwamba NHIF ni wazeewa makato, ndio, maana wanachokata kwako wewe unayelalama, ndicho kinachowalipia matibabu maelfu ya watu ambao ama wanaumwa wao au wategemezi wao.

Kuna jamaa wanapiga kelele humu, lakini utakuta tegemezi wake ana magonjwa sugu kibao, na anakula pesa za mfuko wa Bima zaidi ya laki 2 kila mwezi, wakati huyo mtoto wa tegemezi anakatwa kila mwezi chini ya elfu 50. Sasa ikiwa tegemezi wake anakula zaidi ya laki 2 kwa mwezi, na yeye na familia yake labda pia anatibiwa hapa na pale, unadhani hizo pesa za juu zinatoka wapi? Zinatoka kwa wanachama wengine ambao wanakatwa pesa ndigo kila mwezi, lakini hawaumwi.

Ukitaka ujue umuhimu wa bima, subiri yakufike.

Kulikuwa na umuhimu kuwa na kipengele cha kujitoa kwenye huu mfuko, ili watu waje wasimulie yakiwapata.

Kumbuka mchango unaotoa NHIF, huwa hautoshi kukupa matibabu.
We jamaa umeeleza vizuri sana.

Watanzania wengi hawajielewi sana sana Watumishi wa Serikali

Watu hawajali Afya zao kabisa, wao wamefanya miili yao madampo

Wakiugua unawaonea huruma

Itafika wakati NHIF itakataa kutibu Magojwa yasiyoambukizwa au watataka kwa hayo magonjwa we naye ulipie gharama kiasi ili utibiwe au wakukate zaidi
 
Yes, mimi ni mulokole na mtumishi kabisa wa Mungu. Nilianza kujiita jina hilo hapa JF mwaka 2007, nikaja kuokoka mwaka 2015. So nilijitabiria neema hii
Hongera zako mkuu 'Mulokole' kwa "kuokoka"!

Jibu lako hili linanifanya niulize swali la nyongeza.

Mhusika akishakuwa mulokole, anaweza akarudi tena hali yake ya zamani, yaani ulokole ukamwisha, au ukishapatikana, ndiyo basi tena unakuwa ulokole wa milele?
 
NHIF intention yao sio kutoa huduma ni kukomoa tu. Imagine kuna dogo mmoja baba yake na mama yake walifariki kitambo akalelewa na kaka yake huko kijijini, kaka amepambana kumsomesha huyo dogo tangu chekechea mpaka leo dogo amemaliza diploma amepata kikazi chake. Kwenye wategemezi wa NHIF si kamuandika kaka yake maana yeye anasema hata baba yake hamkumbuki sababu alilelewa na kaka yake huyo tangu akiwa mdogo.

Eti NHIF wamemkatalia. Ona sasa kwa bahati mbaya ktk harakati za msiha huko kijijini kaka yake kaoata ajali, yani dogo anahangaika huyo hadi anatia huruma. Mbaya zaidi yeye ndio tegemezi kwa kaka yake. Amenipigia simu juzi mpaka analia ananiambia bro kaka anakufa nisaidie, gharama zimekua kubwa na NHIF hawamtambui kama mtegemezi wangu wakati mshahara wangu wanakata kioa mwezi.

Niliwaza nikajisemea hivi hawa ndo wanataka bima ya afya kwa wote?

Hii nchi wapuuzi ni wengi sana
Bima inatambua Wazazi 2, inatambua Tegemezi 4 walio chini ya Miaka 21
 
Serikali iweke option, ikiwa mfanyakazi hataki kujiunga NHIF aweze kujitoa kwa hiari...!! Isiwe lazima kuchangia, iwe willing ya mtumishi kujiunga au kujitoa
Ukiugua?
 
Tatizo watanzania wako negative sana. Hawajui hata maana ya insurance. Ukiacha vitu hivi vikawa havina taratibu utaua mfuko. Watu wanalalama kwamba NHIF ni wazeewa makato, ndio, maana wanachokata kwako wewe unayelalama, ndicho kinachowalipia matibabu maelfu ya watu ambao ama wanaumwa wao au wategemezi wao.

Kuna jamaa wanapiga kelele humu, lakini utakuta tegemezi wake ana magonjwa sugu kibao, na anakula pesa za mfuko wa Bima zaidi ya laki 2 kila mwezi, wakati huyo mtoto wa tegemezi anakatwa kila mwezi chini ya elfu 50. Sasa ikiwa tegemezi wake anakula zaidi ya laki 2 kwa mwezi, na yeye na familia yake labda pia anatibiwa hapa na pale, unadhani hizo pesa za juu zinatoka wapi? Zinatoka kwa wanachama wengine ambao wanakatwa pesa ndigo kila mwezi, lakini hawaumwi.

Ukitaka ujue umuhimu wa bima, subiri yakufike.

Kulikuwa na umuhimu kuwa na kipengele cha kujitoa kwenye huu mfuko, ili watu waje wasimulie yakiwapata.

Kumbuka mchango unaotoa NHIF, huwa hautoshi kukupa matibabu.
Mimi wazee wangu wote wako na magojwa sugu kila mwezi wanapomwenda clinic bili hua ni laki Saba mpaka milioni na ushehe, kiukweli nawaza bila NHIF abadani tusingeweza mudu gharama za matibabu, bima ya afya ni kitu Cha mhimu sana.
 
Mimi wazee wangu wote wako na magojwa sugu kila mwezi wanapomwenda clinic bili hua ni laki Saba mpaka milioni na ushehe, kiukweli nawaza bila NHIF abadani tusingeweza mudu gharama za matibabu, bima ya afya ni kitu Cha mhimu sana.
Ni clinic ya nini hiyo mpaka igharimu pesa zote hizo?

Au wanafanya MRI kila wakienda clinic?
 
Back
Top Bottom