NHIF Waongeza gharama za Bima ya Afya kwa Watoto, sasa kulipa Tsh. 120,000/= badala ya Tsh. 50,400/=

NHIF Waongeza gharama za Bima ya Afya kwa Watoto, sasa kulipa Tsh. 120,000/= badala ya Tsh. 50,400/=

WaTanzania asili yetu ni watu wa kulalamika lalamika bila hata kutumia akili zetu ku- reason out, hiyo kasumba ililetwa na siasa za ujamaa za kuchonganisha sera za kibepari na raia wake, 120,000 ni sawa na sh 10,000 kwa kila mwenzi kwa ajiri ya afya ya mwanao.

Kwa kweli hiyo sio nyingi, kwa nchi nilizo tembelea bima ni gharama kubwa sana mara 5 au 10 na ya kwetu, tuwe fair some time, mtumishi wa wastani anakatwa 40,000 ya mshahara wake kila mwezi kwa ajiri ya bima hao ndo wanao fidia hiyo pesa tuwe waelewa katika vitu vya msingi kama afya ya wstoto wetu kama huwezi kutenga 10k kwa ajiri ya afya ya mwanai kila kwanini unaendelea kuwapa wanawake mimba?

Covax, ni kweli tuna kawaida sana ya kulalamika lakini sidhani ni sahihi kudhani tabia hiyo ndio msingi wa malalamiko!! Sio kwa sababu ya kulalamika ndio tunalalamika! Kwa jinsi madawa yanavokuwa hayapatikani au magonjwa kutolipiwa bima, ongezeko lolote lisiloendana na uboreshaji wa huduma - ni wizi!! Ndicho kinacholalamikiwa na wengi hapa japo wengi wameshindwa kukieleza.

Unazungumzia gharama ya juu ya bima za wenzetu - je gharama hizo zinawiana na kiwango cha bima??? Nadhani jibu litakuwa ni NDIYO. Je ukiondoa hili ongezeko, kuna guarantee imetolewa kuhusu uboreshaji au upatikanaji wa huduma???
 
Ndo umuulize mtoa mada amekitoa wapi, maana NHIF wameifuta kabisa, sisi wengine twatibiwa watoto wetu hadi ikifika mwisho wake ndo kwa heri

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Toa hiyo amount ambayo analipa mzazi pamoja na mtoto mmoja kwa amount ambayo analipa mzazi peke yake
 
Kuna Katibu mkuu wizara ya afya miaka ya nyuma aliwapuuza madaktari wakati wana madai yao ya msingi na akazima ule mgomo.

Mama yake alipopata maradhi akapekekwa Muhimbili ili atibiwe na madaktari walewale, Ki ukweli Alicia pale Muhimbili hakupata huduma stahiki.

Sasa mtu kapoteza mama kwa kujifanya mjuwaji kosa ana Madaraka, kuna mijitu mjinga sana.

Nakumbuka zamani road licence tulikuwa tunalipia 20,000 kwa magari yote, alipoingia Zakhia Meghji kuwa waziri wa fedha akapandisha 150,000 mpaka 350,000, kwakuwa yeye anatumia shangingi la serikali.

Matokeo yake watu tukawa tunabandika sticker za kariakoo kwa 20,000 tu serikali inakosa mapato.

At least huyu aliefuta road licence na kuihamishia kwenye mafuta unaweza kusema anayo akili.

Sasa ukimuona Zakhia Meghji Sasa hivi utadhani amekoswakoswa na kombora la Mrusi shenzi zake, Ki sukari kinatamfuna tu.
Duh
 
Hakuna Serikali ni rafiki ya maskini, tutafute hela.
Ukiona kiongozi wa Serikali anawakenulia bodaboda ama wapika wali ujue ana jambo lake.
 
Hii nchi ina viongozi wa ajabu sana.
Mwananchi huyu anae shindwa kumnunulia mtoto sare ya shule, ndie anae ambiwa alipe bima ya familia. Mwananchi huyu anae kula mlo mmoja ndie alipe bima ya afya. Mwananchi snae katwa tozo hata kwenye pesa akiyo tumiwa na mwanae ndie akate bima ya afya. Huku wanao agiza haya wako kwrnye V8 inayo jazwa mafuta na mlala hoi.
Bima ana lipiwa na mlala hoi.
Ccm imefikia mwisho wa kufikiri. Tuna hitaji mawazo mbadala.
 
