Ni aibu msomi kufanya biashara ambayo hata asiyesoma anaweza kufanya

Ni aibu msomi kufanya biashara ambayo hata asiyesoma anaweza kufanya

Msomi hata msoma magazeti ni masomi

Nadhan ungeweka "mtu alie elimika instead of msomi"
 
Wasomi Vijana, mliosoma elimu kubwa za madigrii na Masta tumekosa ubunifu hakika.
Yashangaza sana, Kijana umesoma IT, Umesoma Engeneering, Uhasibu eti unakuja Mtaani unawaza Kufunga Banda la Chips, sijui Kulima matikiti mara duka la vipodozi ni aibu kubwa.

Haiwezekani, Msomi elie elimika unashindwa kuja na mawazo mbadala ya kusaidia Jamii, kuja na mawazo mapya, kuja na Idea za kisomi, mwishoe umepata ajira unachukua mkopo alafu unawaza kufungua duka la Nguo???

Kibaya sio kufanya biashara hizo hapo nilizosema, kinachosikitisha ni kwamba unazifanya biashara hizo kama mtu ambae hajasoma, hakuna kipya wala ubunifu yani ni vuluvulu tu.

Mimi nashangaa sana, Msomi mzima unawekeza milioni 20 kwenye duka la nguo kama la Mangi ambae kaishia la saba na unaifanya biashara hiyo kama yeye?


Nimeikubali Idea ya Benjamin Fernandez, yule jamaa aliyemaliza Stanford university, kaja na Idea ambayo zilikuwepo lakini kaboresha kidogo na sasa ni mwendo wa kupiga pesa tu.

Embu tuacheni Idea za Ajabu, sijui kulima tikiti, sijui juisi ya Muwa, tuje na Idea solid ambayo asilimia kubwa inakuwa ni service business na sio manufacturing ambazo asilimia kubwa ni hasara tu.

Nakaribisha majadiliano,
Wewe umewekeza kwenye idea gani?tuanzie hapo
 
Wasomi Vijana, mliosoma elimu kubwa za madigrii na Masta tumekosa ubunifu hakika.
Yashangaza sana, Kijana umesoma IT, Umesoma Engeneering, Uhasibu eti unakuja Mtaani unawaza Kufunga Banda la Chips, sijui Kulima matikiti mara duka la vipodozi ni aibu kubwa.

Haiwezekani, Msomi elie elimika unashindwa kuja na mawazo mbadala ya kusaidia Jamii, kuja na mawazo mapya, kuja na Idea za kisomi, mwishoe umepata ajira unachukua mkopo alafu unawaza kufungua duka la Nguo???

Kibaya sio kufanya biashara hizo hapo nilizosema, kinachosikitisha ni kwamba unazifanya biashara hizo kama mtu ambae hajasoma, hakuna kipya wala ubunifu yani ni vuluvulu tu.

Mimi nashangaa sana, Msomi mzima unawekeza milioni 20 kwenye duka la nguo kama la Mangi ambae kaishia la saba na unaifanya biashara hiyo kama yeye?


Nimeikubali Idea ya Benjamin Fernandez, yule jamaa aliyemaliza Stanford university, kaja na Idea ambayo zilikuwepo lakini kaboresha kidogo na sasa ni mwendo wa kupiga pesa tu.

Embu tuacheni Idea za Ajabu, sijui kulima tikiti, sijui juisi ya Muwa, tuje na Idea solid ambayo asilimia kubwa inakuwa ni service business na sio manufacturing ambazo asilimia kubwa ni hasara tu.

Nakaribisha majadiliano,
Mimi nimekuelewa vizuri sana mkuu.

Ukosefu wa UMOJA, UBUNIFU na UGUNDUZI ni tatizo kubwa sana kwa waafrika weusi, hasa wa kusini mwa jangwa la sahara.

Mark Zuckenberg, mwanzilishi wa Oracle, na kampuni zingine zimegunduliwa na wanafunzi wa kawaida kabisa ambao wameamua kuwa TOFAUTI na wengine.

Sisi kosa letu tuna tabia ya kuiga na kufanya biashara kwa mazoea.

Tukisikia biashara flan mpya inalipa tunakimbilia huko na hatufanyi kwa ufanisi pia.



KWA MFANO:-

Ilianza :

- Ufugaji wa kware

- Ufugaji wa kuku aiba ya Israel, sasso, malawi n.k

-Ufugaji wa Sungura

- Ufugaji wa nguruwe

- kilimo cha vitunguu na matikiti

Zote ni biashara nzuri ila watu wengi saana wakakimbilia huko ila wachache sana wamefanya kwa ufanisi.

Wengi hatuna UBUNIFU, na wasomi walipaswa wawe tofauti kiufanisi sana na wasiosoma.
 
Me naona sio mbaya msomi kufanya biashara moja na asiyesoma ila ubunifu wako ndio utakuweka tofauti na Hugo ambae hajasoma .Pia baada ya miaka kadhaa utakua wap na umebadilika kiac gani na kuboresha biashara yako na kuwa na tofauti hta mteja wako akija anajua kabsa hpa na pata huduma tofauti na bora kabsa
 
Mleta mada inaoneokana hujui maana ya kukimbiza fursa!

Gradueti hawezi kuacha kuwekeza kwenye kitu chenye transaction na kuwekeza ktk mambo ambayo hayawezi hata kumpa kula kisa tu amesoma.
 
Mkuu,

Suluhisho nimeweka, Tuwaze kufanya vitu kwa utofauti, yani kama ni biashara ya chips basi fanya kama KFC ambayo unafanya tena kwa utofauti, sio unafungua banda la chips kama la mluguru wa pale buguruni
Hakuna asiyependa kununua kitu kipya kutoka dukani tatizo pesa.

Hivyohivyo hakuna asiyependa kuwa na kitu kama KFC, McDonald's nk tatizo mtaji boss.
 
Mimi sioni tatizo akiamua kufanya hata hizo, ila baada ya miaka 5 asiwe kama muuza chips au mlima tikiti wa kawaida.

Sio kila msomi atakua na resource za kumuwezesha kuanzia juu...

msomi na asiyesoma wakiwa wanafanya kitu kimoja nategemea vision na realization zao zitakua tofauti
Fact, Logic, Point.

Nikweli kabisa mtoa mada angalia Focus sio unachokiona kwasasa uyo KFC nani wote hawakuanza huko.
 
Aisee,
Watu wana ela ila hawajui pakuziweka,
kwa mtu ambae ni mjasiriamali na anapenda kufanya hivyo,
akiwa na idea iliyosimama ela zipo mkuu,

watu wanaandika pepa, wanashindanisha idea, wanazipeleka kwa masponser na ena zinamwagaa.

hao akina Zurckeberg na bill Gates hawakuwa na ela, bali walifanya watu wakaona na wakaeka ela
Bill Gates, Richard yule mmiliki wa Virgin companies hawakufika hata hiyo degree ya kwanza. Usiwaweke kwenye hilo fungo lako tafadhari. Deal na hao unaotaka kuwafunda.
 
Back
Top Bottom