benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,533
- 3,187
Habari za awali zinadai kwamba Mfuko wa Taifa wa BIma ya Afya umefuta rasmi bidhaa ya "Toto Afya Kadi" iliyokuwa inatolewa na mfuko huo kwa watoto wa chini ya miaka 18 wanaosajiliwa ili kuwawezesha kupata huduma za matibabu katika vituo vilivyosajiliwa na NHIF nchi nzima.
Ikumbukwe kuwa Toto Afya Kadi ilikuwa inatoa nafasi kwa watoto chini ya miaka 18 kutibiwa kwa gharama ya Tsh. 50,400/= kwa mwaka mzima.
Lakini miongozo iliyotoka hivi karibuni inaonesha kuwa mwanachama aliyekuwa akitibiwa kwa bima hii hawezi kufanya malipo mapya pale bima yale inapokwisha muda wa matumizi (hawezi kurenew).
Hivyo ni kama imeondolewa kimyakimya na hata ukitaka kulipia Bima hiyo hivi sasa wanakwambia kuwa huduma haipo.
======
NHIF yatoa ufafanuzi kuwa hawajafuta kifurushi cha Toto Afya ila wameboresha ili na wazazi wao waingie.
Ikumbukwe kuwa Toto Afya Kadi ilikuwa inatoa nafasi kwa watoto chini ya miaka 18 kutibiwa kwa gharama ya Tsh. 50,400/= kwa mwaka mzima.
Lakini miongozo iliyotoka hivi karibuni inaonesha kuwa mwanachama aliyekuwa akitibiwa kwa bima hii hawezi kufanya malipo mapya pale bima yale inapokwisha muda wa matumizi (hawezi kurenew).
Hivyo ni kama imeondolewa kimyakimya na hata ukitaka kulipia Bima hiyo hivi sasa wanakwambia kuwa huduma haipo.
======
NHIF yatoa ufafanuzi kuwa hawajafuta kifurushi cha Toto Afya ila wameboresha ili na wazazi wao waingie.