Ni aibu kubwa sana kwa Wilaya kongwe ya Kyela kukosa gari la Zimamoto

Ni aibu kubwa sana kwa Wilaya kongwe ya Kyela kukosa gari la Zimamoto

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Kyela ni miongoni mwa Wilaya kongwe kabisa za Tanzania , lakini ni Wilaya ya mwisho kabisa kufaidi keki ya nchi hii , kwa miaka yote tangu uhuru imeongozwa na Wabunge wa ccm tu , akiwemo yule mmoja aliyetamba hadharani kwamba ANAMILIKI DIGRII 4 na wala hana njaa yoyote .

Halmashauri ya Wilaya hii haijawahi kuongozwa na chama kingine zaidi ya ccm tangu uhuru wa Tanganyika , huku Mwenyekiti aliyepita wa Halmashauri hiyo akiitwa Hunter Mwakifuna aliyekuwa Diwani wa Ipinda , huyu akishirikiana na DED aliyepita walichukua Soko la Wilaya ambalo ni mali ya wananchi na Chanzo Kikuu cha Mapato na kuipa ccm , yaani soko lililokuwa mali ya Halmashauri sasa hivi ni mali ya ccm (Naapa mbele za Mungu kwamba iko siku nitalirejesha mikononi mwa umma).

Lakini pamoja na Sarakasi zote hizo za watu hawa Wameshindwa kabisa kuwa na UBONGO UTAKAOWAKUMBUSHA UMUHIMU WA KYELA KUWA NA GARI LA ZIMAMOTO , hii ni Aibu kubwa mno na fedheha kwa Watu wa Kyela , Hivi ninavyoandika haya Hospitali ya Binafsi ya Dr Mwaihula , iliyo maeneo ya Mpanda ambako ni karibu na ofisi za Relwe inateketea kwa moto bila msaada wowote , vidumu vya maji vya wananchi havijafua dafu , Mwaka uliopita hospitali ya wilaya ilishika moto na wananchi wakaokoa kwa kutumia njia za kienyeji za kuzima moto , Je siku soko la Kyela lililo katikati ya mji likishika moto (siombei lakini yanatokea) ni nani atasalimika ? kwanini viongozi wa Kyela hawaioni hii hatari , wanataka nini kiteketee ili waone umuhimu wa gari la Zimamoto ?

Nakulilia Kyela , nakuahidi iko siku nitakukomboa .
 
Hao si wanyakyusa achana nao hao ,acha waisome namba tuu
 
Kyela Zimamoto ya Nini mnataka ikazime Moto mashamba ya mpunga au?

kimjii chennyewe choka mbaya
 
Mambo yanayoendelea kyela na ilivyo na ukongwe wake ni shida sana pale sijui tatizo ni nini
 
Dar water table iko karibu watu wanachimba visima wenyewe nyinyi pesa za mchele mnapekeka wapi? Kwenye ushirikina au?
mwaka wa 4 huu hakuna wateja wa Mchele , hii ni baada ya wafanyabiashara wengi kufirisiwa
 
Usishangae hakuna hata water reservoir zipatazo hata tano wilaya nzima.
Hamna kabisa ile wilaya ina vyanzo vikubwa vya mapato ina Bandari,Ina Border ya Kasumulu(Malawi) ina Zao Adhimu la Cocoa kuna Mchele safi toka kyela ni bado kuna uvuvi kutoka ziwa nyasa.Sema watu wake nao wamezidi kujifanya mamwinyi hawataki kazi kushinda vibarazani kumdema yule ni free mason.
 
Hamna kabisa ile wilaya ina vyanzo vikubwa vya mapato ina Bandari,Ina Border ya Kasumulu(Malawi) ina Zao Adhimu la Cocoa kuna Mchele safi toka kyela ni bado kuna uvuvi kutoka ziwa nyasa.Sema watu wake nao wamezidi kujifanya mamwinyi hawataki kazi kushinda vibarazani kumdema yule ni free mason.
Kwenye uvivu nakupinga
 
Back
Top Bottom