Ni basi gani uliwahi panda ukajuta na ukasema hutokaa ulipande tena?

Ni basi gani uliwahi panda ukajuta na ukasema hutokaa ulipande tena?

Ally's, Dar-MwanzaBasi zuri sio yutong Wala marcopolo,sijui Subaru Ile khaaaa ......Dereva kijana wa kiarabu anakula majani Kama mbuzi ,,hakuna Sala niliacha kuomba hiyo siku

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hii gari niliwahi kupanda dereva akiwa huyo muarabu yani anamwaga moto balaa
 
Nyingne complex ya dar to mwanza nasikia sasa hv wanafugia mbuzi
Gari limetoka dar na vioo vyote kila tukipga tuta kioo kinadondoka kufika mwanza vimebaki vioo 3 [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] hapo sjagusia maliasili(kunguni) na ubovu wa gari. Speed kobe safari siku 2
 
Al hushoom kutoka Moro kwenda Dodoma enzi hizo tulitoka moro asubuhi tukafika dodoma usiku.

Usisingizie tochi kipindi hiko kulikuwa hakuna tochi wala vibao vya 50. Gari inasimama kila kituo kupakia abiria dakawa, turiani, sijui dumila kote huko linasimama.

Sijui hii kampuni kama bado lipo.

Ipo mzee [emoji23]
 
Kwasababu zakibiashara na huenda sasa hivi wamebadilika hivyo sitawataja, wanabrand ya rangi Blue na ofisi zao pale Shekilango..hawa watu walitutoa Ubungo saa sita mchana kwenda kahama badala ya saa 12 asubuhi.

Darlux
 
Abood Mneya niliingia saa 6,hizi gari za kudandia tu unakata ticket ndani hazifai kabisa
 
Harambee, Sai baba zote za Dar to Arusha
Misungwi, ilikuwa inaenda Nachingwea sijui kama bado ipo. Enzi hizo mpaka Ndanda tulitumia siku 4 kamili.
 
Muingeze na rafiki yake Harambee, sijui kama bado yupo barabarani. Gari ilikuwa inavuja, aliyeko nje ana afadhali [emoji23]
Falcon inabidi upande na mwamvuli kwenye basi,goma mvua ikinyesha linavuja balaa hawa waarabu wanaungaunga sana!
 
Muingeze na rafiki yake Harambee, sijui kama bado yupo barabarani. Gari ilikuwa inavuja, aliyeko nje ana afadhali [emoji23]
🤣🤣 Harambee bado ipo
Ars - Dar
Gari mvua ikinyesha inavuja kama upo chini ya mwembe
 
Hizo sijui simba mtoto nishapakia kutoka korogwe to moshi aisee sehemu ya masaa 4 tulitumia masaa 7. Kidogo nilipanda kapricom nilifurahi kwanza zinatembea vzr afu safi ndani angalau.

Na majuzi nilipanda gari moja toka dodoma to dar Mungu wangu ile ni dala dala. Sema jina siku imake vzr ila hapana ile gari ni ya hovyo.
Nilipandaga New Force zipo vzr. Kuna gari za kutoka Dom to Njombe aisee ile gari jina nimesahau haahh gari inaharibika kila kituo. Mpaka tukahamishiwa kampuni zingine.
 
Back
Top Bottom