GreatDini ni taratibu walizojiwekea wanadamu wakijaribu kumtafuta Mungu. Huwa wanatumia akili kumtafuta Mungu.
Kristo hakuleta dini duniani, Bali wokovu. Alikuja kutuokoa tuliopotea. Kristo alipokuja alikuta dini duniani za Kiyahudi - Mafarisayo na Masadukayo. Watu Hawa wa dini hawakuwa wanamwelewa Kristo. Hata leo watu wa dini huwa hawamwelewi Kristo.
Fuata hiyo Sala ya mtumishi Setfree hapo juu kwa kumaanisha kisha utapokea Wokovu na Roho wa Mungu atakufunulia mengi ambayo akili yako kamwe haiwezi kuyaelewa!
karibu kwenye ufalme
Ajabu weng wao ni wakristo so church totally fail to play its role.Ungekuwa unasoma Biblia usingekosa majibu ya maswali yako. Biblia inaeleza wazi hizi ni siku za mwisho ndio sababu maadili yameporomoka. Ukisoma 2 Tim 3:1-2 imeandikwa hivi:
"Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo..."
JESUS IS COMING SOON, REPENT OF YOUR SINS BEFORE IT'S TOO LATE.
Inaonekana wewe ulisoma vitabu vya Karl Marx kwa juu juu.Sidhani kama utakuwa sahihi, mtu kama karl marx aliitendea haki phd yake kwa kujenga hoja ambazo mpka leo zinaesha mashiko yake (marx's theories of life) sasa hapa bongo kuna phd ngapi tumezipa kazi serikalini na hakuna cha maana? Hao una haki ya kuwaita wapumbafu
Kwanza jiulize, wewe unayo PhD?Kuna watu wana elimu ya juu kabisa, wana PhD, lakini ni wapumbavu wa kutupwa. Hebu leo tuangalie baadhi yao:
Richard Dawkins (PhD in Biology). Huyu ameshinda tuzo nyingi kwa kazi zake za sayansi, lakini anatumia muda mwingi kuhubiri kuwa Mungu hayupo. Anasema maisha yalitokea kwa bahati tu!
Lawrence Krauss (PhD in Theoretical Physics) - ameandika kitabu "A Universe from Nothing," akidai eti the universe can originate without a divine creator. Katika kitabu hicho, hana hoja za maana, anazungusha zungusha tu maneno.
Karl Marx (PhD in Philosophy). Huyu alikuwa staunch atheist. Ndiye aliyepandikiza sumu ya Ukomunisti, akifundisha kwamba dini ni "opium ya watu." Matokeo yake? Mamilioni walikufa kwa sababu ya mawazo yake potofu.
Hao watu Mungu anawaita “Wapumbavu”
"Wapumbavu hujisemea moyoni: “Hakuna Mungu.” – Zaburi 14:1(BHN)
Kumbe mtu anaweza kuwa na PhD, lakini kama anadai kwamba Mungu hayupo, mtu huyo ni MPUMBAVU kabisa mbele za Mungu.
Mungu kama anakuita Mpumbavu, unatarajia nini?
hilo neno la mungu unalojua wewe liliandikwa na nani? si na binaadamu? una uhakika gani mungu yupo hadi useme mungu mwenyewe aliwaita watu wapumbavu?Aliyeanza kuwaita hivyo ni Mungu. Mimi nime-quote Neno la Mungu. Ni wapumbavu kwa sababu PhD zao haziwezi hata kuzuia wasizeeke.
sawa sasa kama dini ni utaratibu wa mwanadamu kumtafuta Mungu, je, huo utaratibu unakubalika mbele za Mungu au haukubaliki?Dini ni taratibu walizojiwekea wanadamu wakijaribu kumtafuta Mungu. Huwa wanatumia akili kumtafuta Mungu.
Kristo hakuleta dini duniani, Bali wokovu. Alikuja kutuokoa tuliopotea. Kristo alipokuja alikuta dini duniani za Kiyahudi - Mafarisayo na Masadukayo. Watu Hawa wa dini hawakuwa wanamwelewa Kristo. Hata leo watu wa dini huwa hawamwelewi Kristo.
Fuata hiyo Sala ya mtumishi Setfree hapo juu kwa kumaanisha kisha utapokea Wokovu na Roho wa Mungu atakufunulia mengi ambayo akili yako kamwe haiwezi kuyaelewa!
karibu kwenye ufalme
Karl Marx alisema "hakuna Mungu" sasa hivi yuko mavumbini. Angekuwa ana akili nyingi angeweza kuzuia Neno hili alilosema Mungu lisitimie:Kugundua kuwa hakuna Mungu nayo ni akili ya hali ya juu.
