babukijana
JF-Expert Member
- Jul 21, 2009
- 14,478
- 18,341
Siku hizi,maana tuliwai kaa siku 2 njia hiyo dom-ira.Dereva alikuwa anaitwa Shafii. Yalikuwa ni Leyland na barabara ilikuwa vumbi tupu. Dodoma Saa 12 asubuhi-Iringa saa 1 jioni.
Iyo chuma ndio uifumanie siku iyo hAizingui mbona utakuwa unalipanda kila siku........masaa ya mbele iyo inaitwaMkuu umenikumbusha siku moja tulikua na safari ya kikazi Arusha - Nzega sasa tulikua wanne na bosi wetu tukamuomba mmoja wetu akatukatie tiketi basi zuri. Jamaa akatuambia kakata Mghamba full luxury tutaenjoy wenyewe...!
Advataiz inaanza siku ya safari tulikua tuondoke saa 1 asubuhi. Tumefika stendi basi halipo. Kuuliza uliza pale tukaambiwa tuwe wapole linakuja mda si mrefu. Mabasi yote ya njia hiyo yameondoka sisi tupo tu, saa mbili, saa tatu, saa nne..!
Mara ghafla tunaona ngarangara moja la kutisha linaingia sisi wala hatukuhangaika nalo tukawa tunaendelea na stori tukajua ni yale mabasi yanayoenda King'ori na Ngarenanyuki huko. Cha ajabu tunasikia jamaa anaita "Haya haya wale wa Singida, Nzega mpaka Kahama chuma hicho apo...!! Hatukutaka kuamini tulichokua tunasikia. Wote tulibadilika rangi pale, tukaanza kugomba ila ndio hivyo hatuna cha kufanya. Aisee ile safari ilikua ya hovyo sana mpaka tunafika hatukua na hamu.View attachment 2223836
Dar luxKwasababu zakibiashara na huenda sasa hivi wamebadilika hivyo sitawataja, wanabrand ya rangi Blue na ofisi zao pale Shekilango..hawa watu walitutoa Ubungo saa sita mchana kwenda kahama badala ya saa 12 asubuhi.
Kuna saratoga DKB AKA sukari yao, dereva alikuwa anapiga mashine mpaka walimfungiaAisee hivi mmegundua magari ya kigoma hayapati ajali Sana au bado hamjagundua?
Madereva wake wengi ninwastaarab wanakimbia inapobidi wanafata sheria mara nyingi. Safari ndefu wanajua hata wakikimbia watalala njiani Tabora kwa Safari ya kutoka dar.
Nb
Zibgatia neno wengi.
Kuna bus moja linatoka Mwanza kuja Mbeya! Bus lina kunguni hiloo.Bus gani umewah panda na ukajutia safari yako.
Ipo mkuu imebakia moja nilipanda inatokea swanga - dar ila ndani siti zimechoka yani ukipanda ukifika dar lazima ukajikande mgongo Na diclopar iusikeKampuni ya Sai baba bado nipo? Kwa kweli at their prime, ilikuwa ni kampuni nzuri na marcopolo zao zile wakati ule ndiyo fashion
Kwanza majinja body lake ni la kuchongea pia injini ni za scania mkuu[emoji16]Basi la majinja nilipanda baada ya kushuka kwenye private car kutokea ruaha mbuyuni,nilipandia moro likiwa limetoka sumbawanga nilikalishwa kwenye corridor ya basi juu ya ndoo ya plastic nilikuwa very disgusted lakini nikajipa moyo "bora nimepandia moro" !
Dah hili bus nikiwahi kumpakia manzi yangu analudi kwake kahama si likazingua njiani[emoji81][emoji38] daah kahama walifika saa 8 usiku.Arizona DAR - KIGOMA
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wanaolijua watanisaidia kuelezea sifa zake.
[emoji16][emoji75] kuna bus ukiliona tu kwa nje unajisemea hapa hamna gariKikubwa kufika salama,, uzuri nakerwa sana nikishuka yameisha ila km mliniudhi sana siwarudii,, sasa usiombe uwe unaenda vijijini ndani huko magari ya huko ndo balaa kamili acheni haya ya kupita barabara kuu na yanaoishia makao makuu ya mikoa,, Tanzania tuna shida nyingi sana acheni tu, nimezunguka mikoa mingi kiasi chake nchi hii, CCM Mungu anawaona aisee
Basi zuri na huduma nzuri ni Asante Rabi luxury Arusha-Mwanza,, sitawasahau hawa watu mkinisoma hapa msibadilike jameni,, safari yangu ile nilitamani tusifike yani ilikuwa raha juu ya raha, basi zuri na safi, lugha nzuri wahudumu wasafi mdada mzuri hana kitambi anaongea km anabembeleza, (ningekuwa dume ningetupa ndoano) mwendo poa, makulaji yao sasa full burudani, filamu za kijanja sio za kichina na mkojani
Allys star zinazotamba saivi ni mbili kuna allys nyuma imeandikwa last card na ile nyuma imeandikwa rockcity zinatoka dar kama unataka kuwahi kufika panda izo ni zinatembea balaa.Ally's Mwanza - Dar. Ile safari sitakaa niisahau, gari ilikua imepulizwa Manukato flani yaliyokua yanatoa harufu mbaya sana yani nilikereketwa mwanzo hadi mwisho wa safari, nilipata tabu sana, nilifika Dar nikiwa hoi bin tahabani