Tunaposema siasa ndio kila kitu, kuna wapuuzi wengi wanajitokeza kupinga na kukejeli kwamba siasa haiwezi kukuletea chakula mezani. Nashauri NHIF waongeze gharama za bima ifike 500,000/= kwa kila mtoto, ili akili ziwarejee watanzania wajue umuhimu kupatikana kwa KATIBA MPYA
Katiba haiwezi saidia lolote kwenye nchi yenye wajinga wengi

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Tunaposema siasa ndio kila kitu, kuna wapuuzi wengi wanajitokeza kupinga na kukejeli kwamba siasa haiwezi kukuletea chakula mezani. Nashauri NHIF waongeze gharama za bima ifike 500,000/= kwa kila mtoto, ili akili ziwarejee watanzania wajue umuhimu kupatikana kwa KATIBA MPYA
Katiba mpya inayopiganiwa Tanzania ni kwaajili ya wanasiasa wagawane keki vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Toa hiyo amount ambayo analipa mzazi pamoja na mtoto mmoja kwa amount ambayo analipa mzazi peke yake
Kwa ufupi hakuna package ya mtoto peke yake iwapo hapitii bima ya shuleni
 
Nchi hii kulipia vitu wana copy Nchi za Ulaya wakati wenzetu wao hawana vyanzo vya kodi zaidi ya watu kuchangia kwa % kubwa huku vyanzo tulivyo navyo utadhani ni vya Waarabu havichangii kitu chochote kumpunguzia Mwananchi maumivu hizo hospital za kanda gharama zake utadhani wanaotibiwa ni Wageni...Roho mbaya na ubinafsi ndio inapelekea muda wote kuja na gharama za ajabu ajabu....
Lazima watu washiuke
 
Wale wanaomuita Rais "MAMA"sijui wanaliongeleaje suala la mtoto wa maskini kupandishiwa Bei ya bima na mama Yao😳😳😳😳

Naamini maridhiano hayahusiani na masuala haya ya maskini 😠😠
 
Haya mambo ya NHIF yananikumbusha miaka hiyo Mzee mmoja alikuwa HR wetu.

Wale wazungu kwenye vikao vya management wakajadili njia bora ya wafanyakazi kupata matibabu je wawe wanaleta risiti ya matibabu kuclaim refund au waingie mkataba na hospitali?

Basi yule Mzee HR Mtanzania mwenzetu bila aibu akasema mishahara yetu tayari ina pesa za matibabu, basi wale wazungu wakaona kwakuwa huyu ni Mtanzania mwenzetu basi yupo sahihi.

Kimbembe akaumwa mke wake tikatika Mzee akampeleka Agha Khan si HR wa kampuni ya wazungu bwana, mama alilazwa wiki mbili tu bill million 15, akachukuwa invoice akapeleka ofisini ili wazungu wamlipie, Sasa ninachowapenda wazungu wapo straight wakamuulize Mzee swala la matibabu si lipo kwenye mishahara ya wafanyakazi?

Huu ndio ubinafsi nauona kwa NHIF, wao hawajioni kama ni Watanzania au wana ndugu wanaoathirika na huu upuuzi wao.

Kwa huruma ya wazungu walimpa cheque yulw Mzee akalipe bill lakini atakatwa pesa yote kwenye mshahara wake.

Kwa roho mbaya ya yule Mzee Mungu akamlaani ampaka anakufa anakaa vigorofa vya NHC vya nyumba viliwi na sebule wakati alipaswa awe na mjengo wa maana na compound ya kutosha.
Hivi kwanini waTz wenye cheo lwenye kampuni/taasisi au shirikabla kigeni hapa Tz hupenda kuwa kandamiza wa tz wenzao.. unakuta wanawaambiabwazungu/wageni hata mishahara na some benefits wazitoe /wapunguze kabisa..
 
Hili jopo lililopitisha hii ni la watanzania kweli?

Mfuko hauna hela, beneficiaries wanataka huduma bora, wao wameona kwa faster wapandishe bei ili mapato ya pande juu! Burden inaenda kwa mwananchi! Hatari!
 
Nchi hii kulipia vitu wana copy Nchi za Ulaya wakati wenzetu wao hawana vyanzo vya kodi zaidi ya watu kuchangia kwa % kubwa huku vyanzo tulivyo navyo utadhani ni vya Waarabu havichangii kitu chochote kumpunguzia Mwananchi maumivu hizo hospital za kanda gharama zake utadhani wanaotibiwa ni Wageni...Roho mbaya na ubinafsi ndio inapelekea muda wote kuja na gharama za ajabu ajabu....

Mkuu umenikumbusha kwa miaka mingi sijasikia tukitangaziwa mapato yatokanayo na;

- Madini
-Gesi asili
-Mali asili na utalii

Ni kama tumeanza upya au mimi sielewi maana kwa sasa ni tozo, mikopo ya kutoka nje, misaada ndio vinatajwa!

Cc pascal
 
Mfuko hauna hela, beneficiaries wanataka huduma bora, wao wameona kwa faster wapandishe bei ili mapato ya pande juu! Burden inaenda kwa mwananchi! Hatari!
Watuonee huruma kwa kweli,huduma zenyewe ni tia maji tia maji haswaa
 
Back
Top Bottom