Kwa Dunia ya Sasa ukisema hakuna MUNGU wewe ni mpumbavu kabisa hatakama ni mwanasayansi mwenyewe professorial, nitakuuliza unipe sayansi ya kiwete kutembea Kwa Maombi ya siku Moja na bubu kuongea Kwa siku Moja bila dawa ya aina yeyote.Upumbavu halali wa Bertrand Russel na Schellenberg kuhusu uwepo wa Mungu
View attachment 3267441
Setfree, amejenga hoja ifuatayo:
Lakini, napendekeza kwamba hoja yake ni batili kwa sababu dokezo la kwanza halikubaliki, maana halina ukweli wowote.
- Mtu mwenye PhD, na anayedai kwamba Mungu hayupo, anakuwa ni MPUMBAVU kabisa.
- Kuna watu wana elimu ya juu kabisa, wana PhD, wanasema kwamba "Hakuna Mungu," wakiwemo kina Richard Dawkins, Lawrence Krauss, Karl Marx, na Bertrand Russel.
- Kwa hiyo, watu hawa ni "wapumbavu wa kutupwa."
Natumia mfano wa "wapumbavu" wawili, mmojawapo wa Uingereza na mwingine wa Ujerumani, kuonyesha kwamba dokezo lako la kwanza ni batili.
Bertrand Russel (Uingereza) alisema kuwa siku ya kiyama Mungu atajapokuja kuwahukumu watu wote yeye atajitetea hivi:
Bwana Mungu, nilijua haupo maana ushahidi uliokuwa hapa duniani haukuwa unatosha kuthibitisha uwepo wako mahali popote duniani.
Kisha Russel akaongeza kusema atamwuliza:
Bwana Mungu, kwa nini siku zote umekuwa unajificha kiasi hiki kama wezi, majambazi, wala rushwa, wazinzi na wahalifu awengine ambao hukimbia macho ya watu?
Hoja ya Russel inao muundo wa kimantiki ufuatao:
Hoja hii inaweza kupewa muundo mbadala ufuatao:
- If God exists, then nonbelief should not occur, meaning that, it would be impossible for people to disbelieve in him (incompatibility premise).
- But, nonbelief phenomenon specified in the above premise occurs in the actual world (existential premise).
- Therefore, deductively, it follows that, God does not exist.
Hoja ya Russel iliungwa mkono na Wlter Schellenberg wa Ujerumani aliyeboresha hoja ya Russel kama ifuatavyo"
- If nonbelief exists then, probably, God does not (improbability premise).
- Nonbelief probably exists (probability premise).
- Therefore, inductively, it follows that, God probably does not exist.
Mpaka hapo ili "upumbavu" wa kina Russel na Schellenberg anaouongelea Setfree ukubalike kwa wasomaji makini inabidi aonyeshe ubovu wa hoja zao hapo juu. Hajafanya hivyo.
- Necessarily, if God exists, anyone who is (i) not resisting God and (ii) capable of meaningful conscious relationship with God is also (iii) in a position to participate in such relationship (able to do so just by trying).
- Necessarily, one is at a time in a position to participate in meaningful conscious relationship with God only if at that time one believes that God exists.
- Necessarily, if God exists, anyone who is (i) not resisting God and (ii) capable of meaningful conscious relationship with God also (iii) believes that God exists. (From 1 and 2)
- There are (and often have been) people who are (i) not resisting God and (ii) capable of meaningful conscious relationship with God without also (iii) believing that God exists.
- God does not exist
Kwa hiyo, Setfree ajue kwamba siku akienda kuwahubiria watu wenye uelewa mkubwa kuliko yeye kama vile kina Russel lazima azabwe vibao kama hiyo jamaa hapo chini.
View attachment 3267240
Unawaongelea kiwete na kiziwi gani, waliopona lini, wapi na walipona kwa sababu ya kitu gani?Kwa Dunia ya Sasa ukisema hakuna MUNGU wewe ni mpumbavu kabisa hatakama ni mwanasayansi mwenyewe professorial, nitakuuliza unipe sayansi ya kiwete kutembea Kwa Maombi ya siku Moja na bubu kuongea Kwa siku Moja bila dawa ya aina yeyote.
Whether Mungu, MUNGU, muNGU, MUngu, mungu, nk bado maana ni ile ile. Wewe kama unaitwa Juma, mtu akiandika jina lako juma utalikataa kisa hajaweka herufi kubwa nwanzoni? Hapa tunaangalia mantiki, sio uandishi wa herufi.Jifunze kutofautisha kati ya mungu na Mungu.
Mathayo 15:30-31:Unawaongelea kiwete na kiziwi gani, waliopona lini, wapi na kwa njia gani?