Kazi kubwa za vyuo vikuu ni tatu:
-kuelimisha/kifundisha (teaching)
-kuandika vitabu (publication)
-kufanya tafiti (Research).
Kati ya kazi hizo tatu research ndiyo huleta maana kubwa sana kwa uwepo wa chuo kikuu chochote mahala popote. Ni sawa na benki, kwa mfano, ina kazi nyingi sana lkn utoaji wa mikopo ndiyo huleta tija na faida zaidi kwa jamii na benki yenyewe..
Nimestushwa na mfululizo wa matamko ya tahadhari dhidi ya korona yanayotolewa na vyuo vikuu hapa nchini kwa jumuiya zao.
Nilitegemea vyuo vikuu hivi viwe vimeshafanya tafiti na kuja na chanjo ya korona badala ya kutupigia kelele bila suluhisho.
Najiuliza maswali mengi kuhusu hivi vuuo vikuu. Hivi kuna wasomi kweli? Ama kuna mkusanyiko wa wahuni wenye vyeti tu? Tija yao nn kwa taifa? Vyuo viku hivi vimeshindwa kushirikiana vikatuletea hata dawa za kufubaza virusi hivi?
Malaria, ukimwi, athma, mafua ni magonjwa ambayo yapo kwa miaka lukuki lkn hivi vuuo vikuu havijagundua hata kidonge!
Sasa navitaka vyuo vikuu hivi kukaa kimya, endeleeni kunywa pombe, kufanya ngono, na kurushiana video za umbea. Mqmbo ya corona waachieni Oxford, Harvard na Berlin universities waizungumzie.
Rubbish!!!