Ni basi gani uliwahi panda ukajuta na ukasema hutokaa ulipande tena?

Ni basi gani uliwahi panda ukajuta na ukasema hutokaa ulipande tena?

Ukipanda basi mwite konda muulize hivi sehemu fulani tunafika saa ngapi? Akikujibu hivi “ hivi ni vyombo vya moto tuombe tu Mungu jua tayari umepatikana,
au ukisikia inategemea barabarani kukoje

mimi nilipanda basi linaitwa simba mtoto natoka TANGA naja DAR
nilichelewa nikakuta RATCO ishajaa
na basi ya mwisho ndio hiyo SIMBA MTOTO
huweziami i ile basi inatembea na FUNDI
Kutoka saa 11 tanga tumefika UBUNGO saa 8 usiku kilaa baada kilometer kadhaa FUNDI anashuka chini Uvunguni

nikahapa sitapanda lile basi tena
 
Mwaka 2014 kwa mara ya kwanza kwenda moshi .imefika saa sita mchana inatakiwa nirudi darkesho,nikaforce nisilipe hotel niondoke siku hiyo hiyo.nilipanda za kenya kuja dar kama sikosei ni Akida.basi tulifika kariakoo saa saba usiku.yaani wao ni mizigo na kupekuliwa pekuliwa. Karibu kila maeneo ya ukaguzi plus taarifa kuwa wanalala njiani hawalali hotelin bongo.mara ya pili tahmeed la kutoka kenya kupitia tanga hadi dar .nalo flilipata ukaguzi plus .
 
NEW FORCE.. sitapanda kwa sababu si waaminifu. Niliagiza parcel flan hv from dar to tukuyu, lakin baada ya mzigo kufika tukuyu wakaanza kunipiga chenga akat mzigo ulishalipiwa kila kitu. Nmekereka mpaka leo.
 
Kampuni ya Sai baba bado nipo? Kwa kweli at their prime, ilikuwa ni kampuni nzuri na marcopolo zao zile wakati ule ndiyo fashion
Nazionaga bado zipo but kuzipanda hapana.
Huwa zinasimama hovyo njiani haziachi abitlria hata wa 2,000!
 
Simba Mtoto ya kutoka Tanga kwenda Dodoma! Ilibakia kidogo tu itumwage Mto Wami baada ya break kufail.

Nilijalaumu sana imekuwaje nikapanda gari bovu kiasi kile! Siku hizi huwa napanda Nacharo tu. Nikikosa siti bora nikapanda hataTashrif! Ila siyo Simba Mtoto!
Tate niko njiani hapa natoka Tanga, yaan naona wengi wanasema Nacharo, Tashriff au Ratco ndio yako vizuri,
 
Tate niko njiani hapa natoka Tanga, yaan naona wengi wanasema Nacharo, Tashriff au Ratco ndio yako vizuri,
Na huo ndiyo ukweli mchungu. Biashara ya usafirishaji inahitaji uwekezaji. Nunua magari mazuri, maada ya miaka michache uza, nunua mengine!

Sasa Simba Mtoto na Raha Leo sijui hela wanapeleka wapi! Kwa sasa hawana tofauti na akina Shambalai! Yaani kuna Simba Mtoto moja ya Tanga - Dodoma, ina siti za 2 by 3! Si dharau hizi kwa watu wa Jiji la Dodoma!
 
Daah manina back 2010 nilikuwa dodoma nikawa na safari ya haraka mida ya saa 8 mchana, chaap kurudi dar, sina gari binafsi nikazama kituoni pale nyuma ya shabiby nikakutana na chuma imetoka singida jamaa kanikatisha ticket mapema kashasepa

Baada ya gari kufika nimepanda kwa kweli nipata chafya pale pale, nkasema hapa natoboa hivi hivi, daah naenda kwenye siti yangu, konda akaniambia huku hamna cha mambo ya siti subiri mtu akishuka ukae, baada ya ku mind sana na kutaka kuleta ubabe abiria kadhaa wakasema wanashuka soon...

Lile gari lilikuwa linanuka harufu ya mavi ya kuku, na mbuzi, kelele mtindo mmoja, siti za chuma viti cushions zimezama kwa chini unazama ukikaa, aisee nilipata tabu sana mnaishi na kuku na mbuzi ndani ya bus, ilibidi niombe msaada kwa shangazi yangu pale gairo akanipa rav 4, yake nikawahi nilicholuwa ninawahi maana gari lenyewe lilizingua kabla hatujafika gairo namsikia konda anasema hapa mbombo ngafu[emoji28]...nkajua hii hatutoboi

Ya pili, nilitoka dsm kwenda dodoma 2009 nikapanda gari flani linaonekana Luxury sana hawa jamaa walikuwa na ma bus yao pale makonde mbezi beach ya kisasa wameyatoa ulaya, daah nilitumia masaa 17...kila baada ya kilometres kadhaa gari inachemsha [emoji23]

Kwa safari zangu za bus ni kilimanjaro na shabiby, i tried al saedy, dar lux na kidia ila hawa kwa sasa hivi nikikosa seat ni afadhali niruke na ungo

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji119] atali mkuu
 
Niliwahi kupanda kimbinyiko, ilikua Dar-Dodoma. Kama ningeondoka na baskeli, wangekuta nishafika Dodoma dadek zao. Maana nilitoka Dar saa nane, nikafika Dom saa sita usiku!

Aisee ilo bus lilikua likitembea au linanyata [emoji23]
 
Back
Top Bottom